DOKEZO Mradi Maji Arusha-mfano wa Wachina kufanya ovyo, wakati makandarasi wazawa wananyanyapaliwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Oct 20, 2014
15,342
24,233

Mradi wa Maji huko Arusha unaelezea madudu yote yanayofanywa na serikali na wachina wanaowapendelea sana kuwapa tenda.

Isingekuwa mvua kubwa iliyonyesha hivi karibuni, ingekuwa kama waswahili wanavyosema, "imeenda hiyo"

Siyo siri, wachina kwa rushwa ili kupata kazi, hawajambo.

Watendaji serikalini wanajua wakimpa kazi mchina, bahasha nzito zinafuata.

Sasa wengi wamekuwa mateja kwa rushwa.

TAKUKURU wanalijua hilo.

Na mtendaji akisha kuwa teja la rushwa mchina anafanya madudu yote tu kule site, na hachukuliwi hatua yoyote.

Sasa ile mvua ya Arusha imewaumbua.

Mchina kachimba barabara na kuweka mbomba, hakushindiloa kijandisi na kurudishia layer za udongo na kifusi sahihi. Yeye kafunika funika, na akalipwa raha mustarehe.

Consultant yupo, Engineer yupo, na Client mwenyekazi yupo na suti zake ofisini.

Hali hii imelalamikiwa na makandarasi wazalendo kwa miaka mingi, lakini utamu wa rushwa unaziba masikio.

Katika mradi huu wa Maji Arusha, wengi wanaingia kwenye kapu la rushwa na kutosimamia kazi.

Idara ya Maji yenyewe, TARURA na hata idara za Mkoa kusimamia kazi, ni wahusika.

Halafu mbaya zaidi serikali yenyewe ati inashangaa madudu hayo inayoyalea.

Serikali ilitegemea nini haswa na hao wachina.
 
Madhara ya rushwa haya. Nilikuwa mhandisi ninasimamia bara bara fulani hivi DSM (nikiwa serikalini) basi kwa urafiki kabisa nikawa ninamshauri contractor (alikuwa mhindi) jinsi ya kufanya ili kuwa na ufanisi wa kazi. Siku moja akanilitea burungutu la fedha ofisini. Yeye alidhani ninamkwamisha kwa vile ninataka rushwa. Nilimkatalia pesa zake nikamjibu tu ninafanya kazi niliyoajiriwa. Anyway baadaye his contract was terminated maana nilisikia alikwenda huko juu kufanya yake lakini ikashindikana. Nilikuwa ninamsimamia pia mchina akanipa offer ya kunijengea nyumba nikamjibu tu mimi nana pesa nyingi tu na sihitaji pesa zako (ukweli sikuwa na pesa). Rushwa ni nyingi sana kwenye hii miradi ya ujenzi.
 
Lakini mbona wamefukia fresh kuanzia mitaa ya kona nairobi mpaka Arusha raha, wapongezeni bana wanafanya kazi vizuri japo makandokando yapo
 
Mradi kama huu lazima uwe na consultant,(mshauri,mkaguzi na msimamizi wa mradi),lazima Kuna quality control inafanyika na mara nyingi test zinachukuliwa site na kupimwa maabara...kama Kuna rushwa hii chain haiepukiki.
Kuna shida kubwa sana ktk utekelezaji wa hii miradi, ni vile tu Kuna rundo la watumishi wasio na weledi na uzalendo ktk usimamizi.
 
Madhara ya rushwa haya. Nilikuwa mhandisi ninasimamia bara bara fulani hivi DSM (nikiwa serikalini) basi kwa urafiki kabisa nikawa ninamshauri contractor (alikuwa mhindi) jinsi ya kufanya ili kuwa na ufanisi wa kazi. Siku moja akanilitea burungutu la fedha ofisini. Yeye alidhani ninamkwamisha kwa vile ninataka rushwa. Nilimkatalia pesa zake nikamjibu tu ninafanya kazi niliyoajiriwa. Anyway baadaye his contract was terminated maana nilisikia alikwenda huko juu kufanya yake lakini ikashindikana. Nilikuwa ninamsimamia pia mchina akanipa offer ya kunijengea nyumba nikamjibu tu mimi nana pesa nyingi tu na sihitaji pesa zako (ukweli sikuwa na pesa). Rushwa ni nyingi sana kwenye hii miradi ya ujenzi.
Asante mkuu kwa kueleza ukweli na uzalendo.
 
Mradi kama huu lazima uwe na consultant,(mshauri,mkaguzi na msimamizi wa mradi),lazima Kuna quality control inafanyika na mara nyingi test zinachukuliwa site na kupimwa maabara...kama Kuna rushwa hii chain haiepukiki.
Kuna shida kubwa sana ktk utekelezaji wa hii miradi, ni vile tu Kuna rundo la watumishi wasio na weledi na uzalendo ktk usimamizi.
Ukiona kazi mbaya katika ujenzi, ujue kuna rushwa kubwa imetembea. Kama vidagaa vimekula rushwa basi vilevile ujue wakubwa juu wachekua kikubwa kwa rushwa. TAKUKURU wamelala, wanangoja mtu akawagongee hodi ofisini.
 
View attachment 2814149

Mradi wa Maji huko Arusha unaelezea madudu yote yanayofanywa na serikali na wachina wanaowapendelea sana kuwapa tenda.

Isingekuwa mvua kubwa iliyonyesha hivi karibuni, ingekuwa kama waswahili wanavyosema, "imeenda hiyo"

Siyo siri, wachina kwa rushwa ili kupata kazi, hawajambo.

Watendaji serikalini wanajua wakimpa kazi mchina, bahasha nzito zinafuata.

Sasa wengi wamekuwa mateja kwa rushwa.

TAKUKURU wanalijua hilo.

Na mtendaji akisha kuwa teja la rushwa mchina anafanya madudu yote tu kule site, na hachukuliwi hatua yoyote.

Sasa ile mvua ya Arusha imewaumbua.

Mchina kachimba barabara na kuweka mbomba, hakushindiloa kijandisi na kurudishia layer za udongo na kifusi sahihi. Yeye kafunika funika, na akalipwa raha mustarehe.

Consultant yupo, Engineer yupo, na Client mwenyekazi yupo na suti zake ofisini.

Hali hii imelalamikiwa na makandarasi wazalendo kwa miaka mingi, lakini utamu wa rushwa unaziba masikio.

Katika mradi huu wa Maji Arusha, wengi wanaingia kwenye kapu la rushwa na kutosimamia kazi.

Idara ya Maji yenyewe, TARURA na hata idara za Mkoa kusimamia kazi, ni wahusika.

Halafu mbaya zaidi serikali yenyewe ati inashangaa madudu hayo inayoyalea.

Serikali ilitegemea nini haswa na hao wachina.
Katika habari za kuishauri CCM na kuirekebisha CCM hutawaona jamaa kama kina Lucas mwashambwa wakitoa hoja za kimaendeleo.
 
Back
Top Bottom