Msaada: Ufafanuzi juu ya Islamic Banking

Msaada: Ufafanuzi juu ya Islamic Banking

Faida ya Nani? Kama aliyekukopesha anafaidika na kukopesha FAIDA INATOKANA NA NINI? USIJITIE UPOFU

Usikurupuke, ndio maana ukaambiwa hakuna mkopo wa pesa! It's a business transaction, benki inafanya biashara na wewe, wanakuuzia bidhaa! Kuna mtu ameweka maelezo hapo nyuma, jaribu kusoma kwanza...! Au ulitegemea uuziwe bila faida?
 
Kwa ulewa wangu biashara ni mfumo ambao unachukua bidhaa unahiweka sokoni kusubiri wateja. Sasa hii ya kukununulia kisha aongaze cha juu MMMH, May be lakini napata wasi wasi sana kama kuna harufu ya riba.
 
Labda kwa hiyo system nyingine ambayo benk inatoa mtaji mimi nafanya biashara kisha tunagawana faida. Kama hiyo system hipo basi labda hiyo ndiyo itakuwa halali.
 
Kwa ulewa wangu biashara ni mfumo ambao unachukua bidhaa unahiweka sokoni kusubiri wateja. Sasa hii ya kukununulia kisha aongaze cha juu MMMH, May be lakini napata wasi wasi sana kama kuna harufu ya riba.

Kama uelewa wako wa biashara umeishia hapo lazima uwe na wasiwasi. Hujawahi kusikia watu wanatoa order watengenezewe kwa mfano mashine fulani (haipo sokoni)? Au unatoa order kwa supplies/logistics companies (hawana bidhaa sokoni) wakununulie bidhaa fulani unayohitaji?
 
Kwa hiyo system ya kukununulia naona uhalali ungekuwepo kama benk ingekuwa na Showroom, Nyumba za kuuza au hata Mduka kwa ajili ya kuwakopesha watu bidhaa na si hiyo ya kuongeza cha juu. Tuwe makini waislamu ndiyo maana Allah katuambia tusome ili tusiburuzwe buruzwe.
 
Kama uelewa wako wa biashara umeishia hapo lazima uwe na wasiwasi. Hujawahi kusikia watu wanatoa order watengenezewe kwa mfano mashine fulani (haipo sokoni)? Au unatoa order kwa supplies/logistics companies (hawana bidhaa sokoni) wakununulie bidhaa fulani unayohitaji?

Yah ninakuelewa vizuri,
Lakini hao supplier huwa wanaenda kununua viwandani ili haweze kuku uzia bei iliyopo sokoni na si kwenda kuchukua kwa jirani na kuongeza dhamani kidogo huo ni uhuni. Samahani kama nitakuwa nimekosea maana siyo mtaalamu sana kwenye biashara.
 
Yah ninakuelewa vizuri,
Lakini hao supplier huwa wanaenda kununua viwandani ili haweze kuku uzia bei iliyopo sokoni na si kwenda kuchukua kwa jirani na kuongeza dhamani kidogo huo ni uhuni. Samahani kama nitakuwa nimekosea maana siyo mtaalamu sana kwenye biashara.

Hapana ndugu yangu, si lazima akanunue kiwandani, biashara ni somo pana ndio maana watu wanasomea. Ukiniambia unatafuta iphone 6s nikaenda kuinunua then nikakuuzia (kwa faida) hiyo haiwi biashara?
 
Hapana ndugu yangu, si lazima akanunue kiwandani, biashara ni somo pana ndio maana watu wanasomea. Ukiniambia unatafuta iphone 6s nikaenda kuinunua then nikakuuzia (kwa faida) hiyo haiwi biashara?

Hapo naona kama utakuwa unafanya kazi ya Udalali maana mfabiashara atakuwa ni huyo ambaye umeenda kuchukua simu kwake.
Na kwa vile hii kitu imekaa kiimani zaidi kwa nini ukachukue kwa jirani huje umuuzie kwa kiongeza kidogo badaya ya wewe kumuelekeza aenda kwa jirani akanunue mwenyewe? Au ni kwa sababu yeye anakuwa hana cash ndiyo umfanyie hivyo?
 
