KINA LUMUMBA WETU: HUZUNI NA MAJONZI YA KUWAPOTEZA HANGA, SHARIFF, SADALLAH NA ABDULAZIZ K. TWALA.
"Karume hakuwapenda Wasomi, na hakuwa akiwaamini kabisa, hata ukiangalia wengi wa Viongozi wa ASP waliofungwa na Karume walikuwa ni wale Wasomi, Kama Othman Shariff.
Othman Shariff na Karume walikuwa ni Mahasimu ndani ya siasa za ndani za ASP hata kabla ya Uhuru wa Zanzibar, baada ya Mapinduzi Shariff aliteuliwa kuwa Waziri wa Elimu kisha mara tu baada ya Muungano na Tanganyika akateuliwa kuwa Balozi wa Tanzania Nchini Marekani.
Inasemwa kuwa wakati flani Shariff aliporudi nyumbani Tanzania kwa mapumziko aliwahi kuonekana akipiga picha katika maeneo ya Ikulu, hilo tu la kuonekana akipiga picha Ikulu lilitosha kulifanya 'Baraza la Mapinduzi' kumtuhumu Balozi Shariff kuwa ni 'shushushu' wa CIA aliyekuwa akipeleleza kwa ajili ya Manufaa ya Serikali ya Marekani.
Mamlaka za Usalama zilimkamata kwa tuhuma za 'Ushushushu na Ukibaraka' lakini zilimuachia mara baada ya Rais Nyerere kuingilia hilo. Alishushwa Madaraka yake kutoka Balozi mpaka kuwa Afisa wa Mifugo katika Mkoa wa Iringa, Tanzania Bara.
Baadaye Usalama wa Taifa wa Zanzibar kwa amri Maalum ya Baraza la Mapinduzi ulitumwa kwenda kumkamata Balozi Othman Shariff Mussa huko Iringa na kumrejesha Zanzibar, Mwalimu Nyerere alijaribu tena kuingilia kwenye hilo baada ya kuombwa kufanya hivyo na Wazee wa Iringa.
Baadaye Nyerere alikubali kumkabidhi Shariff kwa Mamlaka za Usalama wa Taifa wa Zanzibar baada ya kushawishiwa na Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi, mara baada ya kufikishwa Zanzibar huo ndio ulikuwa mwisho wa Shariff.
Abdallah Kassim Hanga alikuwa Msomi kutoka Urusi na mtu Mashuhuri sana Miongoni mwa Wanachama Vijana wa Chama cha Afro-Shiraz (ASP). Mara baada ya Mapinduzi alitangazwa kuwa Makamo wa Rais wa Serikali ya Mpinduzi ya Zanzibar chini ya Karume kabla ya kuhamishiwa Jijini Dar es salaam kwenye Serikali ya Muungano mara baada ya Muungano.
Punde tu Hanga alimtumbukia nyongo Nyerere kwa sababu ya Ukaribu wake na Kambona, aliyekuwa Waziri wa Nyerere wa Mambo ya Nje na Ulinzi. Wakati wa Uasi wa Jeshi la Tanganyika (King's African Riffles) mwaka 1964, alikuwa ni Kambona aliyekwenda kuzungumza na Wanajeshi wale akijaribu kuwatuliza wakati Nyerere akiwa Mafichoni.
Mara baada ya Kambona kukosana na Nyerere na kwenda Uhamishoni, Hanga naye alitazamwa kwa Jicho baya kwa kuwa alikuwa karibu mno na Kambona. Punde aliondolewa kwenye Baraza la Mawaziri na akaamua kuhamia Conakry, Nchini Guinea kwa kuwa alikuwa ameoa Mwanamke wa Kiguinea.
Baada ya muda, Rais Nyerere alipeleka Ujumbe kwa Rais Ahmed Sekou Toure wa Guinea, ambaye ndiye aliyekuwa amempa hifadhi Hanga Nchini mwake, akimuomba akubali kumrudisha Hanga Nchini Tanzania na akimuahidi kuwa Hanga asingedhuriwa na angebaki salama.
Kwa bahati mbaya, Mara baada ya Hanga kurejea Tanzania alikamatwa na akadhalilishwa hadharani wananchi wote wakishuhudia. Katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam Nyerere alimleta Hanga Uwanjani hapo akiwa na Pingu mikononi.
Katika Hotuba yake aliyoitoa viwanjani hapo, Rais Nyerere alimdhalilisha na kumsema vibaya Hanga na kama haitoshi akakubali kumrudisha Zanzibar ambako aliteswa na kisha kuuawa kinyume kabisa na ahadi aliyoitoa kwa Rais Sekou Toure".
Source: http://kidojembe.blogspot.com/2013/01/unamfahamu-mwafrika-aliedhulumiwa-kwa.html
President Julius Nyerere is pictured on January 16th when he addressed an open air rally where the detained former Tanzania Minister and Vice-President of Zanzibar was brought to face the people. Mr. Kassim Hanga (seated between two police officers) is under detention with a number of other top Tanzanians after allegedly boasting that he had been called from voluntary exile in Guinea to lead an army coup on Zanzibar.
IMAGE:© Bettmann/CORBISDATE PHOTOGRAPHED January 16, 1968
LOCATION Dar-Es-Salaam, Tanzanian
Nukuu:
Hanga ni huyo alie chini ya ulinzi wa polisi wawili.
source: Mzalendo.net
Na hapa JF:
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/63054-nyerere-alishiriki-mauaji-ya-kassim-hanga-9.html