Msiomkubali mwalimu Nyerere angalia hapa.

Msiomkubali mwalimu Nyerere angalia hapa.

ni msomi wa zamani na rais wa kwanza wa tanzania, hakuna anaepinga hilo, nawe usipinge kuwa yeye ndiye aliifanya hii nchi kuwa maskini wa mwisho duniani, alikuwa dikteta, na ndiye chanzo cha udini tanzania kwa kulitumikia kanisa katoliki zaidi ya wananchi wake ambao wengi wao si wakatoliki na ndio sababu mpaka alipostaafu mwitongo akihudumiwa na ma sista wa kanisani kama ma hausigeli wake na ndio katuzwa uwenye heri akingojea muujiza wa kumfanya mtakatifu.

tumeshachoshwa na kelele za mashekhe....hizi ni hoja za maasikini wa akili
 
Christopher Kasanga tumbo, Joseph Kaselabantu,Oscar Kambona,Tuntemeke sanga,Edwin Mtei,Christpher mtikila,Lifa chipaka hawa wote ni wazee wa ghahawa na Kashata? Ikiwa umekariri hivyo hata hoja za hawa wazee niliowataja huwezi kuelewa.Zipo hoja nyingi za msingi za wanaompinga that is why hata yeye mwenyewe kwenye hotuba zake alikiri kuwa hakuwa akiongoza serikali ya malaika.Taarifa za Kifedha Uswiz zinasema viongoz wa tz walianza kuficha fedha uswiz 1974 je nao ni wazee wa kashata? Hata kama kwa mtazamo wako Nyerere alikuwa bora kuliko wengine pia tambua haiondoi uwezekano wa kukosolewa!

Hivi umemsikia Edwin Mtei anavyomuongelea Mwalimu? au unakumbuka mwalimu mwenyewe alivyosifia sera nzuri chama cha Mtei CDM! Unakremu ee?
 
Opportunists wa leo wengi hawampendi. Wanazua kila aina ya uovu kama wao ni wema sana.
Time will tell hata yanayofichwa tutayaona hadharani
 
Stori hizi zimepitwa na wakati...Ni kelele masikioni...Njoo na tungo ingine mpya..

Rais wa kwanza wa Tanzania Mzee Nyerere katuwekea historia ambayo tuliokuwepo wakati wake hatuisahau daima:

Tulikosa hata dawa za meno wakati wake, tukaletewa dawa za kichina ukipigia mswaki, haupati testi ya chumvi wala sukari.

Umeshawahi uziona hizi?

Maxam%20120g.jpg
 
Ni msomi wa zamani na Rais wa kwanza wa Tanzania, hakuna anaepinga hilo, nawe usipinge kuwa yeye ndiye aliifanya hii nchi kuwa maskini wa mwisho duniani, alikuwa dikteta, na ndiye chanzo cha udini Tanzania kwa kulitumikia Kanisa Katoliki zaidi ya wananchi wake ambao wengi wao si wakatoliki na ndio sababu mpaka alipostaafu Mwitongo akihudumiwa na ma sista wa kanisani kama ma hausigeli wake na ndio katuzwa uwenye heri akingojea muujiza wa kumfanya mtakatifu.

Pole sana kwa mtazamo hafifu namna hii.
 
Shujaa kwako!mtu aliyetawala kwa miaka 25,akashindwa kvambua mahitaji MUHIMU ya raia wake,kwa kipindi chote hicho hakuweza KUJENGA JAPO CHUMBA KIMOJA TU CHA DARASA! HATA KM MOJA TU YA BARABARA YA TOPE ACHILIA MBALI LAMI.ALIYETAKA TULINGANE NA WANYAMA KWA KUTEMBEA UCHI.SINTA MSAHAU!

We kweli mtumishi wa pesa(S'h'e'ta..n.i)!! mie shule niliyosoma ilijengwa mwaka 1980 na serikali ya Mwalimu nakumbuka mwalimu mkuu alikuwa anahangaika kwenda wilayani kufuatilia pesa serikalini! Shule ilikuwa na madawati, madaftari ya bure!! jamani acheni kujidhalilisha wenye akili tunazidi kuwashusha hadi woote!!
Unajua wakati tunapata uhuru kulikuwa na mikoa haifikiki kabisa kwa barabara?? .......Na Mungu atawalaani kwa kusema uwongo...mtakuwa watu wa kulalamika maisha yenu yoote!
 
