Dkt. Abbas, unapigwa changa la macho juu ya Makandarasi wa Maji

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Oct 20, 2014
15,313
24,171
20210309_104752[1].jpg


Kama kuna Wizara ngumu kwa makandarasi nchi hii, basi ni Wizara Ya Maji.

Wizara hii haijielewi katika fani ya ujenzi.

Matatizo waliyonayo wizara hii ni tofauti kabisa na wizara nyingine.

Ni ukweli usiopingika kuwa Makandarasi wabobezi na wanaojielewa hawachukui kazi za Wizara ya Maji.

Ukitaka kupigwa Tanganyika Jacki na mwanasiasa basi unachukua kazi za Wizara hii.

Wizara ya Maji kuna uozo mwingi sana katika procurement za miradi yake ya Ujenzi.

Miradi mingi haina design(usanifu) za kina.

Miradi mingi ya Maji haina fedha za miradi na zikiwepo hazifiki kwa walengwa.

Sababu rahisi za kujieleza kwenye uso wa umma ni kuwalaumu makandarasi!

Hatuoni tarumbeta hizo na visingizio kwenye miradi inayotekelezwa kwenye wizara zinazojielewa kama Wizara ya Ujenzi na TANROADS.

Wizara ya Maji imelalamikiwa sana juu ya very poor Project Management katika idara ake zote, ile kumlaumi mkandarasi kwa kiasi fulani kinaeleza kushindwa kwa mwenye mradi(Wizara ya Maji) kwa ujumla.

Mtu usipojua kuendesha baiskeli, na inakuangusha kila mara, njia rahisi kujieleza ni kusema baiskeli ni mbovu.

Lakini kiuhalisia wengine wanaendesha baiskeli hiyo kwa weledi tu, haiwaangushi, tatizo ni kukubali kuwa hujui kuendesha baiskeli!
Ndiyo wizara yetu ya Maji

Sasa tukiona magazetini, hasa gazeti la serikali Daily News, ati Msemaji wa Serikali naye anaingia mkumbo wa kutoelewa kiini cha tatizo, ndo lile lile linaitwa passing the buck!

Dkt. Abbas changa la macho hilo!!
 
Kila kitu ni kigumu kama watendaji wake ni wagumu kufanya uchambuzi, kutengeneza bajeti stahiki, kuweka mpango kazi na usimamizi makini

Hata 2015 kurudi nyuma ilikua ngumu sana kupata kitanda pale Mwaisela, mgonjwa kulazwa chini ilikua kawaida sana ila sasa vitanda vipo tena vitanda safi
 
Safi kabisa , mtawatapata wale makandarasi wajuaji wasiokataa kazi na wanaoweza kupandisha maji mlima Kilimanjaro!
Kwani na wewe ni mmojawapo wa wakandarasi mkuu, mbona unatetea huo Ujinga!!

Tukiondokana na ujingaujinga wa wakandarasi matapeli na tusioneane aibu, Nchi yetu tutakuwa tumeanza kuzichungulia dhahabu mahali zilipo
 
Kwani na wewe ni mmojawapo wa wakandarasi mkuu, mbona unatetea huo Ujinga!!

Tukiondokana na ujingaujinga wa wakandarasi matapeli na tusioneane aibu, Nchi yetu tutakuwa tumeanza kuzichungulia dhahabu mahali zilipo
Wajinga wakubwa zaidi ni ninyi msioelewa.

Wajinga zaidi ni wale wanaotoa kazi bila vigezo vya kazi kukamilika, hawasimamii kazi, hawalipi makandarasi na bado wakabwabwaja kuwalaumu makandarasi.

Na wajinga zaidi ni nyie mnakenua meno kwa kutoelewa!
 
kwani wizara ya ujenzi ina mradi gani tofauti na chattle airport?
Hata iwe kwenu, huu wakati si wa kucheka na nyani

Mkandarasi mmoja anapoaminiwa kwenye jamii ya watu zaidi m60 ni Jambo kubwa na heshima kubwa Sana kwake!

Anapofanya vibaya, jamii yote anaikosea, asivumiliwe mtu huyo
 
Hata iwe kwenu, huu wakati si wa kucheka na nyani

Mkandarasi mmoja anapoaminiwa kwenye jamii ya watu zaidi m60 ni Jambo kubwa na heshima kubwa Sana kwake!

Anapofanya vibaya, jamii yote anaikosea, asivumiliwe mtu huyo
Mkuu wewe ujijue kuwa una pumba kichwani, mambo ya kitaalam waachie wenyewe.
 
Hata iwe kwenu, huu wakati si wa kucheka na nyani

Mkandarasi mmoja anapoaminiwa kwenye jamii ya watu zaidi m60 ni Jambo kubwa na heshima kubwa Sana kwake!

Anapofanya vibaya, jamii yote anaikosea, asivumiliwe mtu huyo
hujajibu swali langu
Kazi za Wizara ya Ujenzi zinakamilika bila maroroso kwa vile zinasimamiwa kitaalam.
Chato imekamilika, kwani hukuona Rais wa Ethiopia akitua?
 
Wajinga wakubwa zaidi ni ninyi msioelewa.
Wajinga zaidi ni wale wanaotoa kazi bila vigezo vya kazi kukamilika, hawasimamii kazi, hawalipi makandarasi na bado wakabwabwaja kuwalaumu makandarasi
Na wajinga zaidi ni nyie mnakenua meno kwa kutoelewa!
Tunspotaka kuwaamini Watanzania halipo kabisa kosa hata kidogo, kosa ni pale mtanzania aliyeaminiwa anapokosa uaminifu!!

Punguani wewe elewa Sana Hii kitu
 
Tunspotaka kuwaamini Watanzania halipo kabisa kosa hata kidogo, kosa ni pale mtanzania aliyeaminiwa anapokosa uaminifu!!

Punguani wewe elewa Sana Hii kitu
Nimesema kujenga siyo jambo la imani, elewa hilo.
Ni jambo la teknolojia.
Sasa ninyi mliojazwa pumba kichwani, kwanza hamuelewi tatizo , na pili mnakuwa rahisi kulaumu bila kulielewa tatizo.
Wizara ya Ujenzi iko vizuri, sasa kama una akili za kukutosha tueleze kwa nini Wizara ya Maji miradi yake inasuasua ,
Au wakandarasi wa Maji wanazaliwa tofauti?
 
Hata iwe kwenu, huu wakati si wa kucheka na nyani

Mkandarasi mmoja anapoaminiwa kwenye jamii ya watu zaidi m60 ni Jambo kubwa na heshima kubwa Sana kwake!

Anapofanya vibaya, jamii yote anaikosea, asivumiliwe mtu huyo
Aisee! Mtu kutojua kitu ni kama kuongea bila kupigwa mswaki.

Kero kwa walio karibu.
 
Nimesema kujenga siyo jambo la imani, elewa hilo.
Ni jambo la teknolojia.
Sasa ninyi mliojazwa pumba kichwani, kwanza hamuelewi tatizo , na pili mnakuwa rahisi kulaumu bila kulielewa tatizo.
Wizara ya Ujenzi iko vizuri, sasa kama una akili za kukutosha tueleze kwa nini Wizara ya Maji miradi yake inasuasua ,
Au wakandarasi wa Maji wanazaliwa tofauti?
Ujenzi haiwezi kulalamikiwa sababu mzee ndiyo anakopigia
 
Back
Top Bottom