Moshi yakataliwa kuwa jiji

Moshi yakataliwa kuwa jiji

Moshi bado kamji kadogo sana, hata Tanga sijui kwanini ilipewa hiyo hadhi ya kuwa jiji, Mbeya...... naona kuna haja ya kuyatazama upya majiji yetu kama kweli yana vigezo.
Sio Tanga hata Mbeya ni uchafu mtupu.
 
Wewe upo ndani ya serikali??
Zipo faida za kutosha wewe ukiwa nje ya serikali hujui ila mojawapo ni kupewa kipaombele kwenye huduma na kupewa bajeti kubwa kuliko wengine,hivyo hivyo hadi Halmashauri,Mji,Manispaa na Jiji.
 
Ni mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan aka (Chifu Hangaya).--- alipewa uchifu na akabatizwa jina hilo, wewe unaishi wapi ??!!Tz au??[emoji1787]
Nakazia mkuu kuna watu kama hawapo tz tena nimesema mh hangaya
 
Na chato wafanye nini ili wawe mkoa?
Chato Serikali iko inakamilisha vigezo vya kuufanya mkoa, leo kama sikosei Ngara na Biharamuro wameridhia kuhama kutoka Kagera kwenda Chato.
 
Moshi bado kamji kadogo sana, hata Tanga sijui kwanini ilipewa hiyo hadhi ya kuwa jiji, Mbeya...... naona kuna haja ya kuyatazama upya majiji yetu kama kweli yana vigezo.
M ona husemi wilaya ya Chato inaidadi wa watu 365,127 Ina km za mraba 3,572 ,mnaipigania usiku na mchana kuwa mkoa, huku mkiiacha kuzigawanya Morogoro na Tabora zenye km za mraba zaidi ya 168,000 ?
 
Kamji unakazunguka na kukamaliza kwa miguu tu halafu kawe jiji!! Hebu wawe serious kidogo.
 
Watu Hupanda Boat kwenda Zanzibar na Kuacha Bahari nzuri Bagamoyo pale....Tena nzuri kweli.
 
Mji wenyew mdogo tu ...

Mji haupanuki na bado unazeeka tu..

Unazidiwa na kahama kwa mzunguko wa pesa
Kahama hapana. Kahama haina mpangilioni, hakuna barabara, kila mahali ni viuchochiloro. Kahama ni kati ya miji yenye mpangilio wa ovyo kabisa. Mzunguko wa pesa upo ila ni kama vimiji vinavyozaliwa kutokana na machimbo ya wachimbaji wadogo.
 
Back
Top Bottom