Rais wa kwanza wa Tanzania Mzee Nyerere katuwekea historia ambayo tuliokuwepo wakati wake hatuisahau daima:

Tulikosa hata dawa za meno wakati wake, tukaletewa dawa za kichina ukipigia mswaki, haupati testi ya chumvi wala sukari.


Umeshawahi uziona hizi?

Maxam%20120g.jpg
Kwa upeo wako finyu ufisadi wa JK na viongozi wake ni bora sana kuliko kupiga mswaki bila dawa??
 
Nyerere alikuwa mtu wa ideas.

Ku tout kukubalika kwake based on a plate at a Scottish university is really insulting the vast scope of his legacy.

Wengine tunapaenzi Edinburgh University kwa sababu Nyerere alisoma pale, hatumuenzi Nyerere kwa sababu alisoma Edinburgh University na "anakubalika" hapo.

Kama umemsoma Nyerere alijali kukubalika nyumbani kuliko nje. Sasa kwa nini tupewe ki plate cha nje kama kipimo cha kukubalika?

Ina maana hatujui kwamba Nyerere alikuwa rais na statesman mpaka Waskochi watuambie hivyo?
 
Opportunists wa leo wengi hawampendi. Wanazua kila aina ya uovu kama wao ni wema sana.
Time will tell hata yanayofichwa tutayaona hadharani

KINA LUMUMBA WETU: HUZUNI NA MAJONZI YA KUWAPOTEZA HANGA, SHARIFF, SADALLAH NA ABDULAZIZ K. TWALA.

"Karume hakuwapenda Wasomi, na hakuwa akiwaamini kabisa, hata ukiangalia wengi wa Viongozi wa ASP waliofungwa na Karume walikuwa ni wale Wasomi, Kama Othman Shariff.

Othman Shariff na Karume walikuwa ni Mahasimu ndani ya siasa za ndani za ASP hata kabla ya Uhuru wa Zanzibar, baada ya Mapinduzi Shariff aliteuliwa kuwa Waziri wa Elimu kisha mara tu baada ya Muungano na Tanganyika akateuliwa kuwa Balozi wa Tanzania Nchini Marekani.

Inasemwa kuwa wakati flani Shariff aliporudi nyumbani Tanzania kwa mapumziko aliwahi kuonekana akipiga picha katika maeneo ya Ikulu, hilo tu la kuonekana akipiga picha Ikulu lilitosha kulifanya 'Baraza la Mapinduzi' kumtuhumu Balozi Shariff kuwa ni 'shushushu' wa CIA aliyekuwa akipeleleza kwa ajili ya Manufaa ya Serikali ya Marekani.

Mamlaka za Usalama zilimkamata kwa tuhuma za 'Ushushushu na Ukibaraka' lakini zilimuachia mara baada ya Rais Nyerere kuingilia hilo. Alishushwa Madaraka yake kutoka Balozi mpaka kuwa Afisa wa Mifugo katika Mkoa wa Iringa, Tanzania Bara.

Baadaye Usalama wa Taifa wa Zanzibar kwa amri Maalum ya Baraza la Mapinduzi ulitumwa kwenda kumkamata Balozi Othman Shariff Mussa huko Iringa na kumrejesha Zanzibar, Mwalimu Nyerere alijaribu tena kuingilia kwenye hilo baada ya kuombwa kufanya hivyo na Wazee wa Iringa.

Baadaye Nyerere alikubali kumkabidhi Shariff kwa Mamlaka za Usalama wa Taifa wa Zanzibar baada ya kushawishiwa na Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi, mara baada ya kufikishwa Zanzibar huo ndio ulikuwa mwisho wa Shariff.

