Mrejesho wa panya wasumbufu

Mrejesho wa panya wasumbufu

Mimi sinaga noma na panya niliwahi kuishi sehemu mlango ulikuwa na nafasi kubwa chini sasa kulikuwa na panya wawili ikifika jioni wanatoka nje wanakuja ndani mimi nikaona nisihangaike nao maana wanatafuta ulaji.
Sasa walivyo washenzi nikiwa sebuleni natazama tv mara wakatishe halafu wakifika katikat wanasimama wanaanza niangalia mimi nawaacha tu.
Walicho nifanya walikula vyeti vyangu wakaingia kwenye stabilize wakakata nyaya wakakata nyaza za friji wakaacha kula vyakula wakawa wanakula nguo.
Hapo ndipo niliona ubaya wao nikawatafutia dawa nikiweka kwenye vyakula hawali iwe dagaa au samaki hawali nikaja kuwanasa kwa mtego wa gundi kwa hasira niliwapa mateso balaa walikufa kifo kibaya sana
Mimi hawa washenzi panya kwanza waliniingizia ndani bonge la nyoka, maana nyoka nao wanawafuata panya wawameze, lakini washanitia hasara kwa speaker zangu za Sony, yaani wamefanya nyumba ndani ya speaker badala ya kukaa na kutulia wakakata nyanya na kutafuna speaker ili kupata karatasi za kutandika malalio ya watoto wao.
 
Nunua hii Dawa kwa wauza Dawa za mende inaua hadi Mayai unaiweka kwenye kona mfano mwishoni mwa kabati,
ebb2b185e1382fa3534c0ab621f8532e.jpg
Kuna mende wapuuzi wapo kwenye vikabati vya pembeni ya kitanda changu, cha maana wanachofuata sikioni ila wanakera sana tu yani! Naomba kujua hio dawa inapatikana wapi mkuu?
 
Mimi hawa washenzi panya kwanza waliniingizia ndani bonge la nyoka, maana nyoka nao wanawafuata panya wawameze, lakini washanitia hasara kwa speaker zangu za Sony, yaani wamefanya nyumba ndani ya speaker badala ya kukaa na kutulia wakakata nyanya na kutafuna speaker ili kupata karatasi za kutandika malalio ya watoto wao.
Kuna kenge mmoja mkubwa sana darini ila juzi kati niliskia ki harufu cha ankara nikajua tu lazma alipiga busu umeme! Atakuwa ka danja maana simuoni kabisa, naona kuna katoto panya kameanza misele ila nikitaka kukasulubu nakaonea imani! Hebu nipeni sumu niweke kajimalize kenyewe!
 
Back
Top Bottom