Msaada: Nina Millioni 10 itatosha kujenga nyumba?

Msaada: Nina Millioni 10 itatosha kujenga nyumba?

Nunua carry fanya biashara ujenge nyumba na sio kachumba
Wewe unamrisha matango mwenzako. Ashasema ana milioni 10 anataka kujenga Nyumba. kwahiyo hapo inaonesha ana maisha simple. Sasa wewe hiyo kirikuu hela ya service ataitoa wapi. Wakati Nyumba ni asset na gari ni luxury.
 
Afu chini afunge matairi ya trekta,asee ni ubunifu mkuu maana si Tanesco wala Dawasco(kama Dar) wataenda kudai bili zao,lazima wasahau tu wakidhani ni Gari LA mizigo[emoji3] [emoji3] [emoji3]

[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Inatosha mkuu kama kajumba katakuwa very simple nakumbuka Mara ya mwisho nimesimamia vyumba viwil dar haikufika hata milion 6 .

Ila mbwembwe ndio zinazo maliza hela mkuu nyumba ni tofali plasta,bati,mbao, mlango na madirisha plus choo
 
Afu chini afunge matairi ya trekta,asee ni ubunifu mkuu maana si Tanesco wala Dawasco(kama Dar) wataenda kudai bili zao,lazima wasahau tu wakidhani ni Gari LA mizigo[emoji3] [emoji3] [emoji3]
hata gari lenye ziro cc linalipiwa tra.
 
Kiwanja ninacho kipo poa tu, ishu ni hicho kihouse
Jenga kajumba ka nyuma uhamie kwako! Kubwa utajenga taratibu ukiwa kwako. Kanakuwa simple vyumba viwili, sebule choo na bafu. Sebule inakuwa dinning pia! Bora unaamkia kwako kuliko kudaiwa kodi huku jamaa kafunga taulo kiunoni!
 
Kama una eneo kubwa la kutosha, nakudhauri ufanye moja kati ya haya;
1. Jenga vyumba viwili, sebule na jiko. Tumia eneo la pembeni mwa kiwanja/eneo lako, iwe simple, mabati ya kawaida sana. Baadae ukipata pesa utajenga nyumba kubwa kwenye eneo hilo hilo, then hiyo utaifanya kuwa ya mpangaji.

2. Jenga foundation yote kwa ramani unayopenda, isiwe kubwa coz ikiwa kubwa sana pesa yote itaishia chini. Then pandisha chumba na sebule tu, baadae utaongeza kadri uwezo unavyoruhusu.

Kujenga sio kazi rahisi.
 
Kuna watu wanajenga za nyumba za laki kadhaa.

Acha matusi mkuu huku mtaani ni pagumu sana unatuumiza unapotaja mamilioni ya pesa.

Unapopambana hali yako, usitingishe za kwetu.
 
Jenga kajumba ka nyuma uhamie kwako! Kubwa utajenga taratibu ukiwa kwako. Kanakuwa simple vyumba viwili, sebule choo na bafu. Sebule inakuwa dinning pia! Bora unaamkia kwako kuliko kudaiwa kodi huku jamaa kafunga taulo kiunoni!
Kweli mkuu
 
Mnachukulia poa nyumba ya vyumba vitatu jamani.
Nina jua ninajua chongumza nina uzoefu na hizi kazi,nyumba ndogo ya kawaida vyumba vitatu haiwezi maliza tofari 3,000 ambazo ni sawa na 3,000,000.nyumba ya vyumba vitatu haiwezi maliza mabati 100 tuseme kila bati 15,000 inakula 1,500,000.tofauri 3,000 kujengea haziwezi maliza mifuko 50 @13,000 inakuja 650,000 hapo bado fundi wa ujenzi let say 900,000 unabakiza hela mbao za kuezekea na mchanga na fundi wa kuezeka,piga jumla kama hapo 10M imekwisha au bado
 
Kiwanja ninacho kipo poa tu, ishu ni hicho kihouse
Hizo pesa zitatosha hata nyumba ya vyumba vitatu self contained yaani choo, bafu, jiko, sebule na kavaranda. Cha kuzingatia ni lazima design yake iwe very compact, built up area isizidi 54 square meters. Tumia matofali ya kuchoma. Tumia changarawe kwenye base ya floor. Msingi tumia matofali ya cement au mawe kutegemea yapi ni nafuu huko kwenu. Tumia mabati ya kawaida ya gauge 30, dari la kawaida, wiring ya kawaida, plumbing ya rahisi, plastering ya cement, rangi ya maji kwenye ukuta na ceiling board za kawaida, madirisha na milango ya kawaida achana na aluminium windows. Tumia fundi mmoja wa kawaida na vibarua wasiozidi 2. Cesspit za rahisi.

Note; Design ndiyo most important, unaweza kupata ushauri kwa mafundi. Hususani chumba cha kulala 2.5m by 3m kinatosha, sitting room 3m by 3.5m, master bedroom 3m by 3m, jiko 2m by 2.5m, bafu cum choo 1.5m by 2m, stoo 2m by 2m.
 
Back
Top Bottom