Abdallah Kassim Hanga alikuwa Msomi kutoka Urusi na mtu Mashuhuri sana Miongoni mwa Wanachama Vijana wa Chama cha Afro-Shiraz (ASP). Mara baada ya Mapinduzi alitangazwa kuwa Makamo wa Rais wa Serikali ya Mpinduzi ya Zanzibar chini ya Karume kabla ya kuhamishiwa Jijini Dar es salaam kwenye Serikali ya Muungano mara baada ya Muungano.

Punde tu Hanga alimtumbukia nyongo Nyerere kwa sababu ya Ukaribu wake na Kambona, aliyekuwa Waziri wa Nyerere wa Mambo ya Nje na Ulinzi. Wakati wa Uasi wa Jeshi la Tanganyika (King's African Riffles) mwaka 1964, alikuwa ni Kambona aliyekwenda kuzungumza na Wanajeshi wale akijaribu kuwatuliza wakati Nyerere akiwa Mafichoni.

Mara baada ya Kambona kukosana na Nyerere na kwenda Uhamishoni, Hanga naye alitazamwa kwa Jicho baya kwa kuwa alikuwa karibu mno na Kambona. Punde aliondolewa kwenye Baraza la Mawaziri na akaamua kuhamia Conakry, Nchini Guinea kwa kuwa alikuwa ameoa Mwanamke wa Kiguinea.

Baada ya muda, Rais Nyerere alipeleka Ujumbe kwa Rais Ahmed Sekou Toure wa Guinea, ambaye ndiye aliyekuwa amempa hifadhi Hanga Nchini mwake, akimuomba akubali kumrudisha Hanga Nchini Tanzania na akimuahidi kuwa Hanga asingedhuriwa na angebaki salama.

Kwa bahati mbaya, Mara baada ya Hanga kurejea Tanzania alikamatwa na akadhalilishwa hadharani wananchi wote wakishuhudia. Katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam Nyerere alimleta Hanga Uwanjani hapo akiwa na Pingu mikononi.

Katika Hotuba yake aliyoitoa viwanjani hapo, Rais Nyerere alimdhalilisha na kumsema vibaya Hanga na kama haitoshi akakubali kumrudisha Zanzibar ambako aliteswa na kisha kuuawa kinyume kabisa na ahadi aliyoitoa kwa Rais Sekou Toure".

Source:
http://kidojembe.blogspot.com/2013/01/unamfahamu-mwafrika-aliedhulumiwa-kwa.html

President Julius Nyerere is pictured on January 16th when he addressed an open air rally where the detained former Tanzania Minister and Vice-President of Zanzibar was brought to face the people. Mr. Kassim Hanga (seated between two police officers) is under detention with a number of other top Tanzanians after allegedly boasting that he had been called from voluntary exile in Guinea to lead an army coup on Zanzibar.

n33dxl.jpg

IMAGE:© Bettmann/CORBISDATE PHOTOGRAPHED January 16, 1968
LOCATION Dar-Es-Salaam, Tanzanian

Nukuu:
Hanga ni huyo alie chini ya ulinzi wa polisi wawili.


source: Mzalendo.net

Na hapa JF: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/63054-nyerere-alishiriki-mauaji-ya-kassim-hanga-9.html
 
Ni msomi wa zamani na Rais wa kwanza wa Tanzania, hakuna anaepinga hilo, nawe usipinge kuwa yeye ndiye aliifanya hii nchi kuwa maskini wa mwisho duniani, alikuwa dikteta, na ndiye chanzo cha udini Tanzania kwa kulitumikia Kanisa Katoliki zaidi ya wananchi wake ambao wengi wao si wakatoliki na ndio sababu mpaka alipostaafu Mwitongo akihudumiwa na ma sista wa kanisani kama ma hausigeli wake na ndio katuzwa uwenye heri akingojea muujiza wa kumfanya mtakatifu.

Nabii hakubaliki kwao, sishangai sana kwa Baadhi ya Watanzania kudharau kazi ya Nyerere, wala hawajaanza kwakwe hata YESU alipingwa tena na kuwambwa msalabani na watu aliokuwa akiwaponya magonjwa yao,na akiwafundisha. It will not stop with Zomba or Nyerere. Hata Wayahudi walisema YESU anakufuru, anajiita Mfalme n.k hivyo usishangae sana TZ but the World respects him for his stand on social justice and human right.
 
