Mbwa kala mbwaa
JF-Expert Member
- Apr 16, 2013
- 219
- 391
- Thread starter
- #61
Hatua ya kwanza: jisamehe wewe mwenyewe, samehe yeyote unayedhani amewahi kukukosea, samehe wote uliowakosea.
Hatua ya pili: Tazama maisha kwa mbele (yaani future), achana na ya nyuma (past events), panga mipango ya kuboresha maisha ya kesho.
Hatua ya tatu: Mawazo ya kujiua ni mawazo ya kuona maisha hayana thamani, achana nayo, unathamani kubwa sana kuliko binadamu yeyote (aliye hai au aliyekufa); kumbuka, hujafanana na binadamu yeyote, hivyo na dhamani yako haiwezi kulinganishwa na mtu au kitu kingine chochote.
Hatua ya nne: Jikumbushe jambo au tukio maishani ambalo limewahi kukupa furaha na amani ya nafsi. Kila wazo la kujidhuru linapokuja akilini, geuka mara moja na kutafakari jinsi ilivyokuwa burudani kwa tukio la furaha.
Hatua ya tano: Rudia hatua ya nne mara kwa mara. Utashangaa baada ya muda wazo baya hukosa nguvu na taratibu hutoweka kabisa kwenye fikra zako.
This is awesome!
Nitazingatia mkuu cabhatica
Last edited by a moderator: