Chiwa
JF-Expert Member
- Apr 17, 2008
- 4,150
- 5,019
inaweza kuzidi ikafika hata milioni sita ila kwa milioni mbili anaweza kuhamia.Kwahio bajeti haitakuwa 2m tena itakuwa 2.3m
nasema hivi ninao mfano hai mwaka 1976 babu yangu alisumbuliwa na mwenye nyumba mjini dar ikabidi aamue kuhama na kuhamia nje ya mji kwa siku ya kwanza tulilala nyumba imefungwa vito tuu lakini bati imepigwa na nakumbuka vilikuwa vyumba viwili na sebure.
siku ya pili upande mmoja ukakandikwa kwa udogo na ndani ya wiki mbili nyumba yote ilikwisha.
ninachokumbuka babu alimlipa fundi wa kufunga fito na kupiga bati na pia kununua fito,kamba na mijengo lakini zoezi la kukandika tulifanya wenyewe babu akikanda udongo mimi, mkewe na shemeji yake tukikandika nyumba.
lakini baadaye palibadilika tukajenga nyumba nzuri na yamaana.
ninachotaka kusema kikubwa hapa sio fedha kiasi gani inatosha kujenga lakini kubwa je unao msukumo wa kutosha toka katika nafsi yako na roho yako na utashi wako kwamba umepania kuhama na kujenga?
kwa hiyo kwa chochote tufanyacho tunatakiwa tuamini kuwa kinawezakana, tufanye sehemu yetu na mwisho kitakuwa.
ziko success story nyingi ambazo nikikueleza hauwezi amini nimeshuhudia nikiwa mwanzo siamini lakini leo nayaona mafanikio yao na najifunza kutoka kwao.