Biashara huwa inakuwa na asilimia ya hasara sasa hiyo kukununulia kwa kuongeza cha juu sioni hata asilimia moja ya hasara
 
Biashara huwa inakuwa na asilimia ya hasara sasa hiyo kukununulia kwa kuongeza cha juu sioni hata asilimia moja ya hasara

Au uwezekano wa benki kupata hasara yoyote.
 
kabla ya kujiunga lazima ujifunze kuwa na hasira,ugomvi, jaziba,chuki nk hapo utakuwa umewiva kweyikweyi

Hivyo ndivyo mnavyodanganyana, hakuna dini kwa Mwenyeezi Mungu zaidi ya kujisalimisha kwake na kufata maamrisho yake yeye Mwenyeezi Mungu mmoja ambae hajazaa wala kuzaliwa.

Hakuna amani na mafunzo ya amani zaidi ya Uislam, kumbuka hilo, usingoje kuhadithiwa, jisomee.
 
Hapo naona kama utakuwa unafanya kazi ya Udalali maana mfabiashara atakuwa ni huyo ambaye umeenda kuchukua simu kwake.
Na kwa vile hii kitu imekaa kiimani zaidi kwa nini ukachukue kwa jirani huje umuuzie kwa kiongeza kidogo badaya ya wewe kumuelekeza aenda kwa jirani akanunue mwenyewe? Au ni kwa sababu yeye anakuwa hana cash ndiyo umfanyie hivyo?



Umesema wewe ni muislamu? Soma kitu kinaitwa "Murabaha" labda kwa upande wa kiimani utaelewa zaidi. Je kama huyo uliyeenda kuchukua kwake ni wholeseller kwa mfano? Unataka kuniambia kwa mfano Wamachinga wanaponunua nguo moja moja pale Ilala (Karume) halafu wakaja kukuuzia kwa faida ilibidi wakuelekeze ukanunue mwenyewe? Wanaofanya ni udalali na uhuni? Etc etc
 
.
Na kwa vile hii kitu imekaa kiimani zaidi kwa nini ukachukue kwa jirani huje umuuzie kwa kiongeza kidogo badaya ya wewe kumuelekeza aenda kwa jirani akanunue mwenyewe? Au ni kwa sababu yeye anakuwa hana cash ndiyo umfanyie hivyo?

Sababu ni nyingi, kama vile unapomwagizia mchuuzi kesho akuletee samaki wakati ferry unapajua, au chinga akuletee kiatu aina fulani wakati vinapouzwa unapajua.
Vile vile, dalali hanunui ili akauze. Anachofanya ni kuwakutanisha muuzaji na mteja au umpe hela yeye akakununulie. Tofauti na anayenunua kwa pesa zake ili auze (anaitwa mfanyabiashara).
 
Really? Profit na interest ni kitu kimoja?

Tuchukulie mfano wa aliyesema ukitaka nyumba inayouzwa kwa milioni 40, wanainunua halafu wanakuuzia kwa milioni 50. sasa hapo suala la profit au business sharing lipo kweli au ni interest katika lugha nyingine?

By the way, hicho unachokiita interest in a true context tukiacha mbwembwe za lugha, si ndio profit yenyewe kwa benki? Interest si ndio inayodefine tofauti kati ya cost na revenue katika ukopeshaji? sasa si ndio profit yenyewe?
 
ALLAH ameharamisha riba na amehalalisha biashara mnatakiwa kuelewa hilo.

Riba nayo ni biashara..ila yenyewe ni biashara ya pesa kwa pesa...badala ya biashara ya pesa kwa mali/bidhaa. Sioni tofauti nyingine hapo zaidi ya msamiati tu!
 
watu wabish sana na hawatak kuelewa kila wanavyoelekezwa
 
Back
Top Bottom