Watu wasiomkubali Mwalimu Nyerere, ni wale wenye wivu, ambao wengependa sifa za Nyerere zingefaa ziende kwao. Wangependa tuseme wao wameinua uchumi, wameleta umoja nk. Ukimtaja Nyerere ni kama unawafunika wao wasionekane. Wanahamu kuona wananchi wanageuza macho kutoka kumwangalia Mwalimu tuwaangalie wao, ikiwezekana sifa za Nyerere tuwamwagie wao. Wananchi watanzania waseme sasa ona viongozi wa sasa wanajenga barabara, shule za kata nk, lakini Nyerere alisomesha watu ambao sasa wanajenga barabara na shule za Kata. Kama utataka kukumbuka kuwa Mkapa, Kikwete na wataalam wengine wanaojidai kuleta maendeleo sasa wamesomeshwa na Nyerere.
Sio kwamba watu hawamkubali Mwl.Nyerere na familia yake hapana,kinachikataliwa ni namna ambavyo watu wanavyolitumia jina lake isivyo sawa kisiasa.

Kumkubali Mwl.Nyerere ni kufuata yale mazuri na kuyapuuza yale ambayo baadhi wanao hayakuwa kuwa katika utawala wake na hata baada ya kustaafu uraisi mwaka 1984-1985.

Kumzungumzia Mwl. Nyerere ni jambo jema kabisa la kujikumbusha uzalendo ulitukuka kwa mtanzania halisi na hivyo kuwa somo tosha la wanamapinduzi wa kweli wenye nia moja ya kulijenga taifa.

Ni wajibu sasa kwa pamoja kufuta nyayo za utajiri wa hekima na busara aliyotuachi Mwl.Nyerere,akiwezekana tuanze mara moja kubadilika kifikra kwa maana ya "uzalendo kwanza,mengine baadae".
 
Ni msomi wa zamani na Rais wa kwanza wa Tanzania, hakuna anaepinga hilo, nawe usipinge kuwa yeye ndiye aliifanya hii nchi kuwa maskini wa mwisho duniani, alikuwa dikteta, na ndiye chanzo cha udini Tanzania kwa kulitumikia Kanisa Katoliki zaidi ya wananchi wake ambao wengi wao si wakatoliki na ndio sababu mpaka alipostaafu Mwitongo akihudumiwa na ma sista wa kanisani kama ma hausigeli wake na ndio katuzwa uwenye heri akingojea muujiza wa kumfanya mtakatifu.

ahahahahaaaa harafu cha kuchekesha mkuu Zomba yupo in between 20 to 30 year sasa sielewi aliuonea wapi uongozi wa Mw Nyerere?????

One day utakubali na kukili kaka,acha roho mbayaaaaaaaa
 
ahahahahaaaa harafu cha kuchekesha mkuu Zomba yupo in between 20 to 30 year sasa sielewi aliuonea wapi uongozi wa Mw Nyerere?????

One day utakubali na kukili kaka,acha roho mbayaaaaaaaa

Pitia pitia humu JF utakutana na post inayoonesha nna umri gani, tena niliibandika leo hii mapema.
 
KINA LUMUMBA WETU: HUZUNI NA MAJONZI YA KUWAPOTEZA HANGA, SHARIFF, SADALLAH NA ABDULAZIZ K. TWALA.

"Karume hakuwapenda Wasomi, na hakuwa akiwaamini kabisa, hata ukiangalia wengi wa Viongozi wa ASP waliofungwa na Karume walikuwa ni wale Wasomi, Kama Othman Shariff.

Othman Shariff na Karume walikuwa ni Mahasimu ndani ya siasa za ndani za ASP hata kabla ya Uhuru wa Zanzibar, baada ya Mapinduzi Shariff aliteuliwa kuwa Waziri wa Elimu kisha mara tu baada ya Muungano na Tanganyika akateuliwa kuwa Balozi wa Tanzania Nchini Marekani.

