Msaada: Gharama za nyumba ya vyumba viwili

Msaada: Gharama za nyumba ya vyumba viwili

Unaweza mkuu...usiwasikilize wanaosubiri maimilioni, adha ya kupanga ni mbaya sana, unajega vizuri na zaweza kubaki, fundi mmoja tu, wewe msaidizi..na unahamia safi kwako...
Kabisa jf imejaa walioshindwa kazi yao kukatisha tamaa wengine.
 
Kumbe tunaweza kidogo kidogo ngoja namiye nijichange nijisukume. Uzi mzuri sana huu nasubiria aliyejenga kabisa kwa kama m5 hivi.
 
Tofari 1400@1000 ni1,400,000.inabaki laki sita .fundi bado,mchanga bado,kokoto bado,mbao bado,nondo bado,maji bado bati bado,misumari bado,kuchimba msingi bado,madirisha na milango bado ,fundi hajaiba kidogo.Labda ujenge mbavu za umbwa.
Acha kudanganya watu. Vyumba viwili tofali 1400?
 
Tofari 1400@1000 ni1,400,000.inabaki laki sita .fundi bado,mchanga bado,kokoto bado,mbao bado,nondo bado,maji bado bati bado,misumari bado,kuchimba msingi bado,madirisha na milango bado ,fundi hajaiba kidogo.Labda ujenge mbavu za umbwa.
Gharama ya kujenga tu vyumba viwili ni Laki 3 bila bati hapo,Ila akiamua anaweza mambo ni kidogo kidogo
 
Mkuu unajenga na chenji inabaki.

-Chumba na sebule ni tofali 800 tu. = 800,000/=
-Bati 15 = 150,000/=
-Cement Mifuko 10 = 140,000/=
-Ufundi 270,000/= Msingi hadi Juu
-Linta Nondo 6 na Mifuko miwili ya cement Kokoto Viroba 12,Mchanga Yebo moja = 182,000/=(120K+12k+50k)
-Mbao 20(4x2 and 2x2) + Misumali =150,000/=
-Mlango m1 na madirisha matatu = (150k +50k x3 ) =300,000/=

Total ni 1,992,000/=

Hayo ni Mahesabu Maximum sana,Kuna vitu unaweza kupunguza kwenye bei ya mlango,dirisha au kwenye bati unaweza ukanunua zile za reject ambazo nzuri kwa 6000 na sio kwa elfu 10.

Kwenye ufundi mnaweza mkabargain kwa tofali mie nimeweka 250 kuna mafundi wa kitaani hadi 200 kwa tofali.
Choo vipi?
Ceiling board/gypsum?
Vifaa vya umeme?
Plumbing?
Plaster/rangi?
Rough floor ndani?

au anapanga matofali tu anaishi bila umeme,maji na choo?
 
Wewe hyo pesa inatosha kabisa hata ukipungukiwa ni kidogo sana.ila mafundi wa dar wana bei ukiweza tafuta wa mkoan wana bei nzuri,M2 itakufikisha sehemu utabakiza finishing tu na hiyo utaifanya ukiwa umeshahamia.hao wanao kutisha wamejenga??na kama wamejenga basi vipato vyao si haba.mwanaume kaza biti aanza ujenzi haraka sana iwezekanavyo.kwanza nakupongeza kwa kupata uwanja.wewe ni dume la ukweli kama Mimi,ukinihitaji kwa mawzo Niko tayari kukusaiidi 24/7
 
Tafuta wataalamu wakusaidie kwa kuwa humu wengi ni wenye wivu wasio jua chochote juu ya ujenzi na wakatisha tamaa.
 
tofali nimeulizia wanauza elfu moja had site usafir juu yao ila sijajua vyumba viwil zinaingia tofar ngap na fund anajenga kwa tsh ngap
huku kwenye jf hutapata suluhisho. kila mtu ana gari, anaishi maisha mazur amejiajir na amefanikiwa! watakukatishi tamaa. ulizia fundi wa mtaani kwako
 
Habari zenu wakuu,

Kwenye shughuli zangu za hapa na pale nimepiga bingo nna milion mbili cash ndani nataka kuondokana na maisha ya kupanga nna kiwanja Goba-Mbezi, je nitaweza kujenga vyumba viwili nikaamia kwa gharama ya milioni2.

Msaada wenye uzoefu please
Inategemea...itakuwa ya kiwango kidogo
 
Ukija pm nitakupa ushuhuda wangu,na naamin hitajuta na utaanza ujenzi Mara moja.kwa kuwa una kiu ya kuhamia kwako inawezekana kabisa,usirudi nyuma tafadhari
 
Wewe hyo pesa inatosha kabisa hata ukipungukiwa ni kidogo sana.ila mafundi wa dar wana bei ukiweza tafuta wa mkoan wana bei nzuri,M2 itakufikisha sehemu utabakiza finishing tu na hiyo utaifanya ukiwa umeshahamia.hao wanao kutisha wamejenga??na kama wamejenga basi vipato vyao si haba.mwanaume kaza biti aanza ujenzi haraka sana iwezekanavyo.kwanza nakupongeza kwa kupata uwanja.wewe ni dume la ukweli kama Mimi,ukinihitaji kwa mawzo Niko tayari kukusaiidi 24/7
Mnamuhadaa huyo jamaa,2m I taisha na attendees kupanga.
 
Haiwezekani, ifanyie biashara uzalishe hiyo pesa..
 
Kama eneo lako ni la mchanga basi chimba shimo la choo ili mchanga unaotoka hapo upigie tofali, kwa pesa hiyo ukiisimamia vzur chumba kimoja unajenga
 
Back
Top Bottom