Mnadhani mnawazidi Wachina akili? Subiri muone.

Mnadhani mnawazidi Wachina akili? Subiri muone.

Prakatatumba abaabaabaa

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2022
Posts
2,231
Reaction score
7,513
Nimeona tunawachekea Wachina mno wanaingia TZ vibaya mno tena wapo wengi, Iko sio jambo la kushangaza mno, jambo la kushangaza je mamlaka zetu zinafahamu hata Chinese people ni wangapi hapa TZ? je wanafahamu kwamba wapo wachina wanafuga Bata na kuku? Je wanafahamu wapo wana maduka mtaani maduka ya kawaida? Je wameshapima athari za hawa jamaa nchini?
Nimeona sasaivi wanachimba dhahabu uko chunya, geita, brothers hiyo nchi yenu ni noma sana watu wanachukua chao mapema.

Nimeona jana Kwa bashasha viongozi wamefungua jengo la biashara la yiwu, yiwu ni mji mkubwa wa biashara Unajulikana duniani kama moja ya masoko makubwa zaidi ya jumla (wholesale markets) je mmeshapiga hesabu ya hasara zake? Watauza bidhaa zao Kwa bei ya hapa tena Kwa rejareja vipi kuhusu wafanyabiashara wa kariakoo? Kumbuka hawa wachina wana mtaji mikubwa, believe me wakipata pesa hawa jamaa sidhani kama inarudi kwenye mzunguko hapa, mission Yao ni kutafuta pesa tu matumizi ni huko kwao, basi pesa itapatikanaje kama wamiliki/watumiaji wamenyang'anywa?

Wameanza kushtuka kupata visa ya kwenda China ni mtifuano mkali na zakuvizia ila wao kuja uku visa ni kama oxygen, kumbuka sisi wabongo kwanza tuna roho mbaya hatupendani ukisema ulete huo mzigo ukiritimba ni wakutosha, ila sidhani kama inatokea kwao,

Kizazi iki na kinachokuja wajikite wapi kwenye uzalishaji au mashambani?

Anyways nobody care, taifa ni kubwa fursa ni tele pambaneni.
 
Tanzania ni nchi ya kujua kuna wachina wangapi??Wakati kila sehemu kunanuka rushwa, kwanza mie naona acha tu wachina wajae nchini kwetu ili tutie akili maana tumelala sana. Wabongo kuanzia wa viongozi wa juu kabisa hadi maskini kapuku anaona ni bora wachina waingie freely wafanye wafanyalo lakini si kwa wabongo walioenda kutafuta maisha nje ya nchi, ndio maana hawataki kusikia uraia pacha. Kwa mbongo yoyote maskini au tajiri wanaona ni bora mgeni kutoka nje atajirike kuliko ndugu yake mbongo aliechukua uraia wa nchi nyingine. Tuna roho mbaya sana kwa ndugu zetu kuliko kwa watu weupe, na hatuna tofauti na wa south afrika. Acha inyeshe tujue panapo vuja.
 
Tatizo wabongo hatuhurumiani. Bidhaa ya mbongo inauzwa shilingi 5500 bidhaa hiyohiyo mchina anaiuza 1800. Unafanya kazi kwa mkandarasi mzawa unalipwa elfu 10 na malipo siyo ya wakati wakati kazi hiyohiyo kwa mchina ni 20000 kwa malipo ya wakati
 
Hatujitambui, unaweza kupambania watz wenzako lakini wao wanataka kukuumiza. Acha wachina waingie Kwa wingi zaidi ya sasa ili akili zikae sawa, maumivu Kila mmoja yamguse Nafikiri ndio itakaa poa, Kwanza bongo Hapa Serikali wezi Hadi watz wenzako wafanyabishara pia ni wezi, ww ukinyooka unaletewa nzi wengi mlangoni....
 
Nimeona tunawachekea wachina mno wanaingia TZ vibaya mno tena wapo wengi, Iko sio jambo la kushangaza mno, jambo la kushangaza je mamlaka zetu zinafahamu hata Chinese people ni wangapi hapa TZ? je wanafahamu kwamba wapo wachina wanafuga Bata na kuku? Je wanafahamu wapo wana maduka mtaani maduka ya kawaida? Je wameshapima athari za hawa jamaa nchini?
Nimeona sasaivi wanachimba dhahabu uko chunya, geita, brothers hiyo nchi yenu ni noma sana watu wanachukua chao mapema.

Nimeona jana Kwa bashasha viongozi wamefungua jengo la biashara la yiwu, yiwu ni mji mkubwa wa biashara Unajulikana duniani kama moja ya masoko makubwa zaidi ya jumla (wholesale markets) je mmeshapiga hesabu ya hasara zake? Watauza bidhaa zao Kwa bei ya hapa tena Kwa rejareja vipi kuhusu wafanyabiashara wa kariakoo? Kumbuka hawa wachina wana mtaji mikubwa, believe me wakipata pesa hawa jamaa sidhani kama inarudi kwenye mzunguko hapa, mission Yao ni kutafuta pesa tu matumizi ni huko kwao, basi pesa itapatikanaje kama wamiliki/watumiaji wamenyang'anywa?

Wameanza kushtuka kupata visa ya kwenda china ni mtifuano mkali na zakuvizia ila wao kuja uku visa ni kama oxygen, kumbuka sisi wabongo kwanza tuna roho mbaya hatupendani ukisema ulete huo mzigo ukiritimba ni wakutosha, ila sidhani kama inatokea kwao,

Kizazi iki na kinachokuja wajikite wapi kwenye uzalishaji au mashambani?

Anyways nobody care, taifa ni kubwa fursa ni tele pambaneni.
Mawinga mmeanza kulala mika🤣
 
Back
Top Bottom