Hiyo yote ni ishara kubwa kwamba taifa letu limegawanyika. Watu wanaumizwa, watu wanatekwa, wanateswa nk...
Watawala wapo kimya wanaendelea na maisha yao, hakuna kiongozi anayekemea dhuluma, chuki, utekaji na kila aina ya uovu..
Wale wanaowaimbia au kusifia watawala ambao wapo kimya wakati mambo ya utekaji, utesaji, mauaji na rushwa yanaendelea wao pia wamekuwa kama maadui kwa wanaoteswa.....
Ndiyo maana leo hao wanaosifia au hata kuwa upande wa watawala wanapopata majanga (msiba, ajali nk) kuna baadhi ya watu (hasa ambao wameumizwa au kuguswa na utekaji, utesaji au mauaji nk) nao hufurahia.
Hali hii ni mbaya sana kwa taifa letu, tunahitaji kuwa pamoja kwa maana sisi sote ni ndugu wa mama Tanzania.
Mpasuko huu hauleti faida yoyote kwa taifa.
Tunahitaji viongozi wenye hekima ya kuwaunganisha watu na si kuwagawa kwa kujenga chuki na kisasi kati yao.