Mtazamo wangu kuhusu wabunge wa UKAWA Kuzomea bungeni

Mti wa Chuma

JF-Expert Member
Jul 2, 2015
331
99
Bunge la 11liliingia siku yake ya nne (4) Ijumaa ambapo ilikuwa siku maalum kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kuhutubia bunge na kufungua rasmi. Kabla ya Mh. Magufuli hajaingia wabunge wa upinzani wanaounda UKAWA walianza kupiga makelele wakimtaja Maalim Seif wa Zanzibar. Hali hiyo ilimlazimu spika wa bunge Job Ndugai kuamuru watoke nje baada ya kuwataka watulie lakini hawakufanya hivyo.
Cha kujiuliza; Walichaguliwa na wananchi kwenda bungeni kufanya vitu vya ajabu?

UKAWA sioni wanachodai hadi kupiga makelele ndani ya ukumbi tukufu la bunge. Katika kufuatilia kwangu kwa undani zaidi kuna mtu nyuma ya wabunge wa UKAWA, na si wote wanapenda kufanya fujo (kupiga kelele).

Kwa mtazamo wangu UKAWA inakoelekea watapoteza mwelekeo pia watakosa matumaini kwa wananchi, uchochezi huu huchangiwa na viongozi wakubwa wa vyama vinavyounda UKAWA. Cha kushangaza hata sheria inayozungumzia ukomo wa kipindi cha Rais Zanzibar wanapindisha.
Kwa mtazamo wangu UKAWA muda si mrefu watatengana.
 
Naheshimu mtazamo wako huo, ila kwakua tuko wachanga sana kisiasa hamtaelewa kilichofanyika na impact yake kwa Jamii ya kimataifa, kwamba kinachofanyika Zanzibar sio sahihi na kwamba Ccm wamevunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Walichaguliwa na wananchi sio wakashangilie upuuzi wa serikali ya ccm, Walichaguliwa ili wapinge dhuluma na uonevu dhidi ya Watanzania wote na jana walipinga. ASANTENI UKAWA.
 
Kinachopindishwa Zanzibar ni kipi ndugu yangu? Mbona suala la Zanzibar halihitaji kua na akili za ziada? Kama hata hili la Zanzibar unaliunga mkono basi kuna tatizo mahali, kuna tatizo lazima.
 
Unaandika kanakwamba ulikufa na ulivyofufuka tu ukakuta zomeazomea bungeni. Jifunze kufikiri na kutafakari chanzo cha tatizo. Unapowanyang'anya watu haki zao za msingi ulitarajia watakuchekea.
 
Kwa sasa UKAWW hawana tena ajenda ya kujinadi kwa wananchi. Wamebaki kushikilia bango suala la Zanzibar tu kama mtaji wao wa kutokea
 
Bunge ni mojawapo ya mihimili ya taifa. Sio lazima waongelee majimbo yao tu muda wote. Wakiungana kupigania haki ipatikane katika taifa tunafurahi wanawakilisha kilio cha zaidi ya asilimia 60 ya wananchi.
Kinachofurahisha zaidi ni kwamba comments za wananchi wengi juu ya maamuzi ya UKAWA ni negativu. Ka kweli wananchi wengi huku mitaani wanalaani sana walichofanya ukawa jana. Nimepita jana mitaa kadhaa kama Mfaranyaki, Bombambili, Makambi, Mateka, Mjimwema, Matarawe, hapa Lizaboni, Lilambo na kwingineko hakika wananchi wamekasirishwa sana na walichofanya UKAWA
 
Hatukuwatuma bungeni kwenda kuichekwa serikali, tuliwatima kwenda kuishauri na kuionya serikali, tiliwatuma kwenda kupigania haki zetu na si kukandamiza haki zetu, na pale haki zetu zinapopokwa watumie kila namna na hata ikibidi kupigana tu kwani hatukuwapeleka pale kwenda kula na kushangaa. Hongera ukawa
 
Unaandika kanakwamba ulikufa na ulivyofufuka tu ukakuta zomeazomea bungeni. Jifunze kufikiri na kutafakari chanzo cha tatizo. Unapowanyang'anya watu haki zao za msingi ulitarajia watakuchekea.



