Kwa kizazi cha sasa hakuna mwenye wito na kazi yoyote bali mshahara.
Walikuwa na uzalendo ni akina msuguri maana hao walikuwa tayari kufanya kazi ya jeshi bila hata kulipwa chochote na wakaridhika. Miaka hiyo jeshi halikuwa na mishahara wala maripurupu ya kuvutia na ndio maana watoto wa masikini na watu wasio na connection ajira pekee ilikuwa ni jeshi.
Miaka hiyo watoto wa vigigo ama vijana wasomi usingeweza kuomba jeshi maana haikuwa kazi ya hadhi. Ilikuwa ni nadra sana kumkuta mwanajeshi anamiliki gari ama nyumba nzuri labda kuanzia cheo cha brigedia angalau.
Baada ya jeshi kuboreshwa miaka ya elfu mbili mwanzoni pamoja na ukosefu wa ajira ndipo vijana wakaanza kukimbilia jeshini wakivutiwa na mishahara bora na uhakika wa ajira.
Kwa hiyo tusidanganyane, mleta mada yuko sahihi sana mshahara mzuri ndio kigezo cha jeshi kupendwa.
Kuna wakati vijana wengi miaka ya kati ya elfu mbili vijana wengi waliacha jeshi na kujiunga TAKUKURU kwa sababu walikuwa na package nzuri kuliko jw.
We jiulize kwa nini polisi na magereza hawakimbiliwi zaidi ya mtu kwenda ilimradi kufuata ajira baada ya kukosa kwingine?
Kwa nini vijana wanapenda TRA,TPA,TCRC, TANROAD nk?
Jaribu siku hao unaoita wazalendo wakate mishahara ama wasilipwe uone tifu lake.
Sent using
Jamii Forums mobile app