Msimamo Rasmi: Wakati Umefika kwa Freeman Mbowe (MB) Kujiuzulu; na Sekretariati Yake...

La Lowassa ni tukio moja ambalo lilipita lakini hii ya kuwafananisha watu na mbwa imekuwa ni kejeli inayojirudia kila siku.

Hata hili litapita, labda kama ww ndio Lowassa useme limepita. Unasema kuwafananisha watu na mbwa linajirudia, ni lini tena lilisemwa ili tuwe na uhakika na usemacho?
 
Endeleza ukabila!!

Tunajua uko mlengo gani kwa faida ya nani.

Wewe ni sawa na zilpendwa,hakuna wa kukuamini tena.

Uliheshimika kwa hoja zako na si kwa jina lako unalotaka kuendelea kulitumia kwa faida ya unaowatumikia.

Mapandikizi yenu yamefeli sasa mnatapata!!

Wewe na Dr.Mihogo wote wanafiki.
Shambulia hoja badala ya watu
Hoja ya ukabila umeiibua wewe
Bavicha mnaua chama kwa kuendekeza upambe,huna,hadhi,uwezo wala nguvu ya kumshambulia Mzee Mwanakijini,inahitajika tafakuri pana ili kupangua hoja zake,Hizo sio size yako
 
Fafanua tafadhali
Mifano ya nchi ulizotumia kufikia conclusion hazina mazingira ya kisiasa, kiuchumi, kiuelewa miongoni mwa wananchi, yanayofanana na Tanzania. Katika nchi hizo sidhani kama polisi hubeba masanduku yenye kura na kukimbilia uchochoroni, na leo tumlaumu Mbowe tumshinikiza kung'oka eti kwa sababu chama anachokiongoza kimeshindwa kuchukua dola katikati ya hujuma za wazi wazi, ambazo zingine zinapaswa kukataliwa na wananchi bila kujali ni wanachama au wapenzi wa vyama gani. Kumnyoshea kidole Mbowe kutaka ang'oke katika uongozi wa Chadema huku wanachama na wananchi wakishuhudia vituko vya akina Mwambe, huku wakishuhudia nguvu ya dola na CCM kutaka ang'oke ni kuwafanyia dhihaka watu hao....sumu haionjwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!
 
Nisahihi mbowe akubali kwamba hali ya chama chini ya misingi anayoisimamia ni mbaya hivyo apishe fikra nyingine hii pia itaonesha demokrasia ndani ya chama kwakuwa ndiyo wanayoihubiri kilasiku, pengine ajaye ataleta maendeleo kwani mbowe sasa hasaidii chama kuwa na demokrasia na maendeleo Bali ubabe na msambaratiko. Tuwe wepesi kupokea mabadiliko hats kwa kushawishi watu wampokee Lowassa na kumpa hadhi kubwa (kumkabidhi nafasi kuu) huku haaminiki ilikuwa ni sababu tosha yayeye kujiuzulu kiheshma pasi na kusubiri watu wamchoke.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Hili ni swali ambalo linahitaji jibu. Kwenye nchi na vyama vya kidemokrasia mojawapo ya kanuni muhimu ni ile inayotaka viongozi wa juu wa chama kuwajibika mara moja pale vyama vyao vinaposhindwa uchaguzi. Hili ni kweli hasa pale kiongozi anapowekeza mkakati mzito na kuwaaminisha wanachama na mashabiki wake kuwa mkakati au msimamo waliochukua utakipa chama ushindi mkubwa. Mkakati au msimamo huo unaposhindwa viongozi wale hawatakiwi kuendelea na madaraka na badala yake hutangaza kuachia ngazi ili kutoa nafasi kwa viongozi wengine kuja na msimamo na mkakati mwingine ambao ni tofauti na ule mwingine. Nitatoa mifano michache.

Uingereza: Jeremy Corbyn
Bw. Corbyn alikuwa ni kiongozi wa chama cha Labour cha Uingereza akiwa kinyume kimisimamo na mwelekeo na uongozi wa Boris Johnson wa chama cha Conservatives. Katika mjadala wa kuondoka ama kuondoka au kubakia ndani ya Jumuiya ya Ulaya Corbyn aliongoza harakati za kubakia kwa muda mrefu. Alibeza misimamo na mipango ya chama cha Conservatives na hata kutaka uchaguzi mwingine ufanyike kuona wananchi wanasemaje.

Kufuatia matokeo ya uchaguzi mwezi Disemba mwaka jana ambayo yaliona Bw. Johnson akishinda na kupata wabunge wengi zaidi Corbyn alijua kuwa msimamo na mkakati wake umekataliwa na wananchi. Japo yeye mwenyewe alichaguliwa katika jimbo lake lakini alikiri kuwa hatokuwa tayari kukiongoza chama hicho kuelekea kampeni nyingine ya uchaguzi.

