Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

kesho (jumapili) kama kuna mtu anataka kupiga simu na kuunguruma kuhusu suala hili (pande zote zinakaribishwa) nitawapatia namba ya studio...!
 
Ndugu Kulikoni,

Si sahihi kusema kwamba Bunge likitaka kujadili na kuhahiki mikataba kati ya serikali na wawekezaji litakuwa limeingilia madaraka ya Executive Branch. Shughuli za Bunge, ambalo ni sehemu ya serikali, zinatawaliwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. Kama alivyonukuu Mzee Mwanakijiji, kipengele hiki kifuatacho kinahusika:

Ibara 63(2) Katiba inasema hivi:
Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka, kwa niaba ya wananchi, kuisimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii
Katiba yetu inataja wazi wazi vile vile kwamba sehemu ya majukumu ya Bunge ni:
kujadili na kuridhia mikataba yote inayohusu Jamhuri ya Muungano na ambayo kwa masharti yake inahitaji kuridhiwa."
Hicho kisehemu cha "kwa masharti yake" naamini maana yake ni kwa "masharti ya Bunge". Sasa kama Bunge linataka kujadili na kuridhia mikataba kati ya serikali yetu na wawekezaji, kwa nini Waziri Kayombo athubutu kulikatalia? His argument for doing so is mischevious and poorly thought out. It calls into question his ability to be a minister.

Wabunge wanataka kujadili na kuhakiki mikataba kati ya serikali na wawekezaji. Sio mingi hiyo mikataba. Hawajasema wanataka kujadili vimikataba vidogo vidogo vya kila siku.

Ni nini kinaifanya serikali ipende kukataa UWAZI kwenye mikataba? Kuna nini cha kuficha? Hiding under separation of powers will not do.

Augustine Moshi
 
Kulikoni,

Your arguments are usually quite good but this weekend you are not your normal self. The Minister's answer that we will cross that bridge when we get to it is a very bad one. Governments have to have answers to various possible scenarios. For example, the PM should have an answer now to the following hypothetical question: What will we do if it does not rain for the next two years? We should not wait until we get two years without rain before we figure out how to handle an extended drought.

Kulikoni, do not defend Kayombo at any cost. He is making bad mistakes. Let him wallow in the mud by himself; you need not join him there.

Augustine Moshi
 
Kitu kimoja ambacho nafikiri serikali inajaribu kufanya kwa kukataa kuleta mikataba hii kwa wawakilishi wa watu ni kuacha taswira ya kuingiliwa madaraka. Wanataka watu waamini kuwa Wabunge wanataka kuingilia majadiliano na makubaliano ya mikataba. Ukweli ni kuwa wabunge hawataki kushirikia majadiliano au kuandika mikataba kwa niaba ya serikali.

Kama wabunge wanataka kuandika mikataba, kushiriki kwa majadiliano na kutia sahihi mikataba hilo ni kosa na ni kweli. Hata hivyo wabunge hawataki hilo. Wanachotaka wabunge ni kwamba endapo serikali inaingia mkataba ambao una maslahi kwa nchi (ya kiusalama au vinginevyo) basi mikataba hiyo kabla ya kutiwa sahihi au hata baada ya kutiwa sahihi inapaswa kuangaliwa na Kamati husika ya Bunge.
 
Kulikoni,

Your arguments are usually quite good but this weekend you are not your normal self. The Minister's answer that we will cross that bridge when we get to it is a very bad one. Governments have to have answers to various possible scenarios. For example, the PM should have an answer now to the following hypothetical question: What will we do if it does not rain for the next two years? We should not wait until we get two years without rain before we figure out how to handle an extended drought.

Kulikoni, do not defend Kayombo at any cost. He is making bad mistakes. Let him wallow in the mud by himself; you need not join him there.

Augustine Moshi

Prof., obviously the "concept" of contingency plans is foreign to our leaders and that is why you get those type of answers. Oh well.....
 
