Mtaji wa Tsh. Milioni 1 hadi 5: Naweza kufanya Biashara gani Tanzania?

Uko mkoa gani Mkuu, nataka kukushauri kuwa anzisha mobile Stationery, ukinunua Epson mashine l850 kwa Bei ya shilingi 900,000,ukanunua na laptop ya shilingi 400,000,dheni ukanunua na generator ya kwaida ya
sh 300,000 ukawa una tembelea maeneo ya vijijini kupiga picha na kutoa papo kwa hapo hakika sh 20,000 kwa siku haikupi shida Mkuu,katika hiyo pesa yako unanunua na pikipiki used kwa sh 1,000,000 hakika hutojuta,kwenye pesa yako unabakiwa na sh 200,000,hii unanunua mafuta Lita 10,sawa na sh 35,000,karatasi za picha box 2,'4x6= 8000,A4 boksi 1= 8000 na limu moja sawa na sh 15000,hapa kwenye laki mbili unabakiwa na takribani sh 13500,Kama uko kijijini lazima ulale na sh 20,000

Kikubwa usinunue Epson mashine ambayo ni used pamoja na generator,buy new ones


Pia uwe na muda wa kutembelea masherehe ukiwa na hiyo mashini yako hakika hutojuta, Epson printer l850 inafanya kazi zote za steshenari hivyo utapiga pesa sana Mkuu.


Mimi ninayo inalisha familia ya mke na watoto wanne na wanavaa na kupendeza, so naongea kwa uzoefu Mimi huyu.
Ipo vizur hii

Sent from my TECNO KD6 using JamiiForums mobile app
 
Habari za wakati huu ndugu msomaji.

Ni siku nyingine nzuri tuliyo barikiwa kuiona na kuiishi. Hakika ni jambo la kushukuru sana kuiona siku nyingine.

Leo kwenye chapisho langu naenda kujibu swali ambalo watu wengi huuliza au kuomba ushauri sana kwa watu. Swali hilo ni hili “Nina mtaji kiasi…. Kwa mtaji huo biashara gani inayolipa nifanye”?. Ungana nami mpaka mwisho kwenye chapisho hili nitakalo jibu swali hilo kulingana na uzoefu wangu na uelewa wangu.
Kwanza kabisa ukiona mtu anasema “nina mtaji kiasi…. biashara gani inayolipa naweza kufanya kwa mtaji huo”? Ukiona unaulizwa swali hilo tambua kuwa unachoombwa hapo ni wazo la biashara. Muulizaji anakuomba umpe wazo la biashara anayo weza kufanya na itakayomlipa kulingana na kiwango cha mtaji alionao. Hii ndiyo maana yake.

Biashara gani ya kufanya..?

Mara nyingi wengi ya wanao uliza swali hili ni watu ambao aidha wamepata hela ya ghafla na inawezekana wanakuwa wamepata hela ambayo hawakutarajia kupata hivyo hela imekuja tu. Pili ni watu ambao walitarajia kupata hela hiyo ila wakati wanatarajia kupata hela hiyo walikuwa hawaiwekei malengo hela hiyo.

Hivyo walitarajia kupata hela hiyo na wamepata ila hawajui wafanyie nini hela hiyo. Na tatu ni watu ambao tayari wana hela. Kuna watu ambao tayari wana hela. Kuna biashara au kazi wanazofanya ambazo zinawaingizia hela. Sasa anakuwa hana wazo la kufanya biashara au kazi nyingine. Kuna kipindi kinafika kwa binadamu ambapo anakuwa na pesa kiasi kwamba anakosa mawazo mapya ya kuendeleza biashara zake.

Kwenye makundi haya matatu, watu wote wana shida inayofanana ingawa wana tofautiana kwenye uzoefu. Kundi la tatu lenyewe lina uzoefu zaidi. Na sema shida yao ni moja kwa sababu wote hawa wanatafuta wazo jipya la biashara ya kufanya.

Siyo vibaya kuomba ushauri wa wazo gani la biashara unayoweza kufanya na ika kulipa. Lakini inategemea unapo amua kuomba ushauri wewe ulikuwa na wazo gani kabla la kufanya biashara. Kwanini nasema hivi?
Nasema hivi kwa sababu wazo la biashara utakayofanya na ikakulipa litazalishwa na kutoka kwenye akili yako mwenyewe. Wazo la biashara utalizalisha na utalitoa kwenye akili yako kwa aidha kwa kuona, kwa kusikia, kwa uzoefu wako na kwa akili yako kubuni wazo jipya la biashara ambayo haikuwahi kuwepo.
Kwa maneno mengine wazo zuri la biashara itakayo kulipa na utakayofanya kulingana na mtaji ulio nao litatoka ndani yako wewe mwenyewe.

