Mtanzania Bingwa wa Dunia

Mtanzania Bingwa wa Dunia

Ongera Ongera ongera FF kwa kumleta Hamisi jukwaani
"Vox populi vox dei"
 
Watanzania hata kumpa hongera huyu kijana? Duh. Au kwa kuwa anaitwa Hamisi?
Acha hasira FaizaFoxy hapo sasa zile hisia za kidini naona zinakutawala, kiukweli huyu kijana ametutoa kimasomaso maana hakuna tunachoshinda kimataifa lakini walau leo tuna cha kujivunia..

Hongera Hamisi, hongera wawezeshaji.. na hongera TANZANIA YETU...
 
Watanzania hata kumpa hongera huyu kijana? Duh. Au kwa kuwa anaitwa Hamisi?
Pamoja na mie kuwa na imani sawa na yako bidada, inaonyesha hawa ndugu zetu si wabaguzi kihivyo maana analelewa na Sister wa kikatoliki! Inaonyesha sisi ndio tunaoanzisha hii jinai. Tujirudi
 
Pamoja na mie kuwa na imani sawa na yako bidada, inaonyesha hawa ndugu zetu si wabaguzi kihivyo maana analelewa na Sister wa kikatoliki! Inaonyesha sisi ndio tunaoanzisha hii jinai. Tujirudi

Hao si wana malengo, uko wapi wewe?
 




Rais Jakaya Kikwete akimpongeza kijana wa Kitanzania Hamisi Mohamed mwenye umri wa miaka 14 aliyeipatia sifa Tanzania kwa kunyakua ubingwa wa Dunia wa mchezo wa kuruka kamba kwenye michuano iliyofanyika huko Orlando, Marekani, mwezi uliopita. Kijana huyo, ambaye awali alilelewa katika kituo cha watoto yatima cha Dogo Dogo Dar es Salaam, alianza kupata mafunzo ya mchezo huo ambapo alishiriki mashindano ya Afrika Mashiriki yaliyofanyika Mombasa na kunyakua Medali ya Dhahabu. Kulia ni mfadhili wa kijana huyo, Amy Canady, na kushoto kwa Rais Kikwete ni Sister Jean Pruitt, mwanzilishi wa kituo cha kule yatima cha Dogodogo Centre

[video=youtube_share;FdifkhentBw]http://youtu.be/FdifkhentBw[/video]

Namuona mtu kama Joti kwenye picha hii.vipi nae kapata shavu nini
 
Hao si wana malengo, uko wapi wewe?
Mie nipo ila nakatishwa tamaa na hawa wana JF ambao ni wanafiki wakubwa kama NAPE kwa kutetea kifo cha Tanganyika. Hii imenifanya nikae pembeni kwani mtu mzima unatetea serikali mbili, haiingii akilini. Chonde chonde kama unamjua Nape mweleze asome majadiliano hapa JF na abadilike.
 
Watanzania hata kumpa hongera huyu kijana? Duh. Au kwa kuwa anaitwa Hamisi?

FaizaFoxy, umeleta habari nzuri sana, na baadhi ya hoja zako huwa zinakua makini sana ila naomba upunguze hisia za kidini, kila mtu anazo ila tunajaribu kubaki nazo binafsi.

Kijana anastahili pongezi tena nasikitika sijaisikia hii habari kwenye vyombo vya habari kama BBC (Huenda waliitangaza lakini sijabahatika kuisikiliza)

Tuwaige wa kenya kwa hili, wanajitahidi sana kuhakikisha wanaweka tofauti zao inapokuja suala la ushiriki wa kimataifa, wangemtangaza sana, kwa kweli hapa kwetu sidhani hata kama habari hii ilipewa umuhimu unaostahili, lazima tubadilike.
 
Last edited by a moderator:
Mie nipo ila nakatishwa tamaa na hawa wana JF ambao ni wanafiki wakubwa kama NAPE kwa kutetea kifo cha Tanganyika. Hii imenifanya nikae pembeni kwani mtu mzima unatetea serikali mbili, haiingii akilini. Chonde chonde kama unamjua Nape mweleze asome majadiliano hapa JF na abadilike.

Kwa hili la kuipoteza Tanganyika hata mimi linaniuma sana. Natumai Nape yumo humu na anakusoma.
 
watanzania hata kumpa hongera huyu kijana? Duh. Au kwa kuwa anaitwa hamisi?
yani w kichwa chako kinawaza udini tuuu kutwa nzima.kwanza umeshanifanya nikuhisi hatakufunga hujafunga..hivi leo ni mfungo ngapi vile?
 
Back
Top Bottom