Kwanza tuache kuzungumza juu ya Bunge kuingilia serikali. Bunge ni sehemu ya serikali. Checks and balances zinazotakiwa kwenye demokrasia ni pamoja na Legislative Arm of Government kuhakiki kwamba Executive Arm of Government haiuzi nchi.

Executive Arm imeuza dhahabu yetu kwa 3% ya thamani yake. Imetuwekea mkataba wa kuilipa IPTL bilioni 3 kila mwezi. Imeuza nchi kwa mikataba mingine ya kiuwekezaji kwa udanganyifu. Sasa Waziri Kayombo anataka waendelee kuuza nchi hivyo hivyo, na Bunge lisithubutu kudai kuhakiki hiyo mkataba!

Mkono mmoja wa serikali unauza nchi na unafoka mkono mwingine unapoulizia kulikoni!

Agustine Moshi
 
Nakusikia Nyani... ndio maana tunafanya mpango wa kuweza kusikika kwenye radio za ardhini huko kijijini..!

Itabidi ujipange kweli kweli kwani redio ambazo watu wanasikiliza huku Bongo ni zile zinazopiga muziki tu...kwa muda mrefu. Wabongo hatuna muda wa kusikiliza "siasa" na mambo mengine ya maana. Ndio maana hata magazeti ya udaku ndiyo wengi tunayachangamkia. Longolongo na ahadi za nchi ya maziwa na asali hatuzikubali tena!!
 
kazi ya kujenga jamii ni kazi kubwa sana, waswahili wanasema kujenga na kugumu kuliko kubomoa.

haya tunajifunza kwa watu mbali mbali na dini mbali mbali.

kwa wakristo wanaona kwa mussa, issa(yesu), na wengineo jinsi walivyokumbana na vishindo ktk kuelimisha jamii zao na kuziweka ktk mstari.

hata ss waislamu mtume wetu alikumbana na matatizo vipangamizi mbali mbali ktk kuelimisha na kuistaarabisha jamii yake.

mkjj na wale sote twenye nia ya kweli na ya dhati ya kulitumikia taifa letu tusikate tamaa, na njia bora kabisa ni kuwaelimisha watu wetu kujua nini wajibu wao na nini haki yao.

wala tusikate tamaa, maana mapambo haya yana mengi wako watakaokutokonyoa ili ushindwe kuendelea na baadhi ya wakati waweza kupoteza maisha.

kwa hiyo mkjj na wengine tutumie kila methods ikiwa magazeti, internets vijarida, radio au tv kufikisha ujumbe kwa jamii.

walioleta maendeleo ktk kila fani walijitolea muhanga maisha yao.

wengi wa watu wanaonufaika si waliotaabika ktk kila fani.

nnaomba kuwakilisha

MUNGU ILINDE TANZANIA, MUNGU WAPE BUSARA NA HEKIMA WATANZANIA WAPE UPENDO WA KUKUPENDA WEWE NA KUIPENDA NCHI YAO.

WAPI NGUVU NA MAARIFA YA KUULINDA MUUNGANO WAO NA KUUIIMARISHA ZAIDI BILA YA DHULMA WALA MANYANYASO BAINA YA WAZANZIBARI NA NDUGU ZETU WATANGANYIKA

MUNGU MJAALIE HEKIMA BUSARA NA UWEZO RAIS WA JAMHURI YETU.
PIA MPE BUSARA HEKIMA UPENDO NA AKILI YENYE KUONA MBALI RAIS WETU WA ZANZIBAR.

PIA WAPE BUSARA NA HEKIMA VIONGOZI WETU WA VYAMA VYA UPINZANI, WAWEZE KUIKOSOA NA KUIELEKEZA VYEMA SERIKALI YETU TUKUFU KWA MASLAHI YA WATANZANIA WOTE.