Hili ndiyo wazo bora la biashara utakayoweza kuifanya na ikakulipa vizuri. Kwa hiyo kama kesho una mtaji umepata ghafla ambao hukutegemea kupata, au ulitegemea kupata mtaji huo lakini hukuwekea lengo/wazo la biashara utakayofanya pindi hela hiyo ikitoka, au wewe tayari una uzoefu wa kufanya biashara/kazi fulani inayolipa na pesa kwako siyo shida ila shida ni akili yako haitoi mawazo mapya ya biashara, basi tambua kabla hujaomba ushauri kwa watu juu ya biashara gani ufanye kwa mtaji wa…. Tambua kuwa mtaji wa biashara ya ukweli na itakayo kulipa itazalishwa na kutokea kwenye akili yako mwenyewe. Jambi muhimu ni wewe kujua namna ya kuamsha akili yako iendelee kuja na mawazo mapya kila unapohitaji.

Kuwa na wazo la biashara ulilozalisha mwenyewe kwenye akili yako ni muhimu kwani utakuwa tayari kutafuta maarifa na kujifunza juu ya wazo hilo jipya la biashara.

Sijasema usiombe ushauri kwa watu. Omba ushauri kwa watu wa kueleze namna ya kutekeleza wazo la biashara yako ambalo akili yako tayari ishalizalisha. Hii itakuwa rahisi kwako kupambana na changamoto za biashara na pia itakuepusha na hali ya kukosa hamasa pindi mambo yakiwa hayaendi kama unavyo taka yaende kwenye biashara yako.

Kabla hujaomba wazo la biashara kwa watu wengine tambua kuwa una mgodi mkubwa kwenye kichwa chako ambao kama utautumia utakuletea wazo au mawazo bora ya biashara utakayoweza kufanya. Namna pekee ni wewe kujua namna ya kujua kutumia mgodi huo ili uwe utakuletea mawazo bora ya biashara.

Moja ya faida ya kuja na wazo la biashara wewe mwenyewe ni kukuepusha na majuto na lawama pindi ikitokea wazo la biashara yako haliendi kama ulivyo shauriwa na watu. Kwani siyo watu wote unao waomba ushauri wa juu ya wazo la biashara unayotaka kufanya watakupa ushauri sahihi. Wengine watakupa ushauri kwa lengo la kujinufaisha wao na wengine watakupa ushauri wa biashara ya kufanya hata kama hawana maarifa yoyote ya biashara na kuweza kutoa ushauri.

Ni hayo tu kwa leo ndugu msomaji.
 
Habari za wakati huu ndugu msomaji wa blog hii www.jamii.app/JFUserGuide? Ni siku nyingine nzuri tuliyo barikiwa kuiona na kuiishi. Hakika ni jambo la kushukuru sana kuiona siku nyingine.
Leo kwenye chapisho langu naenda kujibu swali ambalo watu wengi huuliza au kuomba ushauri sana kwa watu. Swali hilo ni hili “Nina mtaji kiasi…. Kwa mtaji huo biashara gani inayolipa nifanye”?. Ungana nami mpaka mwisho kwenye chapisho hili nitakalo jibu swali hilo kulingana na uzoefu wangu na uelewa wangu.
Kwanza kabisa ukiona mtu anasema “nina mtaji kiasi…. biashara gani inayolipa naweza kufanya kwa mtaji huo”? Ukiona unaulizwa swali hilo tambua kuwa unachoombwa hapo ni wazo la biashara. Muulizaji anakuomba umpe wazo la biashara anayo weza kufanya na itakayomlipa kulingana na kiwango cha mtaji alionao. Hii ndiyo maana yake.



Biashara gani ya kufanya..?

