Kwa mwanasheriaOk ushauri wako tafadhari....
OK sawa mkuu ila mambo ya misiba Watanzania wana kawaida ya kusaidiana sana mwambie jamaa abadilike akipata matatizo hatokwenda Bank kuomba msaada watu anaowasaidia ndio watakaomsaidia pia watu wapo kazini ila kutoa Ten tuu pindi mtaani kukiwa na janga wanaona kama anatoa damu..Ok yeye anaishi mbali kidogo na huyu nduguye, sasa alihitaji pesa kurahisisha usafiri kwenda huko msibani na kujipanga kwa lolote la ziada.
Mkuu wanguNimepokea, taarifa usiku huu za rafiki yangu aliyepatwa na msiba mwishoni mwa mwaka jana na kuzika January mwaka huu.
Ni mtumishi wa serikalini kapatwa na msiba ghafla akaenda kukopa Bank ya ABC ili kumsaidia na masuala ya msiba, Tsh milioni 2 hiyo tarehe 29/12/2023.
Kaambiwa baada ya masaa 24 pesa itaingia ila hadi leo tarehe 8/01/2024 pesa hakuna na kwa taarifa ni kuwa, taarifa zake kwa mkuu wake wa kazi zimeishapita kasaini apewe mkopo ila kaambulia patupu hadi leo.
Msiba uliishaisha kwa msaada wa raia wema wakamkopesha akayamaliza huko kwao, sasa ndiyo naongea naye hapa anaomba ushauri jinsi ya kujitoa kwenye mkopo huu hewa.
Msaada kwa huyu ndugu kama ni wa kisheria ajitoe tu kwenye hili janga.
Sijakuelewa yaani msiba upo mikoani huku zaidi ya 1000km kutoka unapoishi halafu upatwe na msiba hao majirani zako wakuchangie nauli uende na kurudi?..OK sawa mkuu ila mambo ya misiba Watanzania wana kawaida ya kusaidiana sana mwambie jamaa abadilike akipata matatizo hatokwenda Bank kuomba msaada watu anaowasaidia ndio watakaomsaidia pia watu wapo kazini ila kutoa Ten tuu pindi mtaani kukiwa na janga wanaona kama anatoa damu..
Kwenye jamii tunazoishi tuna vitu vya mambo ya kusaidiana kwenye matatizo na mnakua kama group hata makazini vile vile ukiachilia mtaani kwa hiyo kila member anapopata matatizo ndani yenu kwa kanuni mlizojiwekea mnamchangia anafanya mambo yake na mchango wake unakua na muda watu tunawasafirisha kutoka Nje ya Nchi unazungumzia 1000Km...Sijakuelewa yaani msiba upo mikoani huku zaidi ya 1000km kutoka unapoishi halafu upatwe na msiba hao majirani zako wakuchangie nauli uende na kurudi?..
.pia washughurikie gharama zote za huko uendapo?
Duh..kwa hiyo title na ulivyoanza, nlnikadhani itaishia kuwa Bank wameng'ang'ania maiti hadi walipwe hela yao.Nimepokea, taarifa usiku huu za rafiki yangu aliyepatwa na msiba mwishoni mwa mwaka jana na kuzika January mwaka huu.
Ni mtumishi wa serikalini kapatwa na msiba ghafla akaenda kukopa Bank ya ABC ili kumsaidia na masuala ya msiba, Tsh milioni 2 hiyo tarehe 29/12/2023.
Kaambiwa baada ya masaa 24 pesa itaingia ila hadi leo tarehe 8/01/2024 pesa hakuna na kwa taarifa ni kuwa, taarifa zake kwa mkuu wake wa kazi zimeishapita kasaini apewe mkopo ila kaambulia patupu hadi leo.
Msiba uliishaisha kwa msaada wa raia wema wakamkopesha akayamaliza huko kwao, sasa ndiyo naongea naye hapa anaomba ushauri jinsi ya kujitoa kwenye mkopo huu hewa.
Msaada kwa huyu ndugu kama ni wa kisheria ajitoe tu kwenye hili janga.
Bank nyingi siku hizi zimevamiwa na watendaji wenye hulka za kihalifu. Na hawaogopi.Shukrani
Ok kwa huo mpango wenu mpo vizuri ila usitumie mfano huo kwa waajiliwa wengine (asilimia kubwa) ni pesa ya kifuta jasho tu kwa wafanyakazi wenzio ambayo ukiibadilisha kwenye matumizi inatoshamaji ya kunywa tu.Kwenye jamii tunazoishi tuna vitu vya mambo ya kusaidiana kwenye matatizo na mnakua kama group hata makazini vile vile ukiachilia mtaani kwa hiyo kila member anapopata matatizo ndani yenu kwa kanuni mlizojiwekea mnamchangia anafanya mambo yake na mchango wake unakua na muda watu tunawasafirisha kutoka Nje ya Nchi unazungumzia 1000Km...
wao si watachukua tu makato yao?Akishapokea hizo pesa azirejeshe tu kama malipo ya mkopo siku hiyo hiyo. Itakuwa haijaanza Riba.
Hizi bank huwa na vi terms and conditions vyakipuuzi sana.Tafuta Wakili atakupa ushauri mzuri zaidi, ila mimi nashauri akatae kuchukua hela kwa sababu bank wamekiuka masharti ya mkataba wa mpoko hela ilitakiwa kutoka ndani ya saa 24, imetoka nje ya muda mambo yake yameshindwa kufanyika kwa wakati....
Awaonyeshe jeuri zaidi aombe compersation aseme alikuwa na biashara na iyo hela ilikuwa ya kuagiza mzigo ambao ungeuzwa sikukuu mzigo ameuza kwa hasara sababu alichelewa kupata pesa kutoka ABC aombe 20M kama hasara aafu aacue mahakama iamue 😂
NB:Tafuta wakili mwenye roho mbaya