MWISHO MUNGU WAPE MAARIFA NA UJUZI ZAIDI WANA BODI WA JF NA WAPE MAARIFA NA BUSARA NJEMA WACHANGIAJI WA JAMBO FORUMS MICHANGO YAO IMEE KTK KULETA MAFANIKIO YA TAIFA LETU.

MUNGU UDUMISHE MUUNGANO
 
Mzee Mwanakijiji,

Umewafafanulia vizuri sana wabunge namna walivyopashwa kumjibu Gaudence Kayombo. Kayombo alidanganya (labda bila kujua) aliposema separation of powers hairuhusu wabunge kuridhia mikataba ya kiserikali kabla haijawa sheria. Ni wazi kabisa toka kwenye ibara za katiba ulizotaja (IBARA 63(2) (E)) kwamba Wabunge wana haki na uwezo wa kuhakiki mikataba kati ya Jamhuri ya Muungano na mtu yeyote.

Inabidi wabunge wawe wanaifahamu vizuri Katiba. Wanaapaje kuilinda kama hata hawaifahamu? Kama wangekuwa wanaifahamu, wangejibu huo uongo wa Gaudence Kayombo hapo hapo, kwa njia ya swali la ziada.

Gaudence Kayombo amejichanganya aliposema wabunge wana uwezo wa kusimamia serikali inavyotekeleza mikataba, na huku anasema hawana uwezo wa kudai kuiona mikataba yenyewe. Kuna level mbili za kuona mkataba. Kuna kuuona kabla haujasainiwa na kuwa wa kisheria, na kuna kuuona wakati umeshasainiwa. Inaelekea kwa sasa wabunge wananyimwa kuona mikataba hata baada ya kusainiwa. Watasimamiaje utekelezaji wake?

Wabunge watumie Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kulazimisha serikali isisaini mkataba wowote bila ridhaa ya Bunge.

Wanaong'ang'ania mikataba iwe siri na isiridhiwe na wabunge wana lao!

Augustine Moshi

AM,

Nafikiri kwa majibu yako, inabidi tujiulize, inakuwaje tuwe na Wabunge ambao licha ya kuwa ni Wawakilishi wa Wananchi, kazi yao kubwa ni kuilinda Katiba na Kutunga Sheria lakini wengi wao hawaijui Katiba yetu vizuri wala kujua Sheria?

Nafikiri wakati umewadia kuanza kuwamulika Wabunge wetu na si Serikali Kuu pekee.

Haiwezekani kuwa katika Bunge letu la Muungano lenye watu zaidi ya 300, hapakuwa na suali la nyongeza au hoja kumbana Koyombo kuhusu madai yake kuwa Bunge halina madaraka na uwezo kupitia mikataba. Ina maana Wabunge wote ni "watupu" kuhusiana na Katiba au ni ile silika ya kukubali kila kitu mradi Mkate waenda kinywani?
 
Mzee Mwanakijiji:

Ingekuwa wachangiaji wetu wote hapa wanachangia objectively kama wewe, wakubwa wetu wengi wangekuwa wanakuja hapa na kujifunza maoni hasa ya wananchi, they're not necessarily correct lakini at least ni views zinazoweza kusikilizwa na wasomi, this is good and I encourage you and others to embrace this line of argument....wakubwa wengi for information tu wapo aware na JF ila honestly sina tena nguvu ya kuwahimiza wapite hapa kwani siku hizi 'upupu' ni mwingi wengi wao wakiingia siku mbili tatu wanalose interest kwa vile hamna hoja.... hivyo ni wito kuwa kama mnataka sauti zenu zisikike basi toeni kwa hoja na uchambuzi yakinifu sio kubwabwaja tu nk...


On the issue:

Separation of powers ni pana zaidi ya alivyoeleza sahihi kabisa mheshimiwa Kayombo, yaani yes ni kweli kama alivyosema mwanakijiji kuwa ipo haki kwa wabunge kujadili mikataba ya serikali ambayo jina la serikali limehusika, sasa wabunge wana haki ya kujadili na kuelezea mapungufu [if any] ya mikataba nk lakini sio kama anavyosema Mzee Moshi kuwa ''kuhakiki'' hii ni kazi ya watendaji wa serikali...

