Paparazi Muwazi
JF-Expert Member
- Dec 23, 2007
- 310
- 79
Mbunge wa Bunge la JMT(CCM) ameponda hoja ya Kambi ya Upinzani ya kutaka mawaziri wasiteuliwe kati ya Wabunge. Bwana Mrope amesema kwamba taifa haliwezi kuokota mawaziri toka mitaani badala yake mawaziri lazima watokane na Wabunge. "Haiwezekani kuokota tu mtu mtaani. Lazima awe amepigiwa kura na kuchaguliwa na watu, hivyo napinga kabisa hao wanaosema mabunge wasiwe mawaziri". Bwana Mrope pia amewaponda wote wanaotumia mifano ya nchi nyingine duniani kujenga hoja yao. "Hao wanatumia mfano wa Marekani, hao Marekani wenzetu wameendelea, wana makompyuta kibao". Bwana Mrope alisisiza hoja yake huku akipigiwa makofi na wabunge walio wengi. Mheshimiwa Mrope aliyasema hayo wakati akichangia muswada wa uendeshaji wa Bunge unaojadiliwa hii leo.
PM
PM