Liverpool VPN
JF-Expert Member
- Aug 29, 2020
- 5,807
- 13,054
Ni rafiki yangu wa kazi, tumpe Jina la John (yupo Halmashauri jirani). Amenipigia simu, na amenieleza jambo fulani nimeshindwa kumshauri.
Sababu ya kushindwa kumshauri ni kwamba; mi ningemjibu fasta kuwa PIGA CHINI NDOA fata SHULE ila "the problem is" alishani tahadharisha nisiwe "bias" katika majibu japo SIFAGILII NDOA.
Wakati ananiomba ushauri alisema ""Mr. Liverpool najua hupendi na hutaki kuoa, ila nakushirikisha hili jambo naomba usiwe bias, japo najua huzitaki ndoa". Na mimi nimeona niwashirikishe humu najua mpo mliopitia situation kama yake na mkapata jawabu.
SCENARIO:-
Mwaka jana kupitia matangazo ya Wizara ya Utumishi mimi na John tuliomba Scholarship ya PhD. Na ashukuriwe Mungu sotee tumepata post.
Wiki kama mbili zilizo pita Wizara ya Utumishi walituma barua za ruhusa kwa waajiri wetu ili waturuhusu kwenda shule pindi admission documents zitakapo tumwa. Mimi nilishirikisha familia na John akaenda kumshirikisha mchumba ake.
Flash back:-
John na mchumba ake walikutana tokea 2018. Uchumba wao ukaendelea kwa mabonde na milima mpaka kufika mwaka huu John alipo amua kuufanya officialize.
January/2022 alimpeleka kumtambulisha mchumba ake kwao. February/2022 John alituma mshenga kwa mchumba. Kwasasa wanaishi wote na wana mtoto mmoja. Na wapo kwenye process za ndoa kanisani. Wanahitaji kupanga tarehe, na mambo mengine ya ndoa.
The Problem:-
John alivyomshirikisha mchumba ake anasema mchumba alipoteza furaha ghafla na alinuna. Alikaa siku mbili haongei na John. Baada ya kubembelezwa sanaa mchumba ndio akafunguka.
1. Hataki John apande ndege aende kusoma kwasababu miaka mi3 ya masomo ni mingi, na yeye hawezi kuishi pekee yake TZ halafu John yupo nje.
2. Amesema na karudia sana hili jambo kwamba ""John akisepa tu basi atamkuta mchumba kashaolewa, kwamaana ye mchumba hawezi kuishi mpweke halafu John yupo nje"".
3. Mchumba kasema hawezi kukaa wiki moja bila kugongana na John, hivyo akisepa "Nani atakuwa anamtoa hamu?"
4. Mchumba analalamika John anamuacha vipi mtoto wao mwenye umri wa miaka miwili na mama pekee yake. Kwahiyo mchumba anahisi kama John anataka kusepa nje amuachie mchumba malezi ya mtoto mwenyewe.
Kaeleza mengi ila kifupi MCHUMBA HATAKI JOHN AENDE SHULE HUKO NJE YA NCHI na KASEMA AKIENDA TU KAMKOSA.
Difficults:-
John yupo njia panda kwa maana NDOA anaitaka na SHULE anaitaka, ila hajui achague kipi aache kipi. John anamuhitaji mchumba Tena anamuhitaji sanaa awe mkewe. John anahitaji sanaa mtoto ake alelewe na mama aliyemzaa, kwamba kutafuta mwanamke mwengine ahitaji kabisaa. Ila mchumba kashamuonya kwamba akipanda ndege na yeye KAMKOSA.
Uzi tayari.
Ushauri wako Muhimu.
#YNWA
Sababu ya kushindwa kumshauri ni kwamba; mi ningemjibu fasta kuwa PIGA CHINI NDOA fata SHULE ila "the problem is" alishani tahadharisha nisiwe "bias" katika majibu japo SIFAGILII NDOA.
Wakati ananiomba ushauri alisema ""Mr. Liverpool najua hupendi na hutaki kuoa, ila nakushirikisha hili jambo naomba usiwe bias, japo najua huzitaki ndoa". Na mimi nimeona niwashirikishe humu najua mpo mliopitia situation kama yake na mkapata jawabu.
SCENARIO:-
Mwaka jana kupitia matangazo ya Wizara ya Utumishi mimi na John tuliomba Scholarship ya PhD. Na ashukuriwe Mungu sotee tumepata post.
Wiki kama mbili zilizo pita Wizara ya Utumishi walituma barua za ruhusa kwa waajiri wetu ili waturuhusu kwenda shule pindi admission documents zitakapo tumwa. Mimi nilishirikisha familia na John akaenda kumshirikisha mchumba ake.
Flash back:-
John na mchumba ake walikutana tokea 2018. Uchumba wao ukaendelea kwa mabonde na milima mpaka kufika mwaka huu John alipo amua kuufanya officialize.
January/2022 alimpeleka kumtambulisha mchumba ake kwao. February/2022 John alituma mshenga kwa mchumba. Kwasasa wanaishi wote na wana mtoto mmoja. Na wapo kwenye process za ndoa kanisani. Wanahitaji kupanga tarehe, na mambo mengine ya ndoa.
The Problem:-
John alivyomshirikisha mchumba ake anasema mchumba alipoteza furaha ghafla na alinuna. Alikaa siku mbili haongei na John. Baada ya kubembelezwa sanaa mchumba ndio akafunguka.
1. Hataki John apande ndege aende kusoma kwasababu miaka mi3 ya masomo ni mingi, na yeye hawezi kuishi pekee yake TZ halafu John yupo nje.
2. Amesema na karudia sana hili jambo kwamba ""John akisepa tu basi atamkuta mchumba kashaolewa, kwamaana ye mchumba hawezi kuishi mpweke halafu John yupo nje"".
3. Mchumba kasema hawezi kukaa wiki moja bila kugongana na John, hivyo akisepa "Nani atakuwa anamtoa hamu?"
4. Mchumba analalamika John anamuacha vipi mtoto wao mwenye umri wa miaka miwili na mama pekee yake. Kwahiyo mchumba anahisi kama John anataka kusepa nje amuachie mchumba malezi ya mtoto mwenyewe.
Kaeleza mengi ila kifupi MCHUMBA HATAKI JOHN AENDE SHULE HUKO NJE YA NCHI na KASEMA AKIENDA TU KAMKOSA.
Difficults:-
John yupo njia panda kwa maana NDOA anaitaka na SHULE anaitaka, ila hajui achague kipi aache kipi. John anamuhitaji mchumba Tena anamuhitaji sanaa awe mkewe. John anahitaji sanaa mtoto ake alelewe na mama aliyemzaa, kwamba kutafuta mwanamke mwengine ahitaji kabisaa. Ila mchumba kashamuonya kwamba akipanda ndege na yeye KAMKOSA.
Uzi tayari.
Ushauri wako Muhimu.
#YNWA