Bunge lilikuwa na haki ya kujadili mkataba wa Richmond in the context of:

- Validity [ ni sababu zipi zilizopelekea mikataba husika ikaingiwa]
-Execution [ umetekelezwa kivipi]
- Deficiencies [kasoro zozote zilizojitokeza nk]

Kama mbunge ana hoja ya msingi katika hayo anaweza kuuliza in terms of swali binafsi na ikiwa wabunge woooote wataridhika basi wanaweza kwa pamoja kutoa kauli iundwe tume huru ya kuchunguza 'kadhia' [ mind the language] ili ukweli ujulikane.... tume ikitoa kauli yake basi hapo inakuwa ndio the beginning of the end for the matter yaani aidha wanaohusika kama wamezembea wataondolewa au kuwa exonerated...

Lakini Bunge kama haliwezi ku-overlap majukumu ya serikali [executive] kwa kuuandika mkataba, kutathmini utekelezaji wake wa day to day nk sasa hoja kuwa mikataba ipitiwe ''kabla'' ni hoja mfu kwa vile there is no legal mandate for the parliament to do that....

Imagine everyday serikali inaingia mikataba mingi sana ya kiutendaji, inatoa tenders, kandarasi na inapokea misaada mingi tu ya kifedha ambayo inainvolve some form of mikataba, kwa hiyo kama mikataba yote hii inabidi ipitiwe na bunge...it will be detrimental to gov't activities....

Ni pale tu ambapo kama bunge lina wasi wasi wa Rushwa ndio linaweza kuipitia au kuhoji uhalali wake.... kama richmond mnahisi ina walakini mwambieni Zitto....

Kulikoni,

Naomba nichukue fursa hii kuonyesha ni jinsi gani Bunge laweza kuwa na Mamlaka ya kuhakiki au kuzuia kuingia kwa mkataba.

1. Wakati serikali ya Marekani ilipoamua kuwapa kampuni ya Dubai kusimamia Bandari zake, Bunge la Marekani lilisitisha uuzaji wa usimamizi wa Bandari uliopitishwa na Ikulu ya Marekani.

2.Bunge la Marekani lilisitisha 2uuzaji wa kampuni kubwa ya Mafuta ya Kimarekani kwa Kampuni ya Kichina ilhali Ikulu ilishaidhinisha uuzaji huo!

3. Bunge la Uingereza lina nguvu Kikatiba na Kisheria kusitisha mkataba wowote ule uwe wa Kibiashara au namna yeyote ambao hauzingatii maslahi na usalama wa Taifa.

Pamoja na kua nimetoa mifano mitatu ya Nchi ambazo si Tanzania, utaona kuwa Mabunge haya yalitumia madaraka yao kuhosi na kusitisha mkataba kabla ya kupitishwa. Na hata ile mingine iliyokwisha pitishwa, bado Mabunge haya yamekuwa na uwezo wa kuzihoji Serikali zao na hata kufuta Mikataba mibovu.

Hii ndio demokrasia ya kuwa na Nguzo kuu tatu za Serikali ambazo zina uwezo wa kuhakiki na kuchangua (kuwajibisha) upande mmoja wa Serikali usio fanya kazi kimakini.

Sasa sisi Watanzania badala ya kufanya hivyo, tunatumia vitisho na vijikao vya Kichama kuhakikisha kuwa Maslahi binafsi na si ya Taifa yanapitushwa!
 
Je tumesahau kuwa Bunge lina nguvu ya kumvua Raisi madaraka na Serikali yake? Je huko ni kuingilia kazi za Serikali?
 
Rev Kishoka,

Asante kwa mifano yako mizuri ya ufanyaji kazi wa mabunge ya wenzetu wa Uingereza na Marekani.