Mara nyingi wengi ya wanao uliza swali hili ni watu ambao aidha wamepata hela ya ghafla na inawezekana wanakuwa wamepata hela ambayo hawakutarajia kupata hivyo hela imekuja tu. Pili ni watu ambao walitarajia kupata hela hiyo ila wakati wanatarajia kupata hela hiyo walikuwa hawaiwekei malengo hela hiyo. Hivyo walitarajia kupata hela hiyo na wamepata ila hawajui wafanyie nini hela hiyo. Na tatu ni watu ambao tayari wana hela. Kuna watu ambao tayari wana hela. Kuna biashara au kazi wanazofanya ambazo zinawaingizia hela. Sasa anakuwa hana wazo la kufanya biashara au kazi nyingine. Kuna kipindi kinafika kwa binadamu ambapo anakuwa na pesa kiasi kwamba anakosa mawazo mapya ya kuendeleza biashara zake.
Kwenye makundi haya matatu, watu wote wana shida inayofanana ingawa wana tofautiana kwenye uzoefu. Kundi la tatu lenyewe lina uzoefu zaidi. Na sema shida yao ni moja kwa sababu wote hawa wanatafuta wazo jipya la biashara ya kufanya.
Siyo vibaya kuomba ushauri wa wazo gani la biashara unayoweza kufanya na ika kulipa. Lakini inategemea unapo amua kuomba ushauri wewe ulikuwa na wazo gani kabla la kufanya biashara. Kwanini nasema hivi?
Nasema hivi kwa sababu wazo la biashara utakayofanya na ikakulipa litazalishwa na kutoka kwenye akili yako mwenyewe. Wazo la biashara utalizalisha na utalitoa kwenye akili yako kwa aidha kwa kuona, kwa kusikia, kwa uzoefu wako na kwa akili yako kubuni wazo jipya la biashara ambayo haikuwahi kuwepo.
Kwa maneno mengine wazo zuri la biashara itakayo kulipa na utakayofanya kulingana na mtaji ulio nao litatoka ndani yako wewe mwenyewe. Hili ndiyo wazo bora la biashara utakayoweza kuifanya na ikakulipa vizuri. Kwa hiyo kama kesho una mtaji umepata ghafla ambao hukutegemea kupata, au ulitegemea kupata mtaji huo lakini hukuwekea lengo/wazo la biashara utakayofanya pindi hela hiyo ikitoka, au wewe tayari una uzoefu wa kufanya biashara/kazi fulani inayolipa na pesa kwako siyo shida ila shida ni akili yako haitoi mawazo mapya ya biashara, basi tambua kabla hujaomba ushauri kwa watu juu ya biashara gani ufanye kwa mtaji wa…. Tambua kuwa mtaji wa biashara ya ukweli na itakayo kulipa itazalishwa na kutokea kwenye akili yako mwenyewe. Jambi muhimu ni wewe kujua namna ya kuamsha akili yako iendelee kuja na mawazo mapya kila unapohitaji.
Kuwa na wazo la biashara ulilozalisha mwenyewe kwenye akili yako ni muhimu kwani utakuwa tayari kutafuta maarifa na kujifunza juu ya wazo hilo jipya la biashara.
Sijasema usiombe ushauri kwa watu. Omba ushauri kwa watu wa kueleze namna ya kutekeleza wazo la biashara yako ambalo akili yako tayari ishalizalisha. Hii itakuwa rahisi kwako kupambana na changamoto za biashara na pia itakuepusha na hali ya kukosa hamasa pindi mambo yakiwa hayaendi kama unavyo taka yaende kwenye biashara yako.
Kabla hujaomba wazo la biashara kwa watu wengine tambua kuwa una mgodi mkubwa kwenye kichwa chako ambao kama utautumia utakuletea wazo au mawazo bora ya biashara utakayoweza kufanya. Namna pekee ni wewe kujua namna ya kujua kutumia mgodi huo ili uwe utakuletea mawazo bora ya biashara.
Moja ya faida ya kuja na wazo la biashara wewe mwenyewe ni kukuepusha na majuto na lawama pindi ikitokea wazo la biashara yako haliendi kama ulivyo shauriwa na watu. Kwani siyo watu wote unao waomba ushauri wa juu ya wazo la biashara unayotaka kufanya watakupa ushauri sahihi. Wengine watakupa ushauri kwa lengo la kujinufaisha wao na wengine watakupa ushauri wa biashara ya kufanya hata kama hawana maarifa yoyote ya biashara na kuweza kutoa ushauri.
Ni hayo tu kwa leo ndugu msomaji wa blog hii ya . Endelea kutembelea blog hii kujifunza zaidi machapisho bora kila siku.
Unaweza kuwasiliana nami kwa kutuma ujumbe Whatsapp kwenye namba hii: 0769770288 au unaweza kutuma ujumbe kwenye email ambayo ni:
Rubbish, gazeti reefu pumba tupu.
 
Heading inasema wazo la biashara kwa wenye 1m. Harafu uzi mrefu brah brah tupu unapoona wanaomba msaada it mean wameshindwa sasa unawarudisha uko

Binafsi nimekerwa na uzi wako.
 
Sijawahi kufanya hata biashara ya kuuza pipi wapendwa, naomba mnishauri kwa hili.

Nina mtaji wa Sh. Milioni moja, naomba mnishauri nifanye biashara gani?

Mwanzo nilipanga kununulia simu kali, subwoofer, friji, na vitu vingine vya ndani, ila nimeona sio issue bora nifanyie biashara lakini ndio hivyo sijajua nifanyie biashara gani.

Wakubwa nina mtaji wa shilingi milioni mbili na nataka nifanye biashara.

Je, biashara gani ninaweza kufanya kulingana na pesa hiyo?

Nimetafakari sana ila nakosa kujua kwa usahihi biashara gani inanifaa.
Fungua Zahanati!! hapo utatibu wagonjwa walioumwa na nyoka tuuu kwa sana! ni vizuri wenye kwenye magonga nyoka meeengi!
 
