Mimi ninauheshimu sana mchango wako katika medani ya elimu nchini lakini ninapatwa na wasiwasi na namba ya gia ya kisiasa unayotaka kuingia nayo Iramba Magharibi. Ninapatwa na wasiwasi kama utaweza kuogelea kwenye mawimbi mazito ya siasa za majitaka na propaganda kama ulivyoanza.
Kitila Mkumbo kumnunua mtu siyo lazima umpatie pesa mkononi. Hotel bure, chakula bure, usafiri bure, magwanda ya chadema bure na hata kadi nyingine ya uanachama nayo ni bure. Hivi vitu vyote vimemtongoza kisiasa na sasa yuko Dar anajirusha kwenye viwanja ambavyo hakutegemea kufika. Huku si ndiyo kumnunua kisiasa.
Ninakutakia safari njema ya kisiasa katika jimbo la Iramba Magharibi lakini kumbuka unaenda kupambana na gwiji la siasa za Tanzania ambaye jina lake ukilitaja ndani ya ofisi za CHADEMA, mtaa wa Ufipa, kuna viongozi ndani ya ofisi huwa wanapata kiwewe.