Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,281
SUALA LA CHADEMA TUMEMUACHIA MSAJILI WA VYAMA
Masuala yote yanayohusu maudhui ya utangazaji kisheria yapo chini ya Waziri mwenye dhamana ya habari, Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 pia imefafanua hilo, Sheria inatungwa lakini Kanuni zinatungwa na Mamlaka inayotekeleza sheria hiyo.
Suala la mabadiliko ya Sheria ya Kanuni za Maudhui Mtandaoni wadau walishirikishwa, suala la Kanuni hizo kurekebishwa wakati huu wa uchaguzi halihusiani na kitu chochote kuhusu uchaguzi kwani mambo mengine ya nchi lazima yaendelee.
Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 imeruhusu mwanafunzi wa taaluma ya habari kuwa na kitambulisho cha mwanahabari ili asipate shida hata akiwa katika mafunzo yake kwa vitendo.
Vyombo vingi vya habari vya kimataifa havina mitambo hapa nchini hivyo kuna baadhi ya maudhui yanayotolewa na vyombo hivyo yanagusa usalama na maadili ya nchi, lazima nchi tuilinde hivyo kanuni imekuja kuweka uratibu katika eneo hilo.
Si kweli kuwa uhusiano wa kidiplomasia wa Tanzania na nchi nyingine umepungua kutokana na namna ambavyo nchi yetu ilipambana na ugonjwa wa Covid19, uhusiano ni mzuri.
Diplomasia inaongozwa na Kanuni inaitwa "reciprocity",Tanzania haikutajwa katika nchi zilizoruhusiwa kuingiza ndege zao Kenya hivyo kama hatujaruhusiwa basi kwa kipindi hiki nao wapumzike kuja. Kwahiyo sio ugomvi bali ni kanuni ya kidiplomasia.
Rais wetu bado ni Mwenyekiti wa SADC, bado Mabalozi wa nchi zingine wanakuja nchini kwetu na sisi tunaendelea kwenda kwenye nchi zao, bado sisi ni wanachama wa UN pia tuna miradi mingi ambayo tunafanya pamoja na benki kubwa ikiwemo ya AfDB na WB.
Wakati wa Uchaguzi hakuna Sheria yoyote inayosimamisha utekelezaji wake, sheria zipo na zinaendelea kutumika. Suala la CHADEMA kuongeza ubeti wao katika wimbo wa Taifa tumewaachia Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa wafate taratibu na sheria.
Masuala yote yanayohusu maudhui ya utangazaji kisheria yapo chini ya Waziri mwenye dhamana ya habari, Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 pia imefafanua hilo, Sheria inatungwa lakini Kanuni zinatungwa na Mamlaka inayotekeleza sheria hiyo.
Suala la mabadiliko ya Sheria ya Kanuni za Maudhui Mtandaoni wadau walishirikishwa, suala la Kanuni hizo kurekebishwa wakati huu wa uchaguzi halihusiani na kitu chochote kuhusu uchaguzi kwani mambo mengine ya nchi lazima yaendelee.
Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 imeruhusu mwanafunzi wa taaluma ya habari kuwa na kitambulisho cha mwanahabari ili asipate shida hata akiwa katika mafunzo yake kwa vitendo.
Vyombo vingi vya habari vya kimataifa havina mitambo hapa nchini hivyo kuna baadhi ya maudhui yanayotolewa na vyombo hivyo yanagusa usalama na maadili ya nchi, lazima nchi tuilinde hivyo kanuni imekuja kuweka uratibu katika eneo hilo.
Si kweli kuwa uhusiano wa kidiplomasia wa Tanzania na nchi nyingine umepungua kutokana na namna ambavyo nchi yetu ilipambana na ugonjwa wa Covid19, uhusiano ni mzuri.
Diplomasia inaongozwa na Kanuni inaitwa "reciprocity",Tanzania haikutajwa katika nchi zilizoruhusiwa kuingiza ndege zao Kenya hivyo kama hatujaruhusiwa basi kwa kipindi hiki nao wapumzike kuja. Kwahiyo sio ugomvi bali ni kanuni ya kidiplomasia.
Rais wetu bado ni Mwenyekiti wa SADC, bado Mabalozi wa nchi zingine wanakuja nchini kwetu na sisi tunaendelea kwenda kwenye nchi zao, bado sisi ni wanachama wa UN pia tuna miradi mingi ambayo tunafanya pamoja na benki kubwa ikiwemo ya AfDB na WB.
Wakati wa Uchaguzi hakuna Sheria yoyote inayosimamisha utekelezaji wake, sheria zipo na zinaendelea kutumika. Suala la CHADEMA kuongeza ubeti wao katika wimbo wa Taifa tumewaachia Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa wafate taratibu na sheria.