Kibaya zaidi ni hivi: Imegundulika, baada ya ugomvi kati ya IPTL na serikali ya BWM, kwamba kunakuweko na kipengele kwenye hii mikataba kinachosema hivi: (not direct quotation, as I ahve not seen the damn thing):
Mahakama za Tanzania hazitakuwa na uwezo wa kujadili huu mkataba. Kama kutakuweko na kutoelewana, usuluhishi ni London.
Yaani Executive Arm ya Serikali inasaini mkataba ambao unasema Judicial Arm ya Serikali haina nguvu kutoa hukumu juu yake! Kama hiyo haitoshi, sasa Executive Arm inaongezea kwamba Legislative Arm nayo haina haki hata kuona hiyo mikataba.

Jamani! Utulivu wa Watanzania unachukuliwa kama ni ujinga? Tumedharauliwa vya kutosha. Hawa akina Kayombo wajiulize wanasema nini kabla ya kufungua mdomo.

Augustine Moshi
 
sasa tofauti iko wapi baina ya mikataba iliosainiwa na bw. Kerl Peter na mfalme mSoveru tuliosoma kwenye historia? kumbe bado tuko enzi zile zile!!!!!!!!!!!!
 
Naona kuna haja ya kufundisha elimu ya uraia maana kama wabunge hawajui kuwa wao ni sehemu ya serikali basi tuna matatizo!!
 
sasa tofauti iko wapi baina ya mikataba iliosainiwa na bw. Kerl Peter na mfalme mSoveru tuliosoma kwenye historia? kumbe bado tuko enzi zile zile!!!!!!!!!!!!


Mzee Mtumwitu, Heshima yako mkuu

Inawezekana tofauti ipo. Mfano, mazingira yaliyokuwepo wakati wa mikataba ya wakati ule, yaani baina ya machifu wetu wa makabila na wageni mithili ya akina Karl Peter, yalikuwa tofauti ukilinganisha na mazingira ya mikataba ya miongo ya karibuni inayohusu watawala wa nchi yetu na wageni mithili ya Sinclair.

Mazingira ya mikataba ya zamani yalikuwa na utata kwa maana kuwa, wale walioridhia ile mikataba hawakujua kusoma wala kuandika. Pia, lugha ya mawasiliano ilikuwa ni tatizo, hivyo, matumizi ya alama na ishara yalighubika maafikiano baina ya pande mbili. Tatizo lilijitokeza wakati wa utekelezaji wa yale makubaliano. Matendo ya wageni yalitofautiana na jinsi machifu walivyokuwa wameelewa yale makubaliano. Walipouliza kulikoni? Walionyeshwa makaratasi ya makubaliano yaliyokuwa na madole gumba ya wale machifu. Ndipo machifu walipoanza kung’aka kwamba, sivyo walivyoelewa wakati wanatia dole gumba.

Historia inatufundisha kuwa, kizazi kilichofuatia baada ya wale machifu, kilipata bahati ya kuifanyia utafiti mikataba ya zamani na kutambua kuwa ilikuwa ni ya ulaghai. Mzee Mtumwitu, naona the history lessons we recently learned at school is not a distant subject. Remember, Chief Abushiri sold his homeland by signing on a piece of paper whose contents he knew not. We were taught he did not have education. Lest these new species of "Nshomiles” who sold everything to South African Companies with their Phd’s. Yet, I wonder what is left of our country that is genuinely ours.

Umesahau Loliondo where an area about 4666 Km square in Arusha region was reported sold or leased for hunting rights to a foreigner at a fee? Nadhani unamkumbuka fukara mmoja kwa jina la Chavda, ambaye aliwafungulia milango "wawekezaji". Waheshimiwa viongozi wetu waliilazimisha marehemu benki yetu ya NBC imkopeshe Chavda mamilioni ya fedha kwa ajili ya kununua na kufufua mashamba ya Mkonge Tanga. Kipofu aliona mwezi, kwani Chavda ambaye wakati anatia saihi mkataba hakuwa hata na senti moja, aliukwaa utajiri wa haraka kama ule wa mshindi bahati nasibu, alafu akaingia mitini na fedha zetu. Kana kwamba haitoshi, haohao waheshimiwa viongozi wetu, wakaitafutia mkataba NBC na kuibinafsisha kwa kisingizio kuwa ina madeni mengi.