India: Rahul Gandhi
Licha ya kuwa na jina kubwa katika siasa za India, kiongozi wa chama cha Congress Gandhi alitarajiwa kubeba chama hicho ambacho familia na ukoo wake ulikuwa kama umekihodhi katika ngazi za juu kwa karibu nusu karne. Hata hivyo, baada ya kushindwa chaguzi za April na Mei mwaka jana, Gandhi alijikuta hana namna nyingine isipokuwa kukubali kuwa yeye hakuwa tena mtu sahihi wa kukiongoza chama hicho.

Katika kauli yake ya kujiuzulu Gandhi alisema "kuwajibika ni muhimu sana katika kuhakikisha chama chetu kinakua huko mbeleni. Ni kwa sababu hiyo nimeamua kujiuzulu nafasi yangu kama Rais wa chama". Hii haina maana hakuwa na mchango, au kuwa alikuwa kiongozi mbaya. Alichofanya ni somo la kawaida la demokrasia; kiongozi akishndwa kuongoza chama chake kushinda uchaguzi anatakiwa kujiuzulu siyo kutafuta udhuru.

Korea Kusini: Hoong Joon Pyo (kiongozi wa upinzani)
Mwaka 2018 chama cha Liberty Korea Party chini ya uongozi wa Bw. Pyo kilijikuta kinabwagwa vibaya kwenye uchaguzi mkuu kiasi cha kumfanya kiongozi huyo kukubali kubeba lawama zote za kushindwa huko na kuamua kujiuzulu.

Taiwan: Mwenyekiti Wu Den yii wa KMT
Baada ya kubwagwa vibaya kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka Huu uongozi mzima wa chama cha KMT uliandika barua zake kujiuzulu ili kuwajibikwa kwa matokeo mabaya ya uchaguzi huo. Mwenyekiti Wu Den yii (cheo sawa na cha Mbowe) akiongozi Sekretariati yake waliandika barua ya kujiuzulu mbele ya Kamati Kuu. Wu alikuwa ameapa kuwa mkakati wake wa uchaguzi utakipatia chama hicho angalau nusu ya viti vyote vya wabunge. Hilo halikutokea! na Walishindwa kwenye Urais kwa tofauti ya asilimia 20 ya kura!

Afrika Kusini: Mmusi Maimane wa DA
Kiongozi huyo alikuwa ni moto moto na alijaribu sana kukivutia chama cha DA kwa weusi wa Afrika ya Kusini. Hata hivyo, juhudi zake hizo hazikuweza kukifanya chama hicho kufanya vizuri zaidi kulinganisha na ANC ambayo ilikuwa inakumbwa na kashfa nyingi. Licha ya kashfa hizo chama cha DA hakikuweza kuvutia weusi wengi. Maimane aliamua kujiuzulu baada ya mikakati na mbingu zake zote kushindwa.

Mifano yote hiyo michache na ipo mingine mingi inatuonesha mambo mengi. Kubwa ni kuwa kiongozi wa chama cha siasa anaposhindwa kutimiza ndoto aliyowahidi wananchi wake yampasa yeye ajiuzulu na kama katika maamuzi hayo aliungwa mkono na viongozi wengine wa juu nao pia yawapasa kujiuzulu.

Mbowe na CHADEMA
Katika siasa zetu za Tanzania inasikitisha kuwa mikakati mbalimbali iliyobuniwa na MBowe na kutekelezwa na harakati mbalimbali imeonesha kufeli zaidi. Watu wamebakia kujivunia mavazi na rangi za magari na wingi wa misemo yenye kuvutia. Wakati umefika kwa Mbowe kujipima kama hawa viongozi wengine na kuona kama kweli anastahili kuiongoza CHADEMA kuelekea uchaguzi mkuu wa 2020 baada ya kukiongoza chama hicho katika kufanya maamuzi mabovu, ya hatari na yenye kukidhoofisha zaidi.

Ni Tanzania tu ambapo kiongozi wa upinzani anakiongoza chama katika kushindwa katika kila uchaguzi na bado anatarajiwa kuendelea kukiongozi miaka mingine. Ni Tanzania tu kiongozi wa upinzani anahukumiwa siyo kwa kuwezesha kuingia madarakani bali kwa kuangalia ni kura ngapi zimeongezeka kwenye mahesabu!

