Mrejesho wa panya wasumbufu

Mrejesho wa panya wasumbufu

Mimi sinaga noma na panya niliwahi kuishi sehemu mlango ulikuwa na nafasi kubwa chini sasa kulikuwa na panya wawili ikifika jioni wanatoka nje wanakuja ndani mimi nikaona nisihangaike nao maana wanatafuta ulaji.
Sasa walivyo washenzi nikiwa sebuleni natazama tv mara wakatishe halafu wakifika katikat wanasimama wanaanza niangalia mimi nawaacha tu.
Walicho nifanya walikula vyeti vyangu wakaingia kwenye stabilize wakakata nyaya wakakata nyaza za friji wakaacha kula vyakula wakawa wanakula nguo.
Hapo ndipo niliona ubaya wao nikawatafutia dawa nikiweka kwenye vyakula hawali iwe dagaa au samaki hawali nikaja kuwanasa kwa mtego wa gundi kwa hasira niliwapa mateso balaa walikufa kifo kibaya sana
 
Hizi haziui siku hz..na wala mende hawazifuati
Zinaua mimi nilikuwa na tatizo la mende ndani kwangu mwaka jana nimeinunua na kumwaga ndani kuanzia sebulen chooni mpaka chumbani sasa hivi hakuna mende kabisa mpaka leo inaua kuanzia mende mpaka mayai
 
Natafuta dawa ya mende wasumbufu
Kama haujapata tumia ICON, inapatikana maduka ya pembejeo. Ukifika waambie wakuuzie original maana nyingi zilizopo ni fake. Hii inauwa mende, mbu na wadudu wengine wote na hudumu kwa miezi kadhaa hivyo kusaudia kuwaua hata wale wanaozaliwa baadae.
 
Nimepitia Michango (Maoni) yote ya WADAU
 
Kweli mkuu mijusi hawanaga noma na mtu kwanza wao kukaa juu hawaingii hata kwenye misosi wala masufuria. Mimi sinaga time nao na nikiwa nataka kufunga mlango akawa yukl kwenye bawaba nikiona namtisha kwa atoke ndipo nifunge. Mijusi sina noma nao kabisa hawa ndugu zetu
Subiri siku utakapowakuta wanalamba mswaki wako bafuni ndipo utaona noma kuwahesabu kama ndugu zako.
 
Wakuu hamjambo?
Nachukua fursa hii kuwashukuru wakuu wote waliyonisaidia mawazo ya kuwamaliza panya ndani mwangu.
Luna mkuu moja humu alinishauri niwape sumu ambaye ni dawa ya maumivu inayoitwa Indosin. Kwa kweli nimefanikiwa kupata hiyo dawa na wamekufa wote.
Kwa heshima kubwa nawashukuru wote waliyonipa mawazo yaliyosababisha kufanikiwa.
Asanteni sana
Umeipata wapi kwani haipo kwenye mauzo, dawa hivyo ilikuwa inawafanya panya wafuate mwanga nje na kufia huko.
 
Nunua hii Dawa kwa wauza Dawa za mende inaua hadi Mayai unaiweka kwenye kona mfano mwishoni mwa kabati,
ebb2b185e1382fa3534c0ab621f8532e.jpg
Nzuri sana hii,in kiboko ya mende
 
Mimi natafuta dawa ya mijusi ndani, siwapendi kama nini?
Waache mijusi hao wanasaidia kupunguza wadudu, mijusi wengi maana yake nyumba ina wadudu wengi, ukiwaondoa hao utaangamizwa na wadudu, kunguni mende buibui nk
Afu mijuzi hawana madhara zaidi ya tumavi twao tudogo, lakini ni kama una zoo home kwako
 
Back
Top Bottom