Msaada kutokomeza wezi?

Msaada kutokomeza wezi?

Mama yangu anafanya hii kitu plus mitego kila kona. Anaweka masinia na masufuria milangoni na madirishani. Bila kusahau filimbi chini ya mto
Dah bro hii ni pasaka , nashukuru kwa kuniongezea siku .

Pasaka njema
 
Kuna alarm systems zinauzwa Alibaba, zinatumia solar, ni vidogo ila wapuuzi wakikaribia tu usiku kinapiga kelele za kufa MTU. Lazima utaamka tu. Vinauzwa pesa ndogo kama dollar 10 hivi
Huna picha zake ndugu? Mimi nazitaka ili wanakijiji waseme mimi mchawi
 
Mbwa wako hawajapewa mafunzo ndugu.
Kwenye camera uliwaona wezi wako waliokuibia?
Niliwaona ila walivaa masks hatujawagundua. Waliwawekea sumu na kuwapulizia dawa. Hata sisi vyumbani walitupulizia dawa. Tumekuja kupata fahamu saa nne asubuhi.

Ilikuwa ni timu iliyojidhatiti waliingia ndani wawili na nje walikaa wawili. Mmoja rangi yake tunadhani ni mwarabu
 
Kwann usiseti timer yaani iwe active kufanya hiyo command muda ule ambao unataka.
Hamna hii imesetiwa ikiona hali tofauti yenyewe inapiga picha haijarishi ni mda gan
 
Uongo huu..hao walikuwekea security fake. Ile waya inapiga shoti ya hayari na alarm mtaa mzima wataamka. Na seting yake umeme ukiondolewa kwa njia yoyote inapiga alarm hakuna namna wanaweza kufanya kwenye fence ya umeme, labda hiyo uliwekewa ya buza kwa mama kibonge. CCTV camera za sasa hivi kazi yake sio tu kuchukua picha unaweka demarcation mtu akivuka tu eneo ulilozuia ina piga picha,alarm kubwa na inakupigia simu kukuamsha.
Jamaa walipitia getini tukio lilitokea 2018 na walicheza na utaalam wa juu sana kwenye kufungua geti kiasi kwamba ilibidi aliyefunga electric gate akamatwe ingawa pia alionekana hausiki. Ndani ya nyumba kulikuwa na gari nne ila wakatoka na moja waliyoitaka. Walinipigia hesabu zaidi ya miezi miwili kwani kuna siku walishafanya attemp ya kuliiba hilo gari ofisini Posta miezi miwili kabla ya kuja kulichukua home.

Mpaka leo sijalipata hilo gari na nimesha-give up
 
Hizo electric fence na CCTV camera wezi wanajua kuzichezea sema tu wasikuamulie, hizo sio kitu kwa mwizi alieamua kukuibia
Emu niambie mfano umeweka electric fence kwa mtaalamu anaejua kazi yako uyo mwzi ataichezeaje ili aweze kukata waya bila ya kin'gora kulia na wenye nyumba kushtuka...? Au bila kuogwa shoti
 
Jamaa walipitia getini tukio lilitokea 2018 na walicheza na utaalam wa juu sana kwenye kufungua geti kiasi kwamba ilibidi aliyefunga electric gate akamatwe ingawa pia alionekana hausiki. Ndani ya nyumba kulikuwa na gari nne ila wakatoka na moja waliyoitaka. Walinipigia hesabu zaidi ya miezi miwili kwani kuna siku walishafanya attemp ya kuliiba hilo gari ofisini Posta miezi miwili kabla ya kuja kulichukua home.

Mpaka leo sijalipata hilo gari na nimesha-give up
Tatzo hao wanatafuta mafundi ambao hata hawajui kufanya installation maana wanawekewa kwa bei rahisi mwsho wanaibiwa na wanasema eti electric fence haina maana au wez wanaichezea hawa jamaa vp
 
Emu niambie mfano umeweka electric fence kwa mtaalamu anaejua kazi yako uyo mwzi ataichezeaje ili aweze kukata waya bila ya kin'gora kulia na wenye nyumba kushtuka...? Au bila kuogwa shoti
Ule waya haukatwi maana ukiugusa vibaya tu Alarm inapiga na Alarm ni king'ora km gari ya Ambulance, pia waya unapiga shot kubwa yaan umeme wake ni mkubwa kiasi Cha kuua na kuchoma usicheze na zile waya mkuu we zione vile vile tu
 
Habari za leo wanajamvi?

Naleta kwenu mada hii nikiwa na majonzi baada ya leo alfajiri kupigwa flat yangu Hisense 55inch.

Wezi wamefungua lock za alminium window na kupindisha nondo kisha wakazama ndani na kufanya yao.

Kiukweli hii hali inaumiza sana.

Naombeni ushauri wa security gani ya kuweka kuwazuia hawa watu.
Kuwazuia haiwezekani labda kuwapunguza.
Solution: katia bima vitu vyako vyote hii ni njia salama maana hata ukiibiwa bima itakurudisha ulipokuwa, na kwa gharama ya hiyo TV bima haiwezi kuzid lak moja kwa mwaka
Pole
 
Tatzo hao wanatafuta mafundi ambao hata hawajui kufanya installation maana wanawekewa kwa bei rahisi mwsho wanaibiwa na wanasema eti electric fence haina maana au wez wanaichezea hawa jamaa vp
Zile waya zinachezewa vizuri tu na wezi wanapita usibishe mkuu, siku hizi dunia ni km Kijiji tu hakuna kinachoshindikana km huna ujuzi usiguse zile waya, wezi hujaribu km zina Moto au hazina moto kwa kumpandisha nyoka km nyoka akiungua wezi hawagusi zile waya
 
Kuwazuia haiwezekani labda kuwapunguza.
Solution: katia bima vitu vyako vyote hii ni njia salama maana hata ukiibiwa bima itakurudisha ulipokuwa, na kwa gharama ya hiyo TV bima haiwezi kuzid lak moja kwa mwaka
Pole
Bima ya Vyombo vya Electronics au?
 
Tatzo hao wanatafuta mafundi ambao hata hawajui kufanya installation maana wanawekewa kwa bei rahisi mwsho wanaibiwa na wanasema eti electric fence haina maana au wez wanaichezea hawa jamaa vp
Mzee kwangu sijaweka kitu fake hata kimoja. Hata hiyo gari waliiba kwa sababu ya gharama yake. Vitu vyote vilifanywa na kampuni kubwa na nililipiwa na ofisi kama sehemu ya usalama wangu.

Kesi ilifika mpk kwa viongozi wote wa juu wa usalama na pia iliundwa timu ya upelelezi ambayo ilipewa mpk ofisi ya muda pale polisi Oysterbay kituo kipya
 
Back
Top Bottom