Mtandao huu wa uhalifu wa wachina ufumuliwe

Mtandao huu wa uhalifu wa wachina ufumuliwe

Kwa hiyo hapa ni uhalifu wa wachina dhidi ya wachina, yeah? Well, kama serikali yao haioni tatizo na wala haitu-hold responsible then sioni umuhimu wa kuingilia. Tuna mambo mengi ya msingi ya kufuatilia kwa sasa.
Hujui tu ni kiasi gani tunapoteza vijana wetu kwenye hizi ishu
 
Ila kwenye mada yako umeongelea mabinti wa kichina kuuzwa kwa wachina nchini. Sasa si tunapotezaje vijana wetu?
Mabinti hao hupelekwa maeneo ya kutoa huduma na vijana wetu! Logistics nyingi kwenye ishu za wachina hufanywa na vijana wetu nitakufafanulia vizuri baadae
 
Mtu anakula mijusi na nyok ndo atashindwa kumla binadamu mwenzie hao jamaa ndo mana maandunje nchi nzima

Hao jamaa wamefanya kazi ya kuijaza dunia na sasa wanajipunguza wenyewe
 
Halafu cha ajabu sasa hivi kwenda China huna mtu wa kukupa invitation kwao hukanyagi ila huku kwetu wapo mpaka vichochoroni pengine bila vibali vya kuishi
Ila serikali yetu hii tukufu imekaa kimya
Alooo nimesahau " Wachina wana mapesa mengi wanakopesha hadi Marekani"
 
Naona sasa hivi huu uzi inataka kufungwa, nishahisi dalili maana kila nikiandika inagoma kutuma na wakati nina zaidi ya MB 50 sijajua kama ujumbe huu utafika, nahisi ONYO tayari washapewa wanaomiliki JF.

Jambazi, ungetutupia walau kipengele kimoja kilichosainiwa alipokuja kiongozi wao hao wachina; kile chenye utata plz kama hautajali.

Miss Chaga, sijui upo nje ya nchi ama, nahofia tu usije ukasumbuliwa, ila binafsi nakushukuru sana kwa kunielewesha mambo fulani fulani hapo juu, Mungu, akulinde tu, sema Amina!

Mshana Jr, usalama wako sijui utakuwaje, maana umeleta habari nyeti sana, tena hadi kuwatambua wachina wanaotoka maeneo korofi na wale wa kawaida, nahisi utafatiliwa na tutakukosa humu ukitupa mawazo ya michango yako iliyo makinika, nawe Mungu, aliye juu na akulinde, sema Amina!

Jamani siyo uwoga, ila najikuta tu nikihofia usalama wa hao tajwa juu hapo, hasa lile la baunsa kumiminiwa risasi 12 na haikusikika hata, sasa wale viongozi WAADILIFU wakilisikia hili, watataka lifuatiliwe, kaka mkubwa Mshana Jr, sijui utakuwa wapi. Nawaza tu kwa sauti ya ndani.

Ahsante!
 
Mbona kwenye Uzi wake, kataja vijana wa kike na wa kiume wa kitanzania nao wanahusika kwa namna moja ama nyengine? Mumsome tu vizuri mtamuelewa, na zaidi kasema hapo atafafanua baadae hilo la Logistic.

Nashukuru maelezo yangu yamefika, maana daah nilitoa macho kweli, na ningesikitika kama nilivyosikitika leo muda mfupi uliopita, kuna mwenzetu alileta uzi wa tatizo la kaka'ke kuwa ni shoga, nikaandika maombi na maoni yangu weeee, daah si yakakataliwa aisee, na Jf hakuna mahala pa Ku-save pointi zako ili zikigoma uongeze bando, urudi kuzitupia tena. Kwa kweli iliniuma sana. Na pia Jf hakuna pa ku-like post yako.

Again, Mshana Jr, ahsante kwa hili na mengine mawazo na nyuzi zako, binafsi nakufuatilia sana, hujui tu, hata nisipo-like maelezo yako ila kaa ukijua nakufuatilia sana kwa kuwa najifunza machache mazuri tokea kwako.

Ahsante!
 
Naona sasa hivi huu uzi inataka kufungwa, nishahisi dalili maana kila nikiandika inagoma kutuma na wakati nina zaidi ya MB 50 sijajua kama ujumbe huu utafika, nahisi ONYO tayari washapewa wanaomiliki JF.

