lusanasaimon
Senior Member
- Jan 19, 2023
- 111
- 264
Nina rafiki yangu yeye amekuja kuniomba ushauri, iko hivi;
Yeye (rafiki yangu) aliamua kuondoka kwenda mkoa x kujitafuta baada ya kumaliza kidato cha nne na kukaa mtaani kwao bila muelekeo wowote.
Anasema Mungu si Athumani alipofika huko alijichanganya na kufanya shugli mbali mbali akafanikiwa kufungua kigoli (biashara) x, na katika mihangaiko hiyo alikujaga kupendana na mwanamke mmoja ambae ni single mother wa mtoto mmoja na wame hustle wote kwa muda wa miaka mitatu.
Wwaliamua kuishi pamoja ili kupunguza bajeti ya kila mtu kupanga chumba chake, ingawa hajawahi kwenda kujitambulisha kwao na mwanamke pamoja na mwenzake kumsumbua kuhusu hilo.
Jamaa anadai huyo mwanamke yuko vizuri na anampenda kwa sababu wamekuwa wanasaidiana na kuvumiliana kwa vingi isipokuwa huyo mwanamke amekuwa na tabia ya kutumia pombe na jamaa hapendi na amekwisha muonya na kumshauri aache lakini mwanamke hasikii, na jamaa anashindwa kumpiga chini kwasababu mwanamke anampenda sana na wamesota sana mpaka jamaa kusimama kiuchumi si haba.
Sasa issue imekuja baada ya jamaa majuzi kutembelea nyumbani kwa wazazi wake anadai wamemsakama sana kuhusu kuoa wanadai amekuwa sasa, na amewaficha kama anaishi na mwanamke kwasababu anahisi hatoweza kutimiza ahadi za kumuoa kwa sababu kadhaa pamoja na hilo la pombe. Kibaya zaidi wameamua kumtafutia mchumba kabisa anadai ni kabinti kazuri tuu.
Sasa anaomba ushauri, atumie njia gani yakumuacha huyo mwanamke bila kumsababishia maumivu?
Najua kuna watu humu wameshawahi kuyapitia haya.
Karibuni kwa maoni yenu.
Yeye (rafiki yangu) aliamua kuondoka kwenda mkoa x kujitafuta baada ya kumaliza kidato cha nne na kukaa mtaani kwao bila muelekeo wowote.
Anasema Mungu si Athumani alipofika huko alijichanganya na kufanya shugli mbali mbali akafanikiwa kufungua kigoli (biashara) x, na katika mihangaiko hiyo alikujaga kupendana na mwanamke mmoja ambae ni single mother wa mtoto mmoja na wame hustle wote kwa muda wa miaka mitatu.
Wwaliamua kuishi pamoja ili kupunguza bajeti ya kila mtu kupanga chumba chake, ingawa hajawahi kwenda kujitambulisha kwao na mwanamke pamoja na mwenzake kumsumbua kuhusu hilo.
Jamaa anadai huyo mwanamke yuko vizuri na anampenda kwa sababu wamekuwa wanasaidiana na kuvumiliana kwa vingi isipokuwa huyo mwanamke amekuwa na tabia ya kutumia pombe na jamaa hapendi na amekwisha muonya na kumshauri aache lakini mwanamke hasikii, na jamaa anashindwa kumpiga chini kwasababu mwanamke anampenda sana na wamesota sana mpaka jamaa kusimama kiuchumi si haba.
Sasa issue imekuja baada ya jamaa majuzi kutembelea nyumbani kwa wazazi wake anadai wamemsakama sana kuhusu kuoa wanadai amekuwa sasa, na amewaficha kama anaishi na mwanamke kwasababu anahisi hatoweza kutimiza ahadi za kumuoa kwa sababu kadhaa pamoja na hilo la pombe. Kibaya zaidi wameamua kumtafutia mchumba kabisa anadai ni kabinti kazuri tuu.
Sasa anaomba ushauri, atumie njia gani yakumuacha huyo mwanamke bila kumsababishia maumivu?
Najua kuna watu humu wameshawahi kuyapitia haya.
Karibuni kwa maoni yenu.