Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,848
- 12,080
Baada ya kushindwa kutoa burudani usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Next Door Arena msanii huyo kutoka Nigeria amekamatwa na Polisi.
=========
Baada ya kushindwa kutoa burudani usiku wa kuamkia leo Agosti 8, 2022 katika Ukumbi wa Next Door Arena, msanii Kizz Daniel kutoka Nigeria amekamatwa na Polisi.
Chanzo kutoka kwa waratibu wa shoo hiyo kimeeleza kuwa msanii huyo alichelewa ndege kutoka Nigeria na kuwasili Dar es Salaam usiku mwingi muda mfupi kabla ya shoo kuanza.
Mara baada ya kuwasilia Dar ikagundulika kuwa begi lake la nguo halionekani.
Usiku huohuo simu zikaanza kupiga sehemu tofauti ili msanii huyo apate nguo, baadaye zikapatikana baadhi ya nguo lakini alizikataa zote, hadi inafika saa tisa usiku hakukuwa na mwelekeo na mwisho hakutokea kwenye shoo.
=========
Baada ya kushindwa kutoa burudani usiku wa kuamkia leo Agosti 8, 2022 katika Ukumbi wa Next Door Arena, msanii Kizz Daniel kutoka Nigeria amekamatwa na Polisi.
Chanzo kutoka kwa waratibu wa shoo hiyo kimeeleza kuwa msanii huyo alichelewa ndege kutoka Nigeria na kuwasili Dar es Salaam usiku mwingi muda mfupi kabla ya shoo kuanza.
Mara baada ya kuwasilia Dar ikagundulika kuwa begi lake la nguo halionekani.
Usiku huohuo simu zikaanza kupiga sehemu tofauti ili msanii huyo apate nguo, baadaye zikapatikana baadhi ya nguo lakini alizikataa zote, hadi inafika saa tisa usiku hakukuwa na mwelekeo na mwisho hakutokea kwenye shoo.