Inasemwa kuwa wakati flani Shariff aliporudi nyumbani Tanzania kwa mapumziko aliwahi kuonekana akipiga picha katika maeneo ya Ikulu, hilo tu la kuonekana akipiga picha Ikulu lilitosha kulifanya 'Baraza la Mapinduzi' kumtuhumu Balozi Shariff kuwa ni 'shushushu' wa CIA aliyekuwa akipeleleza kwa ajili ya Manufaa ya Serikali ya Marekani.

Mamlaka za Usalama zilimkamata kwa tuhuma za 'Ushushushu na Ukibaraka' lakini zilimuachia mara baada ya Rais Nyerere kuingilia hilo. Alishushwa Madaraka yake kutoka Balozi mpaka kuwa Afisa wa Mifugo katika Mkoa wa Iringa, Tanzania Bara.

Baadaye Usalama wa Taifa wa Zanzibar kwa amri Maalum ya Baraza la Mapinduzi ulitumwa kwenda kumkamata Balozi Othman Shariff Mussa huko Iringa na kumrejesha Zanzibar, Mwalimu Nyerere alijaribu tena kuingilia kwenye hilo baada ya kuombwa kufanya hivyo na Wazee wa Iringa.

Baadaye Nyerere alikubali kumkabidhi Shariff kwa Mamlaka za Usalama wa Taifa wa Zanzibar baada ya kushawishiwa na Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi, mara baada ya kufikishwa Zanzibar huo ndio ulikuwa mwisho wa Shariff.

Abdallah Kassim Hanga alikuwa Msomi kutoka Urusi na mtu Mashuhuri sana Miongoni mwa Wanachama Vijana wa Chama cha Afro-Shiraz (ASP). Mara baada ya Mapinduzi alitangazwa kuwa Makamo wa Rais wa Serikali ya Mpinduzi ya Zanzibar chini ya Karume kabla ya kuhamishiwa Jijini Dar es salaam kwenye Serikali ya Muungano mara baada ya Muungano.

Punde tu Hanga alimtumbukia nyongo Nyerere kwa sababu ya Ukaribu wake na Kambona, aliyekuwa Waziri wa Nyerere wa Mambo ya Nje na Ulinzi. Wakati wa Uasi wa Jeshi la Tanganyika (King's African Riffles) mwaka 1964, alikuwa ni Kambona aliyekwenda kuzungumza na Wanajeshi wale akijaribu kuwatuliza wakati Nyerere akiwa Mafichoni.

Mara baada ya Kambona kukosana na Nyerere na kwenda Uhamishoni, Hanga naye alitazamwa kwa Jicho baya kwa kuwa alikuwa karibu mno na Kambona. Punde aliondolewa kwenye Baraza la Mawaziri na akaamua kuhamia Conakry, Nchini Guinea kwa kuwa alikuwa ameoa Mwanamke wa Kiguinea.

Baada ya muda, Rais Nyerere alipeleka Ujumbe kwa Rais Ahmed Sekou Toure wa Guinea, ambaye ndiye aliyekuwa amempa hifadhi Hanga Nchini mwake, akimuomba akubali kumrudisha Hanga Nchini Tanzania na akimuahidi kuwa Hanga asingedhuriwa na angebaki salama.

Kwa bahati mbaya, Mara baada ya Hanga kurejea Tanzania alikamatwa na akadhalilishwa hadharani wananchi wote wakishuhudia. Katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam Nyerere alimleta Hanga Uwanjani hapo akiwa na Pingu mikononi.

Katika Hotuba yake aliyoitoa viwanjani hapo, Rais Nyerere alimdhalilisha na kumsema vibaya Hanga na kama haitoshi akakubali kumrudisha Zanzibar ambako aliteswa na kisha kuuawa kinyume kabisa na ahadi aliyoitoa kwa Rais Sekou Toure".