Mkuu mimi si mgeni ndani ya nchi yangu. Ufumbuzi wa tatizo si kupiga makelele kama watoto wadogo bali ni kupatia tatizo usuluhisho.
 
pole sana kwa kuwa hujui na labda hujawahi kufuatilia mabunge ya nchi nyingine nini huwa kinafanyika. Kwa jamii ya watu kama wewe itatuchukua miaka mingi sana kupata haki zetu za msingi na demokrasia ya kweli katika nchi hii.
 
Hatukuwatuma bungeni kwenda kuichekwa serikali, tuliwatima kwenda kuishauri na kuionya serikali, tiliwatuma kwenda kupigania haki zetu na si kukandamiza haki zetu, na pale haki zetu zinapopokwa watumie kila namna na hata ikibidi kupigana tu kwani hatukuwapeleka pale kwenda kula na kushangaa. Hongera ukawa



Kupigana ndo haki ipatikane?
 
Kinachofurahisha zaidi ni kwamba comments za wananchi wengi juu ya maamuzi ya UKAWA ni negativu. Ka kweli wananchi wengi huku mitaani wanalaani sana walichofanya ukawa jana. Nimepita jana mitaa kadhaa kama Mfaranyaki, Bombambili, Makambi, Mateka, Mjimwema, Matarawe, hapa Lizaboni, Lilambo na kwingineko hakika wananchi wamekasirishwa sana na walichofanya UKAWA
Hata mimi nilikasirishwa kwanini waliwahi kutoka nje, nilitaka waendelee kudai haki mpaka mwisho.
 
Kwa sasa UKAWW hawana tena ajenda ya kujinadi kwa wananchi. Wamebaki kushikilia bango suala la Zanzibar tu kama mtaji wao wa kutokea

Acha ushabiki wa kijinga. Mambo ya Zanzibar usiyachukulie kirahisi kiasi hicho kisa buku 7 unazopewa. Big up Ukawa.
 
Wananchi wa songea mji huku kwetu wamepongezi maamuzi ya ukawa kwa maana wamechoka na unyanyasaji wa ccm

Hivi unaweza tueleza sababu ya uchaguzi znz kufutwa ilihali walishatangaza majimbo 31?
 
likiisha la zanzibar, huku magufuli kakamata hja zao zote

wenye akili tu bunge hil ndio wata shine
 
Wananchi wa songea mji huku kwetu wamepongezi maamuzi ya ukawa kwa maana wamechoka na unyanyasaji wa ccm

Hivi unaweza tueleza sababu ya uchaguzi znz kufutwa ilihali walishatangaza majimbo 31?



Tayari imeshafutwa, hii imepita.
 
Wapiga kura wao tumeridhika kabisa......wale waliowapigia kura CCM hawawezi kufurahi wakiona mabwana wao wakizomewa

Bunge la 11. Iliingia siku yake ya nne (4) ijumaa ambapo ilikuwa sikuu maalum kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kuhutubia bunge na kufungua rasmi. Kabla ya Mh. Magufuli hajaingia wabunge wa upinzani wanaounda UKAWA walianza kupiga makelele wakimtaja Maalim Seif wa Zanzibar. Hali hiyo ilimlazimu spika wa bunge Job Ndugai kuamuru watoke nje baada ya kuwataka watulie lakini hawakufanya hivyo.
Cha kujiuliza; Walichaguliwa na wananchi kwenda bungeni kufanya vitu vya ajabu?
UKAWA sioni wanachodai hadi kupiga makelele ndani ya ukumbi tukufu la bunge. Katika kufuatilia kwangu kwa undani zaidi kuna mtu nyuma ya wabunge wa UKAWA, na si wote wanapenda kufanya fujo (kupiga kelele)
Kwa mtazamo wangu UKAWA nakoelekea watapoteza mwelekeo pia watakosa matumaini kwa wananchi, uchochezi huu huchangiwa na viongozi wakubwa wa vyama vinavyounda UKAWA. Cha kushangaza hata sheria inayozungunzia ukomo wa kipindi cha Rais Zanzibar wanapindisha.
Kwa mtazamo wangu UKAWA muda si mrefu watatengana.
 
Back
Top Bottom