Jile79
JF-Expert Member
- May 28, 2009
- 17,668
- 13,271
aloycious, Jile79, MR UNINFORMED
Kawaida mwanadamu anajifanya mjuaji, lakini mambo yako wazi ! Biashara ina mabo mawili, 'faida' na 'hasara'
Biashara katika Uislaam inasimamia hapo, kuwa mna share faida au hasara. Lakini mtoza 'riba' yeye hawezi hata siku moja kukubali kubeba hasara, ndio maana anashikilia hati yako ya nyumba.
Mwenyezi Mungu anasema kuwajibu wale wasio amini na wanaoendekeza riba:
'Wale walao riba hawasimami ila kama anavyo simama aliye zungwa na Shetani kwa kumgusa. Hayo ni kwakuwa wamesema: Biashara ni kama riba. Lakini Mwenyezi Mungu ameihalalisha biashara (profit and loss) na ameiharamisha riba. Basi aliyefikiwa na mawaidha (ujumbe huu ) kutoka kwa Mola wake Mlezi, kisha akajizuia (kushiriki biashara ya riba hata kama nyuma huko aliwahi kufanya) basi yake ni yaliyo kwisha pita (amesamehewa) na mambo yake yako kwa Mwenyezi Mungu. Na wenye kurudia (wabishi) basi hao ndio watu wa Motoni, humo watadumu.
Na Mwenyezi Mungu huiondolea baraka riba, na huzibariki sadaka. (ndio maana mabenki yana filisika !)
Enyi mlio amini (Waislaam) Mcheni Mwenyezi Mungu ! na acheni riba zilizo baki (compound) ikiwa nyinyi ni Waumini.
Basi mkifanya jitangazieni vita na Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Na mkitubu (mkiacha) basi haki yenu ni rasilimali zenu. Msidhulumu wala msidhulumiwe.
Qur'an: 2: 275- 279.
Ni kwa nini kila mara waislamu wanapenda kusema "katika uislamu"????? badala ya kuzungumzia economic principles?
Hata Lipumba muislam aliyebobea kwenye uchumi anaweza kukusaidia na hatasema kuhusu "katika uislam"
Ukiingiza sn imani unajikuta "ktk uislam unaruhusiwa vitu vingi wake wengi, kuua, etc