Source:
http://kidojembe.blogspot.com/2013/01/unamfahamu-mwafrika-aliedhulumiwa-kwa.html

President Julius Nyerere is pictured on January 16th when he addressed an open air rally where the detained former Tanzania Minister and Vice-President of Zanzibar was brought to face the people. Mr. Kassim Hanga (seated between two police officers) is under detention with a number of other top Tanzanians after allegedly boasting that he had been called from voluntary exile in Guinea to lead an army coup on Zanzibar.

n33dxl.jpg

IMAGE:© Bettmann/CORBISDATE PHOTOGRAPHED January 16, 1968
LOCATION Dar-Es-Salaam, Tanzanian

Nukuu:
Hanga ni huyo alie chini ya ulinzi wa polisi wawili.


source: Mzalendo.net

Na hapa JF: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/63054-nyerere-alishiriki-mauaji-ya-kassim-hanga-9.html

Sasa ulitaka amwache ili aendeleze mikakati ya kupindua serikali yake?? Vp unafikri ni Hanga tu au ni Tanzania tu, karibu kila nchi hata huko Marekani mashushu wakubwa wa CIA wakati mwingine huishia jela.

Wakati nchi za Kiafrika zikipata Uhuru palikuwa na wasomi wachache sana na wengi walisoma katika nchi za Kibepari au za Kijamaa na walikuwa wakija na mawazo tofauti sana. Jiulize kwanini nchi nyingi za Kiafrika zilikuwa na mapinduzi sana, je ni mtu aliamka asubuhi tu na kwenda kupindua nchi? La palikuwa n mikakati ndani na nje ya nchi kufanya mapinduzi.
Kama Nyerere asingekua mkali na wasomi na wanamapinduzi wa kipindi kile angesha pinduliwa kama walivyofanya katika nchi za Uganda,Nigeria,Ghana n.k . Hata wewe ukiwa raisi alaf kuna watu wanatishia uraisi wako kwa njia isiyo rasmi lazima udeal nao,

Ukimaliza kushangaa ya akina Oscar Kambona na Hanga uanze kushangaa ya Babu Seya na familia yake ya wanamuziki
 
Sasa ulitaka amwache ili aendeleze mikakati ya kupindua serikali yake?? Vp unafikri ni Hanga tu au ni Tanzania tu, karibu kila nchi hata huko Marekani mashushu wakubwa wa CIA wakati mwingine huishia jela.

Wakati nchi za Kiafrika zikipata Uhuru palikuwa na wasomi wachache sana na wengi walisoma katika nchi za Kibepari au za Kijamaa na walikuwa wakija na mawazo tofauti sana. Jiulize kwanini nchi nyingi za Kiafrika zilikuwa na mapinduzi sana, je ni mtu aliamka asubuhi tu na kwenda kupindua nchi? La palikuwa n mikakati ndani na nje ya nchi kufanya mapinduzi.
Kama Nyerere asingekua mkali na wasomi na wanamapinduzi wa kipindi kile angesha pinduliwa kama walivyofanya katika nchi za Uganda,Nigeria,Ghana n.k . Hata wewe ukiwa raisi alaf kuna watu wanatishia uraisi wako kwa njia isiyo rasmi lazima udeal nao,

Ukimaliza kushangaa ya akina Oscar Kambona na Hanga uanze kushangaa ya Babu Seya na familia yake ya wanamuziki

Jela, mahakama, sheria nakubaliana nazo kwa kila mkosa, lakini hili la kuanikwa na kusutwa mtu ni sheria ya wapi? bila kufikishwa mahakamani? tulikuwa vitani? ilhali nchi yetu imekabidhiwa madaraka bila kumwaga damu zaidi ya mbuzi ya damu aliyofanyiwa makafara Nyerere na wazee wa bagamoyo.

Kwa hayo tutamkumbuka sana Rais wetu wa kwanza Mzee Nyerere.
 
Ni msomi wa zamani na Rais wa kwanza wa Tanzania, hakuna anaepinga hilo, nawe usipinge kuwa yeye ndiye aliifanya hii nchi kuwa maskini wa mwisho duniani, alikuwa dikteta, na ndiye chanzo cha udini Tanzania kwa kulitumikia Kanisa Katoliki zaidi ya wananchi wake ambao wengi wao si wakatoliki na ndio sababu mpaka alipostaafu Mwitongo akihudumiwa na ma sista wa kanisani kama ma hausigeli wake na ndio katuzwa uwenye heri akingojea muujiza wa kumfanya mtakatifu.
ni ngumu sana kumkubali mtu mwingine kama wewe mwenyewe hujikubali
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom