Mtandao huu wa uhalifu wa wachina ufumuliwe

Mtandao huu wa uhalifu wa wachina ufumuliwe

Wachina ni watu wenye dharau sana aisee


Halafu tusijidanganye eti ni hawa tu wahalifu wachache tulionao hapa ndo wenye dharau, la hasha! Ninavyoona mimi baraka zao zinatoka hukohuko kwao!

Dawa yao ni kutumia sheria za kwao kwa makosa wanayofanya hapa kwetu, maana inaonekana hawa jamaa ni sugu kwa sheria zetu ambazo kwao ni laini sana!
 
Hayo megenge ya kihalifu ya Wachina na Japan yamesambaa dunia nzima na kila nchivwanayoaamia kwa wingi wana hio michezo, mfano Brazil kuna jamii kubwa ya wajapan sasa wana makundi yao ya kihalifu yanasumbua sana lio hakuna biashara hawafanyi kuanzia unga, ngono na nyala za wanyama. Sasa naona hawa wachina waliojaa hapa kwetu wanafukuzia dili za kuuza bidhaa zinazotokana na wanyama na biashara ya ngono. Kuna wengine wamejaa DRC wanafanya biashara ya ngono mpaka wakahojiwa na BBB Swahili wakasema hawawezi kurudi China sababu biashara inalipa sana huko Kinshasa.
 
Kuna wengine mwaka jana kule Dodoma walikutwa wanamiliki kiwanda cha kienyeji cha kusindika nyama ya punda na kuisafirisha kwao.imagine,nyama ya punda!!!
 
Wachina ni wazuri kwa upande mmoja na ni wabaya kwa pande zote hasa ukutane na wale ambao walipishana na shule na pia wakawa wanatokea maeneo ambayo hata barabara hakuna usafiri wao ni wa kamba utajuta
 
Kuna wengine mwaka jana kule Dodoma walikutwa wanamiliki kiwanda cha kienyeji cha kusindika nyama ya punda na kuisafirisha kwao.imagine,nyama ya punda!!!
Si ni kule Ikungi njia ya kwenda Singida nyuma ya ma godown ya Bhanji? Nimekula ile nyama mara 3 kwa siku kwa siku 90 kuanzia supu ya asubuhi roast ya mchana mpaka mchemsho wa jioni...katika siku hizo 90 hakuna siku ambayo ilipita bila kula hiyo nyama ya punda
Kuna wengine mwaka jana kule Dodoma walikutwa wanamiliki kiwanda cha kienyeji cha kusindika nyama ya punda na kuisafirisha kwao.imagine,nyama ya punda!!!
 
SERIKALI IWE MAKINI NA WACHINA WA FU JIAN
sio wachina wote ni wabaya kivile, lakini wachina wa FU JIAN ndio wenye matukio sana ndio maana baadhi ya mataifa wakiangalia mchina husika anatoka huko hawampi visa sisi huku hatujastuka...lakini ndio hawa wengi wanaofanya biashara za kamari hapa nchini

Kisa hiki cha mwaka jana
Kuna mchina alitafuta mabaunsa wa kumlinda (huyu mchina alikuwa na ugomvi na wenzake, wote ni wamiliki wa madanguro, hivyo wakapokonyana wateja)
akapata vijana watatu mabaunsa toka gym moja mwananyamala akawa anatembea nao popote aendapo
Siku moja akiwa na mabaunsa wake akakutana na wale wachina wengine zikapigwa kung fu za kufa mtu lakini wale walipozidiwa walimpiga risasi binti wa huyu mchina mwenye walinzi
Baunsa mmoja kuona vile akataka kumvamia yule mchina mwenye silaha ili ampokonye, aliishia kulishwa risasi 12 mwilini
Hii kesi haikufika popote na Baunsa alizikwa kwao bagamoyo kwa msaada mkubwa wa mchina
Kuna mengi ya wachina jamani
Duuuuuuuuhhhh....inasikitisha aiseeee
 
Imagine Kaka mkubwa Mshana Jr, hadi muda huu nilikuwa nakusubiria uliposema utaendelea. Nikiamka salama, naanza na Jf mengine yatafuata.

Muwe na Usiku Murua.

Ahsante!
 
Imagine Kaka mkubwa Mshana Jr, hadi muda huu nilikuwa nakusubiria uliposema utaendelea. Nikiamka salama, naanza na Jf mengine yatafuata.

Muwe na Usiku Murua.

Ahsante!
....mziki wa uhamiaji ulipoisha ndio ikaanza sasa ule mtafutano na kuwindana mpaka siku walipokutana live na kusababisha kifo cha kijana wetu mtanzania aliyekuwa na ndoto nyingi
Kilipita kipindi cha kama mwezi mzima hivi kila upande ukisikilizia halafu baada ya hapo huyu mmoja akahamishia kambi masaki kwenye ghorofa moja( apartment) sijalitaja lakini kodi ilikuwa usd 2500 kwa mwezi, hapo akaongeza mabinti wengine wawili kwahiyo jumla akawa nao wanne
Huku biashara ikaendelea tena! Kulikuwa na Noa 2 full tinted na vijana wawili madereva , waliokuwa wanafanya kazi mpaka usiku wa manane
Iko hivi kijana anapokea oda toka kwa boss kuwa ampelekee mteja mzigo sehemu fulani akifika huko anamsubiri, akimaliza anapokea tena oda ya kumpeleka kwengine! Hawa mabinti walikuwa na nguvu ya ajabu kwakuwa kwao kulala na wanaume wasiopungua 6 kwa siku ni kitu cha kawaida sana
Mwezi ule ule likaja kundi lingine kwenye ile ghorofa, hawa walipanga floor ya pili wakati wale walipanga floor ya tatu....!
Hapo ukatokea tena mtafaruku mwingine lakini kipindi hiki ikiwa ni mabinti kwa mabinti bila kuwahusisha maboss...ugomvi ulikuwa mkubwa mpaka wa kukatana na visu na kuumizana sana... ..wote wakapewa notice ya saa 48 wawe wamehama....! Ikawa hamna namna wakahama......
Itaendelea
 
Back
Top Bottom