Jambazi, ungetutupia walau kipengele kimoja kilichosainiwa alipokuja kiongozi wao hao wachina; kile chenye utata plz kama hautajali.

Miss Chaga, sijui upo nje ya nchi ama, nahofia tu usije ukasumbuliwa, ila binafsi nakushukuru sana kwa kunielewesha mambo fulani fulani hapo juu, Mungu, akulinde tu, sema Amina!

Mshana Jr, usalama wako sijui utakuwaje, maana umeleta habari nyeti sana, tena hadi kuwatambua wachina wanaotoka maeneo korofi na wale wa kawaida, nahisi utafatiliwa na tutakukosa humu ukitupa mawazo ya michango yako iliyo makinika, nawe Mungu, aliye juu na akulinde, sema Amina!

Jamani siyo uwoga, ila najikuta tu nikihofia usalama wa hao tajwa juu hapo, hasa lile la baunsa kumiminiwa risasi 12 na haikusikika hata, sasa wale viongozi WAADILIFU wakilisikia hili, watataka lifuatiliwe, kaka mkubwa Mshana Jr, sijui utakuwa wapi. Nawaza tu kwa sauti ya ndani.

Ahsante!
Kuna mengi bado sijaandika! Nitaandika nikishavuka boda
 
Arusha, kuna mchina alikuwa mkandarasi siku moja asubuhi akakanyagwa na grader, utumbo ukazolewa na beleshi na kazi ikaendelea kama kawa
 
Wameleta madude ya kuchezea kamali yana "nembo za magari" na kuayasambaza hadi huku vijiji vya ndani kabisa, hapa Ng'washilalage ukimwagiza mtoto akununulie kiberiti lazima adumbukize hiyo sh. 200/ kwenye li mashine la mchina ili itage 200 zingine, ikiliwa utamuona anarudi akilia.
Punda zetu ndio kabisa zinaisha!
 
Sawa Kaka mkubwa, ila usalama wako kwanza, hakikisha umevuka zaidi ya mipaka miwili (nchi mbili tofauti), ubadili na nyenzo, ndiyo utuletee mambo aisee.

Ni aibu kwa nchi kuwa katika orodha ya nchi zinazofadhili uhalifu kama huo, eti tunasikia na kuona kwenye vyombo vya habari vya kimataifa, mf; 'watanzania saba na wachina wanne, wafa vifo vya utata, nchini Tanzania. Na inasemekana walikuwa kwenye mtandao wa ..........'. Ni aibu kwa kweli.

Binafsi, huwa najinyamazia tu, maana bado watoto wangu wadogo sana, wanahitaji ukaribu wa baba yao mimi. Ninachofanya ni kuwaombea tu, maana daah!

Ahsante!
 
Hawa jamaa watakuwa na mtandao.
na ningeomba Serikali hawa jamaa warudishwe wakahukumiwe kwao,hahaha,maana najua wakifika tu ni kunyongwa hapo hapo tena uwanjani.Maana raisi wao kapinda

Huu ujinga wanafanya wakiwa huku tu

Hii issue ya biashara ya binaadam wanaifanya saana.Na wizara ifuatilie mtandao wao hawa watu.Kutakuwa na Viongozi wanahusika kwenye dili hizi.Wachina ni waoga saana,ila wakijengewa confidence wanakuwa ni watu hatari saana.
 
Sawa Kaka mkubwa, ila usalama wako kwanza, hakikisha umevuka zaidi ya mipaka miwili (nchi mbili tofauti), ubadili na nyenzo, ndiyo utuletee mambo aisee.

Ni aibu kwa nchi kuwa katika orodha ya nchi zinazofadhili uhalifu kama huo, eti tunasikia na kuona kwenye vyombo vya habari vya kimataifa, mf; 'watanzania saba na wachina wanne, wafa vifo vya utata, nchini Tanzania. Na inasemekana walikuwa kwenye mtandao wa ..........'. Ni aibu kwa kweli.

Binafsi, huwa najinyamazia tu, maana bado watoto wangu wadogo sana, wanahitaji ukaribu wa baba yao mimi. Ninachofanya ni kuwaombea tu, maana daah!