Mikataba ya zamani ilisheheni maajabu ya Mussa. Mikataba ya sasa hivi inajivinjari kwa mbwembwe za filauni. Tunaambiwa vipengele "fulani” ndani ya mikataba mfano ya Rada, IPTL, Richmond, ATC, madini, n.k, ndivyo vinavyoliangamiza taifa letu kwa kupitia njia ya mkato. Wanaoweka mikataba kwenye darubini, kwa maana ya kuisoma na kuhakikisha kuwa haina vipengele vya kututia matatani ni “wasomi”. Kumbuka, ilisisitizwa mashuleni kuwa tunasoma kuhepuka makosa waliyoyafanya akina Abushiri na wenzake. Sasa huu ufilauni unatoka wapi?

Binafsi, naamini yalikuwepo matatizo mawili enzi za machifu yaliyopelekea mikataba ya ulaghai. Moja ni tatizo la shule, ambalo tumejitahidi kulishughulikia. Pili ni tatizo la watu kutokuwa na nguvu, ambalo tulilifumbia macho. Machifu walikuwa na nguvu kuzidi watu waliowaongoza. Jamii haikuwa na nguvu za kusitisha au kurekebisha maamuzi ya machifu. Machifu walikuwa ndio chimbuko la utawala na kila kitu na kila kitu kilichohusu jamii. Walizaliwa kutawala, hivyo, maamuzi yao yalikuwa ya mwisho na wakati mwingi, hayakushirikisha mashauriano ya watu. Kwa kifupi, walikuwa ni miungu watu.

Hivi ndivyo ilivyo sasa hivi. Ingawa watu wamesoma, lakini Raisi wetu wa nchi anazo nguvu kama walizokuwa nazo machifu. Nchi inaongozwa kwa ridhaa yake. Ingawa hakuzaliwa kuongoza, lakini ni kama Mungu mtu. Uamuzi wake katika masuala ya msingi ya nchi ni wa mwisho. Katiba yetu imempa uwezo wa kupinga utashi wa watu anaopashwa kuwatumikia (kitu ambacho ni hatari sana). Katiba yetu imewafanya wabunge (ambao wanapashwa kuwa wawakirishi na watumishi wa wananchi) wasiwe na nguvu za kisheria za kuwatumikia au kuwawakilisha wananchi, badala yake wawe vikaragosi na watumishi wa Raisi.

Sioni sababu ya kungoja vizazi vya mbeleni kuifungua mikataba ya sasa hivi ili kujua hasa nini tatizo la hawa waheshimiwa viongozi wetu. Hii kazi tunaweza kuifanya sisi. Njia ya kwanza kufikia azma au lengo hili ni kuhakikishe kuwa katiba yetu inatambua kwa dhati kuwa watu ndio chimbuko la mamlaka yoyote na si vinginevyo. Iseme hivyo, na imaanishe hivyo. Hatuwezi kuendelea kulipia gharama za kuweka mustakbari wa maisha ya mamilioni ya watu chini ya fadhila za mtu mmoja ambaye ni Raisi wa nchi. Lazima mizengwe iondolewe ndani ya katiba yetu ili wabunge wafanye kazi kwa maslahi ya waajili wao, ambao ni watu wala si vyama vya siasa au Raisi wa nchi. Nasikitika kusema kuwa, sasa hivi wabunge hawana uwezo huo.

Bajameni, we have to empower the people.
 