Binafsi naamini kuondoka kwa Mashinji leo kuwe ndio msumari wa mwisho wa kuonesha ubaya, na upotofu wa maamuzi ya Mbowe kama Mwenyekiti. Suala hili ni suala la kidemokrasia na siyo suala la binafsi. Na ninaamini Sekretariati nzima ya CHADEMA isijiuzulu na kutoa nafasi kwa wanachama wengine kushika hatamu za uongozi wa chama kuelekea uchaguzi mkuu wa 2020. Kuendelea kujificha kwenye kumlaumu Magufuli na CCM ni kujaribu kutafuta visingizio visivyoisha. Tangu 2005 hadi leo hii bado upinzani chini ya MBowe haujapata dawa sawasawa ya kukabiliana na CCM.

Kuukataa ukweli huu ni sawasawa na mtu anayejifumba macho kujificha na mwanga wa tochi unaommulika. Ni kweli anaweza asiuone mwanga huo lakini haina maana kwenye mwanga huo yeye haonekani.

Kudai ati "CCM iweke usawa" ati "tunapambana na dola" na kuwa "Magufuli ameminya demokrasia" ni visingizio vilivyopitwa na wakati na ambayo havina msingi katika uelewa wa siasa za kawaida za upinzani mahali popote duniani. Wale wapinzani wanaotaka chama tawala kiwatengenezee mazuria, kuwapambia maua na kuwaimbia nyimbo za kuwatia moyo hawafai hata chembe kuendelea kuuongoza upinzani huo.

Ni wakati wa Ndg. Freeman Mbowe kuamua kujiuzulu mara moja na siyo kutafuta udhuru na visingizio vya kushindwa. Afuate mfuano wa viongozi wengine ambao waliweza kuuangalia ukweli wa kushindwa kwao na kuusalimu kwa kujiuzulu.

Labda, Labda, UPINZANI wa kweli unaweza kuibuka.

MM. Mwanakijiji
Mbona sijawahi kukusikia ukitoa msimamo Mrema, Cheyo, Doutwa, Lipumba au Magufuli wajiuzulu?
 
Mbona siku nyingi tu tuliwaambia Chadema ni chama chake yeye binafsi Mbowe kwa maslahi ya ukoo wa Mbowe, msipate shida kulielewa hilo.

Kama Watanzania wengine ambao hawakuelewa kwa nini Dr. Slaa alinyimwa haki yake kugombea pale aliponyang'anywa tonge mdomoni. Mna wakati mgumu kumwelewa Mbowe na kampuni yake binafsi.
 
Mbowe hapo alipo anacheeka...

Nothing so far has seemed to work for them...kama aliondoka bwana yule na bado hiki chama kikabaki strong, bwana huyu ana lipi hasa? Labda useme kaondoka na taarifa za mipango, mbinu au siri chafu... Madhara yapo japo si makubwa kama ambavyo akina fulani wanavyoaminisha watu huko twittani na instagramuni!
 
Nahisi hujanielewa..
Mkuu unapima joto?
Kwa kifupi Mbowe is not for sale,is the die hard leader.
Na kwakuwa hatanunuliwa na hao wasiothamini utu wa mtu,bado ana nguvu na hari ya kujenga chama chake.
Wala usiwe na wasiwasi kama atakiongoza maisha,utafika muda nae atangatuka.
Je hujiulizi kwanini Nyerere aliongoza TANU hadi CCM akiwa Mwenyekiti zaidi ya miaka 40 wewe unamkomalia Mbowe mtoto wa jana?
Chadema kina mfumo wake wa uongozi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbowe hapo alipo anacheeka...

Nothing so far has seemed to work for them...kama aliondoka bwana yule na bado hiki chama kikabaki strong, bwana huyu ana lipi hasa? Labda useme kaondoka na taarifa za mipango, mbinu au siri chafu... Madhara yapo japo si makubwa kama ambavyo akina fulani wanavyoaminisha watu huko twittani na instagramuni!
Tusidanganyane hapa. Hakuna chama cha siasa kinachofurahia kuondokea na wanachama wake tena viongozi wa juu. Hawa viongozi wanavyoondoka kila kukicha ni dhahiri wanapunguza pia imani kubwa kwa wanachama wa chini. Infact, Chadema inapuputika taratibu.

Chadema ikiendelea kulifumbia macho tatizo hili na kuona kila anaendoka hana athari yoyote atakuja kubaki mbowe na mtei ambao ndo wenye maslahi yao kwenye hicho chama.


Sent from my SM-A730F using JamiiForums mobile app
 
Wote waliotaka kugombea nae wamerudi nyumbani kwa waliowatuma maana ngoma imedunda. Hizo mbinu mpya unazozitaja ni za kuendeleza chama ama kukiuza kama wengine walivyouza ubunge/udiwani wao?
Tatizo cdm hawaandai viongozi, na inakuwaje ukubwa wote huu wa chama hakuna viongozi walio andaliwa kushika hatamu?
 
Back
Top Bottom