Ahsante!
Mwendelezo wa kilichotokea siku hiyo....niliitwa uhamiaji pale posta (kuna mengi sitayasema hapa kwasababu zilizo wazi)kulikuwa na mchina kakamatwa na kibali bandia cha kuishi nchini, mchina huyo alikuwa ni mwanamke, baada ya mahojiano ya kina ilijulikana kuwa kapatiwa kile kibali na afisa wa pale pale ambaye naye alikamatwa bila kukawia, kufika jioni ya siku ile walikuwa wameshakamatwa watu watano wote wakiwa kwenye mtandao mmoja na wachina kuanzia kutengeneza vibali mpaka mambo ya kuuza wanawake....wote wakapelekwa central polisi kasoro mmoja yule wa uhamiaji
Tuliondoka central police saa tano usiku na kutakiwa kufika pale saa kumi na moja alfajiri kwa ajili ya kumchukua yule mchina na kumpeleka uhamiaji tayari kwa taratibu za repatriation
Nilifika pale 05:40 alfajiri nilikuta maaskari wa zamu pale nikawasabahi na kuamua kuelekea canteen kupata kifungua kinywa, ni wakati naelekea canteen ndio nikamwona yule binti mchina kwenye selo ndogo na kuamua kumsalimia
Kitendo kile kilinifanya niwekwe chini ya ulinzi na kwa haraka sana nikapewa kesi ya kutaka kumtorosha mtuhumiwa...kufika saa 12: 15 asubuhi nilikuwa nimeshapelekwa records kupigwa picha kuchukuliwa alama za vidole , kukabidhi kila kitu kaunta (mkanda viatu saa wallet simu nk na kupewa risiti na kuwekwa kwenye lockup nyuma ya kaunta pale central
Yalitokea mengi kwa muda mfupi sana vitisho vilikuwa vingi sana lakini kufika saa moja asubuhi nilikuwa huru....
Nitaendelea. ...
 
....inaendelea
Yakayokea mengi sana kwa siku ile nzima lakini kufika jioni ya siku ile mchina tayari alikuwa yuko angani
Sasa kumbe huyu binti alikuwa ni mmojawapo wa makahaba na wale wachina maboss walikubaliana wasiwaguse kabisa wale mabinti kuepuka kuleta mgongano wa kimaslahi ila huyu mmoja akashindwa na uzalendo akachukua jumla
Ugomvi ulikuwa mkubwa uliopelekea hawa wanahisa kutengana na mmoja kwenda uhamiaji kuchoma ishu
Hasira za kuchomana zilisababisha ugomvi mkubwa sana na walipigana sana! Mshindwa akakimbia kuchomesha ishu mshindi akaenda kuongeza nguvu ya mabounsa na akatoa angalizo kuwa popote watakapokutana ni kichapo
Haya yote yalifanyika kwenye ardhi ya Tanzania kwa msaada mkubwa wa wazawa kwakuwa kila mchina aliunda kundi lake na watu wake kwenye kila kitu....
Stay tuned more to come.......
 
....inaendelea
Yakayokea mengi sana kwa siku ile nzima lakini kufika jioni ya siku ile mchina tayari alikuwa yuko angani
Sasa kumbe huyu binti alikuwa ni mmojawapo wa makahaba na wale wachina maboss walikubaliana wasiwaguse kabisa wale mabinti kuepuka kuleta mgongano wa kimaslahi ila huyu mmoja akashindwa na uzalendo akachukua jumla
Ugomvi ulikuwa mkubwa uliopelekea hawa wanahisa kutengana na mmoja kwenda uhamiaji kuchoma ishu
Hasira za kuchomana zilisababisha ugomvi mkubwa sana na walipigana sana! Mshindwa akakimbia kuchomesha ishu mshindi akaenda kuongeza nguvu ya mabounsa na akatoa angalizo kuwa popote watakapokutana ni kichapo
Haya yote yalifanyika kwenye ardhi ya Tanzania kwa msaada mkubwa wa wazawa kwakuwa kila mchina aliunda kundi lake na watu wake kwenye kila kitu....
Stay tuned more to come.......
...waiting
 
Hawa ni marafiki wa chama chetu pendwa wameletwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo na vya kati.
 
Jamani,so sad aiseeee, ina maana Serikali yetu hawajui kabisaaa haya mambo
Hawa wachina kumbe ni wapuuzi kiasi hiki
Hawa askari wa siku hizi wa vyeti feki utakuta wanapewa taarifa na raia wema.....wanakwenda eneo la tukio wanatukizwa kwa kupewa dola kadhaa tena mara kwa mara na wao wanapiga kimya ili uovu uendelee na wao wapate mgao.......shenzi sana askari wasio waadilifu.........mbwa wa kunyonga kabisa
 
Back
Top Bottom