Msaada: Anapost sana picha zake Insta na Facebook

Msaada: Anapost sana picha zake Insta na Facebook

Juzi tu nimetoka kupiga mtu chini mambo hyahya ya kitoto kwenye ishu siriaz!
 
Nahisigi hilo ila inanipa taabu sana hawezi kustahimil vitu vidogo km kutopost picha ya ndan siitakuwa balaa na nikimudhi lazima aniweke DP ya ujumbe unaonihusu
Haaaaaahaaaaaaaa yaani we jamaa km mimi tu kiugomvi kdg lazma wabadili DP ss km c utoto ni nn? vijembe km wake wenza? dawa ni kuvipiga chini tu vikija pata akili too late nna uhakika utashindwa tu kuna mdau hpo kashauri "km unampenda nenda nae taratibu" ni ushauri mzuri jaribu mi nlivumilia mwisho nkashindwa!
 
Halafu kingine nilichoona hapo ni kama vile huyo dada ni mswahili. Jitahidi kudate na wanawake wanaojitambua, sio hao wenye Mambo ya kiswahili.
Viswahili sana hv vitoto mm juzi nimekapiga chini kamoja imetokea kutoelewana mnaongea yanaisha mambo ya kuwekeana mabango profile ya nn? inankera sana hyo tabia!
 
Huyu yupo mguu ndani mguu nje.Bado anajinadi sokoni.Be careful.Watch it!
 
Mkuu, moja katika vitu tunavyokosea sana ni kupenda nusu Package halafu tukitegemea kufurahia the whole package. Mwili wa mwenza wako ni nusu package, tabia yake ni nusu nyingine. Sasa huwa aidha tunavutiwa na tabia ama Urembo. Hapo wewe ni wazi, kinachokufunga ni urembo wake. Lakini tibia yake isha kukera. Mwenza mwema anatakiwa angalau akufurahishe nusu nusu kila upande(urembo na tabia).
 
Hiyo ni interest yake!!! Ilimradi hapost nje na maadili na secret zenu basi sioni taabu!! Utampoteza mdada kwa vitu visivyo na tija
 
ana umri gani mkuu?
anapenda kuwa modal au video queen anapenda sana kupiga picha!
me wa kwangu yupo kama wako tu nampenda ivoivo mwanzon nilihis kama ww lakini mwisho wa siku nilikuja kujua ukweli kwamba ni kwann yupo hivo. wapo watu wazima pia wana interest hizo za kupenda kupga pcha sana

ukiangalia hii picha unamuona pia mkuu wangu vile anavopenda kupiga picha
d253191f9a0ac29276e18dec01e72fcd.jpg

kwaiyo huyo wa kwako mchunguze sana utapata jibu me kwa kwangu amenipa passwrd za insta na facebook kwaiyo nikiamua mda wwote huwa nachungulia dm na inbox kwake kuna nini
 
Hili linanipasua kichwa acha kila nikiwaza ila mwanamke yupo tayari kubadli dini nakuolewa na mimi ila nimemwambia mm siwezi kukuoa ndo ubadili dini kama unataka tuoane badili tukiwa wapenzi hadi ndugu zako wajue umebadilika ila sio kwenye ndoa ndo ubadili

Ndo mana anajitafutia zake mtu mwingine mwenye imani yake mtandaoni. Ukija kushtuka picha anazopost zimempa mume.shangaa tu.
Kubadili dinj unadhani kazi ndogo
 
Habarii wakuu
Nampenzi wangu nampenda sana tuna miaka miwili kwenye uhusiano yeye mwislamu na mimi mkristo ananipenda sana hilo sina mashaka nalo ila shida yake anapenda sanaa kupost picha instagram hata ambazo kwangu naona hazina tija au kupost kwa mwanamke alonampenzi na anatarajia kuwa mke wa mtu nishamuonya sanaa yaani hata akifumua nyewele yeye anapost tu.

Naombeni msaada wa mawazo nifanyaje manake hana privacy na ninwepesi kuomba msamaha ila lazima apost picha zake kama sio fb ni instagramu mpka nawazaga hizi " umependeza mpnz wangu huwa hazitoshi mpka likes na comment za mitandao"

Mh, mi nisingeweza vumilia huo ujinga, ila pia wanaume hatueleweki, akikwamini asilimia zote ukimtosa je? atakuwa ajaamua asilimia zote kuwa nawe ila hata simlaumu.
 
Back
Top Bottom