Chagua moja wapo
IDEAS ZA KUTOKA KIMAISHA KWA MTAJI MDOGO


1.Nunua pikipiki ya Dhamana ukaanza biashara ya Boda boda.
2.Fungua saluni
3.Mradi wa tofali za kuchoma
3.Fuga kuku
4.Somea ujuzi wowote
5.Mradi wa kushona nguo
6.kijiwe cha kuchomelea
7.kijiwe cha milango na madirisha ya aluminum
8.Mgahawa Mdogo
9.Kijjwe cha kahawa
10.Mashine ya kupukuchua mazao mfano mahindi, mpunga, mtama, karanga, nk
11.Mashine ya kukata nyasi, kupalilia
12.Kuuza mbuzi, kuku,
13.Biashara ya mazao.
14.kukodi bus, daladala na kuzisimamia upate cha juu
15.Kutengeneza sabuni, sanitizer, handwash,
16.Kutengeneza unga wa lishe
17.Kilimo cha umwagailiaji water pump, mbegu, madawa
18.Jiko la supu
19.kutengeneza mkaa mbadala
20.Kuuza chips
21.Kukaanga kuku
22.Kutengeneza vitafunio
23.Kuzalisha ethanol
24.kufuga poko mbuzi katoliki
25.Kufungua kilabu cha pombe za kienyeji
26.Kufungua vijiwe vya Kukusanya ubuyu maporini yakitimia magunia unaleta mjini
27.Kuuza juice
28.Kuuza juice ya miwa
29.Kijiwe cha kukaanga samaki jioni
30.Shughuli za upambaji kumbi
31.Kusambaza bidhaa majumbani
32.Kusambaza bidhaa basic needs kwenye maduka ya vijijini yaani unanua mjini unasambaza kwa oda viduka vya vijijini.
33.Kuzunguka minadani kuuza nguo za mitumba, vyombo, nk
34.Kufungua tuition center
35.Kufungua grocery
36.Kuwa wakala wa bidhaa za viwandani
37.kijiwe cha kukusanya taka za plastic, chuma,oil chafu na tairi chakavu.
38.Kufungua genge la kuuza basic home need
39.Kufungua ofisi ya kupiga nguo pasi.
40.Ofisi ya kutengeneza viatu na mabegi
41.Kutengeneza vyombo vya kupikia mfano, majiko, ndoo, sufuria, mifuniko, vikaangio, nk
42.Saluni ya kutengeneza kucha za wanawake
43......Jengea vyumba vitatu wazazi wako nyumba ya Bati upate baraka
44..Nunua shamba
45.Nunua ng'ombe wadogo watano kwa laki na nusu anza ufugaji.
Au nunua mbuzi anza kufuga
46.Fungua kijiwe cha kuonyesha mpira
47.duka la nguo za kupoint classic za mitumba piga pasi tundika kwenye enga
48..Ofisi za baiskeli za kukodi hapo unapata baiskeli nane
49..Duka la spea za pikipiki na baiskeli
50.Duka la dawa na vipodozi
51..ofisi ya kuchaji simu kwa sola vijijini
52..ofisi ya uwakala wa kutuma na kutoa pesa
53.. Bustani za kuzalisha miche ya miti na matunda
54... Ufugaji nyuki na kuuza asali
55.. Kuzalisha unga wa muhogo
56..Direct sale yaani door to door delivery hapa unakuwa na torori na speaker unapita KILA nyumba unauza bidhaa na kuchukua oda ya nini wanataka Ili kesho uwaletee.
57.Utengenezaji pellets chakula cha mifugo,samaki.
58..unga wa lishe
59..mikeka
60.bidhaa za mianzi.
61.utengenezaji wine,
62.usafi wa majumbani
63.kuuza uji wa ulezi,mchele
64.utengenezaji mbolea za mboji na za maji.
65.utengenezaji wa vigae vya cement na vya udongo.
66.kupanda miti kwa ajili ya nguzo na mirunda
67.utengenezaji wa ndala
68.utengenezaji viatu
69.Upondaji kokoto
70.ufundi simu na radio
71.Utengenezaji mifagio
72.utengenezaji crips za Mihogo,ndizi,viazi,nk
73.Utengenezaji tambi,ubuyu
74.panda mlonge,au nyonyo,au mibono au muarobaini Ili uje uuze mafuta,au utengeneze sabuni.
75.Kutengeneza siagi ya karanga
76.Home delivery hapa ni kupita KILA nyumba na kuchukua oda za mahitaji yao then unaenda kununua unawaletea
77.Utengezaji wa vifungashio vya karatasi
78.utengenezaji mitungi,vyungu,majiko ya udongo
79.
 
Back
Top Bottom