Msaada: Nataka kubadilisha cheti changu kuzaliwa pamoja na baadhi ya herufi za majina yangu na mama yangu

Msaada: Nataka kubadilisha cheti changu kuzaliwa pamoja na baadhi ya herufi za majina yangu na mama yangu

Mlume Ndago

Member
Joined
Jul 28, 2025
Posts
41
Reaction score
53
Habari wakuu,
Poleni na msiba wa kitaifa tunaoendelea kuuomboleza.

Moja kwa moja nijikite kwenye mada husika kwa kuwaomba msaada wa mawazo na ushauri kwa ujumla.

Mimi nina cheti cha kuzaliwa lakini cheti changu ni cha zamani sana kimetoka tangu mwaka 1988.
Katika cheti changu jina langu limekosewa herufi moja ya mwisho, na majina ya mama yangu pia yamekosewa mawili la kwanza na la mwisho katika yale majina yake matatu .
Msaada ninaohitaji ni kujua;

1.Endapo nitaenda ofisi za RITA nahitajika kwenda na nyaraka zipi ili niweze kurekebishiwa jina langu na majina ya mama yangu?
2.Je, naweza kwenda ofisi yoyote ya RITA iliyo karibu nami katika wilaya yoyote Tanzania au lazima niende katika ofisi ambayo ipo katika wilaya niliyozaliwa?
Yangu ni hayo tu, naombeni ushirikiano wenu kwa yeyote mwenye kujua au kufahamu anaweza kutoa ushauri au msaada kwa ku comment
Asanteni na muwe na siku njema...🙏
 
Hivi Bado mnaendanga ofisini kwa huduma zinazopatikana online? Binafsi physically ntaenda hospital na labda kikao
 
Ndiyo kazi ninayoifanya muda huu.

Kila kitu siku hizi unaweza kufanyia online.

Ingia hapa: erita.rita.go.tz utajisajili kisha utaenda kwenye Birth Servicesz kisha utaenda Old to New Application ili kupata cheti kipya.
20251109_181950(1).jpg


Note: Kwa case yako, kama jina lako lilikuwa limekosewa, ina maana na kwenye docs zingine kama za shule na nida si zitatofautiana ukibali jina?
Ukiamua kubadili jina basi hakikisha linaendana na docs zako zingine zooote.
 
Nahitajika kwenda na chazamani? Na hakutakuwa na nyaraka nyingine zinazohitajika ili kupata hicho kipya?
Achana na hicho cha zamani omba kingine.

Pale kwenye kujaza taarifa zako penye kutumia vitambulisho vingine kama NIDA au Leseni unaweza skip tu mwanzoni ila hatua za mwisho ndo kuna option ya kuupload at least viambatanisho viwili vya kukuthibitisha wewe.
 
Ndiyo kazi ninayoifanya muda huu.

Kila kitu siku hizi unaweza kufanyia online.

Ingia hapa: erita.rita.go.tz utajisajili kisha utaenda kwenye Birth Servicesz kisha utaenda Old to New Application ili kupata cheti kipya.
View attachment 3499454

Note: Kwa case yako, kama jina lako lilikuwa limekosewa, ina maana na kwenye docs zingine kama za shule na nida si zitatofautiana ukibali jina?
Ukiamua kubadili jina basi hakikisha linaendana na docs zako zingine zooote.
Kwa scenario yake Old to New itamsumbua maana kasema kuna taarifa hazipo sahihi kwenye hicho cha zamani
 
Ndiyo kazi ninayoifanya muda huu.

Kila kitu siku hizi unaweza kufanyia online.

Ingia hapa: erita.rita.go.tz utajisajili kisha utaenda kwenye Birth Servicesz kisha utaenda Old to New Application ili kupata cheti kipya.
View attachment 3499454

Note: Kwa case yako, kama jina lako lilikuwa limekosewa, ina maana na kwenye docs zingine kama za shule na nida si zitatofautiana ukibali jina?
Ukiamua kubadili jina basi hakikisha linaendana na docs zako zingine zooote.
Documents zangu zote majina yanafanana hakuna shida kuanzia vyeti vya shule, NIDA n.k
Isipokuwa cheti cha kuzaliwa tu
 
Ndiyo kazi ninayoifanya muda huu.

Kila kitu siku hizi unaweza kufanyia online.

Ingia hapa: erita.rita.go.tz utajisajili kisha utaenda kwenye Birth Servicesz kisha utaenda Old to New Application ili kupata cheti kipya.
View attachment 3499454

Note: Kwa case yako, kama jina lako lilikuwa limekosewa, ina maana na kwenye docs zingine kama za shule na nida si zitatofautiana ukibali jina?
Ukiamua kubadili jina basi hakikisha linaendana na docs zako zingine zooote.
Nikipata cheti kipya kama ninavyotaka basi docs zote zitakuwa zinafanana.
Ila nimejaribu kuingia kama ulivyonielekeza lakini hawanitumii E-mail ya ku activate akaunti
Screenshot_20251109_193409_Samsung Internet.jpg
 
Ndio maana nikauliza kuomba chengine zinahitajika nyaraka zipi na zipi?
Na je kama itatokea nimeulizwa cheti changu cha awali kimeenda wapi au kipo wapi nijibu vipi?
Kuna list ndeefu ya nyaraka unazoweza kuambatanisha, ila minimum zinahitajika 2.

Unaweza kuweka Birth Cert ya zamani NIDA ID, Voter ID, Hati ya Kusafiria, NIDA/Voter ID za wazazi.
 
Back
Top Bottom