Ndugu WOS,
Pole sana kwa Msiba Mkubwa wa Baba,Mwenyezi Mungu akuongezee nguvu na Ujasiri katika kipindi hiki kigumu cha Maombolezo.sala na maombi yetu yapo pamoja nawe....Poleni sana wale wote mlioguswa kwa karibu na msiba Huu!!!
- Mkuu WoS, pole sana na msiba huu na kama kawaida hapa sisi wote ni ndugu, iwapo unahitajika msaada wowote ulio katika uwezo wetu usisite kusema mkuu, siku zote tupo hapa pia kwa ajili ya each other, kwa hiyo tupo pamoja mkuu na wakati wowote.
Mungu akubariki wewe na familia yako muweze kukipita hiki kipindi kigumu sana cha maisha ya bin-adam, na pia ambariki marehemu.
Pole sana kwa kumpoteza mzazi wako mpendwa ndugu yangu. Wakati huu wa maombolezo ndiyo muda mzuri wa kujikumbusha tena kuwa sote tuko njiani; baba katangulia na sisi tutafuata.
Mimi na familia yangu tunamwomba sana Mwenyezi Mungu aipumuzishe roho ya marehemu baba yako mahala pema peponi.
Natoa salam hizi za rambi rambi kutokana na taarifa hizi za BAK kuhusu msiba wa mzazi wa member anayejiita Women of substance. Ninamtakia marehemu mapumziko mema ya amani milele. Amin.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.