Msaidizi wa Mwigulu atimkia CHADEMA

Msaidizi wa Mwigulu atimkia CHADEMA

Ndani ya CHADEMA binadamu wote wana thamani. Ni huko kwa Magamba utu wa binadamu hupimwa kwa fedha na vyeo. Na siku Rais kutoka CHADEMA atakapoapishwa, watu wa kawaida ni lazima wahudhurie maana hao ndio atakaowahudumia.

Yani katibu mkuu wa chama anapokea dagaa khaa hiki ni chama AMA Gari la mkaa
 
mwigulu...sio mtu mzuri hana siasa za kistaarabu..anasiasa za chuki...aige mfano wa januari makama, zitto, mnyika...
 
Umakini wa chadema umebakia kwenye kupayuka majukwaani tu! Muda si mrefu wataanza kulia lia huyo shamba boy ni kibaraka wakati katibu wao kampa kadi kwa mbwembwe nyingi! Cdm msitumie masaburi kufikiri
 
sina shaka na kujiunga kwake na chama cha ukombozi cdm, naamini viongoz wetu wanamfahamu vizur kuliko mimi, pia viongozi wangu wapo makini sana ,nashauri tu uanachama ni haki yake nafasi ya uongozi ndani ya chama, tujiridhishe sana asije kuwa ndio kaagizwa na mchemba, kutengeneza mkanda wa video au chochote
 
Mkuu hapo kwenye chadema kuwa na viongozi makini acha unazi na unafiki! Katika siku za karibuni tumeshuhudia jinsi uongozi wa chadema ilivyo mbumbumbu na wakurupukaji wakubwa,challenge kidogo tu madudu kibao! Bora hata dovutwa
sina shaka na kujiunga kwake na chama cha ukombozi cdm, naamini viongoz wetu wanamfahamu vizur kuliko mimi, pia viongozi wangu wapo makini sana ,nashauri tu uanachama ni haki yake nafasi ya uongozi ndani ya chama, tujiridhishe sana asije kuwa ndio kaagizwa na mchemba, kutengeneza mkanda wa video au chochote
 
mbona kwenye lile bandiko la ruzuku ya ccm sikukuona mkuu! Ulikuwa wapi tafadhali nijuze

Huwa wanachunguli kwenye kadirisha na kusepa,hawezi kukujibu lolote halafu una habari kama ni mgonjwa?
 
Hiyo ndio shida yenu CCM.Leo umeamua kumwita mpiga kiwi,hayo but punguzeni majibu mepesi katika maswala mazito kama hay.Swala la chama kupoteza mwananchama sio suala dogo katika tasnia ya siasa.

Usishangae hata yeye akihamia NCCR manunuzi,akina ritz watamuita mzibua vyoo.
 
CDM haitapokea wanachama kutoka CCM - Mbowe
CDM itajitoa mchakato wa katiba ikifika April 30 kama madai yetu hayatatekelezwa - Mbowe

Chama Makini

hukumuelewa. Tunawapokea lakini hatutawapa nafasi za uongozi.
 
Bonge la responce...Hii ilitakiwa ifanyike kwenye jimbo la Serukamba, Nkamia, Kibajaji, Ndugai, Makinda et al ... Mchuzi wa Mbwa shurt inywewe ikiwa ya moto!....

Kweli mkuu, kama Sukumaland(Mwanza na Shinyanga) na Buha(Kigoma) huko ndiko kulikuwa na CCM kweli, iliangukia CHADEMA. Basi 2013 majimbo yote CCM itaenyeshwa vya kutosha. Mwigulu si tishio ni mpuuzi tu. Hakuna aliyekuwa na kiburi nchi hii kama Lawrence Masha(Former Minister for Home Affairs) siku ya kura alifunzwa adabu na Wananyamagana!. Mwigulu dawa yake ni Dr Kitila Mkumbo. Wanairamba muungeni mkono Dr Mkumbo, Mwigulu anawatia aibu sana.
 
Yani katibu mkuu wa chama anapokea dagaa khaa hiki ni chama AMA Gari la mkaa

Dagaa ukiwakusanya ndiyo wanaounda chama!!!! Hata wale wenu anaopokea Katibu wenu si dagaa au? Tunaomba dagaa wengi wa kwenu waende CDM!!! Dagaa hoyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!! Karibuni ila msije mkawa mmetumwa!!!
 
Mimi ninauheshimu sana mchango wako katika medani ya elimu nchini lakini ninapatwa na wasiwasi na namba ya gia ya kisiasa unayotaka kuingia nayo Iramba Magharibi. Ninapatwa na wasiwasi kama utaweza kuogelea kwenye mawimbi mazito ya siasa za majitaka na propaganda kama ulivyoanza.

Kitila Mkumbo kumnunua mtu siyo lazima umpatie pesa mkononi. Hotel bure, chakula bure, usafiri bure, magwanda ya chadema bure na hata kadi nyingine ya uanachama nayo ni bure. Hivi vitu vyote vimemtongoza kisiasa na sasa yuko Dar anajirusha kwenye viwanja ambavyo hakutegemea kufika. Huku si ndiyo kumnunua kisiasa.

Ninakutakia safari njema ya kisiasa katika jimbo la Iramba Magharibi lakini kumbuka unaenda kupambana na gwiji la siasa za Tanzania ambaye jina lake ukilitaja ndani ya ofisi za CHADEMA, mtaa wa Ufipa, kuna viongozi ndani ya ofisi huwa wanapata kiwewe.
Acha hizo. Iramba watapata ukombozi ndani ya miaka 2
 
Back
Top Bottom