Kyoma, maneno mazito hayo! Sasa kama wasomi wetu ndio wanatuingiza kwenye matatizo haya, tutafanya nini ili wajue kuwa tumechoka? Ni jinsi tunaweza kuwawezesha wananchi wenzetu kujua wajibu wao na nafasi yao katika kuhakikisha viongozi wanafanya kile wananchi wanataka?
 
Naona kuna haja ya kufundisha elimu ya uraia maana kama wabunge hawajui kuwa wao ni sehemu ya serikali basi tuna matatizo!!

Sio wabunge tu jamani hata mimi sielewi jambo hili

maana nilidhani utawala wa nchi umegawanyika mara tatu yaani
1 serikali
2 bunge
3 mahakama.

na kwamba bunge si sehemu ya serikali bali wao wanapashwa kusimamia utendaji wa serikali kwa niaba ya wananchi.

lakini utata huu kwangu unaanzia mbali katika elimi ya uraia hiyohiyo tulikofundishwa serikali ni wananchi. Mimi hapa hii maana kwa kweli sijawahi kuikubali na ndio maana pengine sikufanikiwa kufaulu vizuri somo hili maana Siku zote mimi naamini serikali ni uongozi wa wananchi.

mfano kitu wakisema ni kwa matumizi ya serikali ni tofauti na kusema hiki ni kwa matumizi ya wananchi, au tukisema serikali ya Tanzania tunamaanisha wananchi wa tanzania au uongozi wa wananchi wa tanzania. Au tunaposema chama cha siasa kikishinda kinaunda serikali je tunamaanisha kuwa kinaunda wananchi au kinaunda uongozi wa wananchi? nisaidieni kutafakari hili.

Ila naamini aliyesema serikali ni wananchi mwanzoni alikuwa na maana nzuri akimaanisha kuwa serikali lazima iungwe mkono na wananchi ili idumu madaraki.

Lakini yote juu ya yote nadhani bunge kudai mikataba kuwa wazi ni jambo zuri ila kudai ipelekwe bungeni bado ni yale yale. Hoja ya wabunje ni ule mchezo wa nyani wakiwa kwenye msafara kila nyani anaona wenzake kuwa wako uchi yeye hajioni.

kama Serikali ilivyo na mapungufu katika utendaji wake kama kuingia mikataba mibovu hata bunge katika yale ambayo wanawajibika nayo wanamapungufu. Ni miswada mingapi wameipitisha yeye kasoro kibao?

Sikiliza Bunge kwakweli utabaki mdomo wazi, wabunge ni wazuri wa kujadili (politics) ila hawana ujasiri wa kupinga hoja mpaka kasoro muhimu zirekebishwe katika muswada ndio upitishwe. Ni mambo mangapi wameongea lakini wanapoulizwa wanaokubali waseme ndio hao hao wanakuwa wa kwanza kusema ndio.

Mimi ningependekeza
Kanza
kabla ya mkataba kusainiwa uwe wazi kitaifa mashirika yasiyo ya kiserikali na yale ya kiserikali na watu binafsi wenye nia njema na watanzania wa/yapitie na wa/yatoe maoni kabla mkataba husika kusainiwa. Pengine kupitia website ya Taifa au chombo husika.

Sasa wabunge wajadili fndings za wataalamu hawa na zao binafsi kama wahusika wameyaapuuzia wakati ni ya msingi.

Pili
PCB waruhusiwe kufuatilia taratibu hizi kabla na baada ya mkataba kusainiwa ili kutafuta wateja wa sheria ya kuhujumu uchumi. Wawe wamehongwa au hawajahongwa wanababaisha tu hoja ya msingi iwe ni kuhatarisha chumi wa taifa kwa mkataba aliosaini au anaotaka kusaini na kama kapokea chochote liwe kosa la pili.

Hitimisho HATUHITAJI POLITICS KWENYE MAMBO KAMA HAYA BALI TUNAHITAJI ACTIONS ambazo zimetokana na proffesional view.
 
Back
Top Bottom