Tetesi: Mojtaba Ali Khamenei kumrithi Ayatollah Ali Khamenei baada ya kuuawa baba

Tetesi: Mojtaba Ali Khamenei kumrithi Ayatollah Ali Khamenei baada ya kuuawa baba

Hii naona ni vita ya kuuwa viongozi tu wa Iran basi na wenyewe wanaweka viongozi wapya mambo yanaendelea yaleyale.
 
View attachment 3550408
Baraza la Mapinduzi la Iran limemtangaza Mojtaba Khamenei (Mtoto wa Ali Khamenei- RIP) kuwa kiongozi mkuu wa Iran.

Ali Khamenei alimlea akimlea na kumwandaa kwa miongo kadhaa mwanawe mwenye roho mbaya, Mojtaba, ili awe kiongozi mkuu ajaye.
Yeye ni mbaya zaidi kuliko baba yake.
Dah,
Huyu hata kabla hajaanza kazi atakuwa tayari anatembea na kitita cha bounty kichwani kwake.

Anaweza kuwa kama yule mrithi wa Nasrallah wa Hezbollah aliyedumu siku moja
 
Duh aisee
 

Attachments

  • Screenshot_20260301-170258_Lite.jpg
    Screenshot_20260301-170258_Lite.jpg
    124.1 KB · Views: 19
  • 1772373704622.jpg
    1772373704622.jpg
    202.9 KB · Views: 17
Duh hizi nchi Iran na Cuba zime suffer sana , karibu 60 years US kazipiga total embargoes and sanctions lakini wameshikilia misimamo yao, makosa yao makubwa ni Iran kutaka kuwafuta Israel na nuclear weapon, Cuba hawataki kuacha ukomunist, na zote zina potential za kuwa first world countries kwa raslimali zao, naona wangeachana tuu na hayo maisha maana sioni US ikianguka leo au kesho na hatawaacha
 
Una majonzi unamuwaza baba unaambiwa tuongoze vitani
 
Yaani huyu vita ikiendela zaidi wanakula kichwa mapema sana

Tatizo kubwa ninalo liona ndani ya Iran na nchi nyingi za Kiarabu/Islam ni kuwa Mossad wamepandikiza moles kila kona.

Hata akiongoza akiwa chini ya mashimo kama panya watamfikia tu labda akubali matakwa ya Israel/USA
Wewe huna tofauti na huyo unaesema mkeo.

Yaani ukubaki kupangiwa Cha kufanya na mtu baki? Hiyo Inawezekana Kwa wanawake kama wewe ila Kwa wanaume never maana wanajua Kuna kuzaliwa na kufa.

Mwisho hata uue kiasi gani Bado utakufa so njia ni Ile Ile ila kulinda Heshima ya kiume Iko pale pale na italindwa Kwa gharama yeyote
 
NAKUMBUKA HAMAS AKIFA MTU ANAWELWA MTU WABAPITA NA MTU

HUYU MTEULE NAMWONEA HURUMA SANA SANA SIDHAN KAMA ANA MSA NA HASIRA ZA USA. A ISRAEL
 
Siyo tetesi tena, tayari kisha sainivhati ya kufo chake.
Screenshot_20260309_070758_X.jpg
 
Siyo tetesi tena, tayari kisha sainivhati ya kufo chake.
View attachment 3555261
Mojtaba Khamenei ameteuliwa kuwa Kiongozi Mkuu mpya wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Tofauti na mtangulizi wake, yeye anajulikana kwa msimamo mkali zaidi na kuungwa mkono na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC).

  • Ana umri wa miaka 56, hivyo bado ni kijana ukilinganisha na viongozi wengi wa kidini nchini humo.
  • Anajulikana kwa kuepuka kujitokeza hadharani, akibaki mtu wa ndani zaidi.
  • Baba yake na maulamaa wa kidini wanamwamini kwa kiwango cha juu.
  • Alikuwa jeshini wakati wa vita vya Iraq na Iran, jambo linalompa uzoefu wa kijeshi.
  • Mke wake, Zahra na mwanaye, waliuawa katika shambulio la anga la Israeli akiwa pamoja na baba yake.
 
🚨🇮🇷 Iran imebadilisha dikteta wa kidini na mwanawe asiye na sifa. Lakini kilichotokea kwa kweli ni hiki: IRGC imepanga mapinduzi ya kijeshi na kuyaita urithi wa uongozi. Ali Khamenei alikuwa Kiongozi Mkuu kwa sababu alikuwa Ayatollah. Mamlaka ya juu ya kidini. Aliamuru Walinzi wa Mapinduzi. Sifa za kidini zilimpa uhalali. Ujuzi wa kisiasa uliweka mfumo katika uwiano.

Mojtaba Khamenei hana chochote kati ya hivyo. Yeye si Ayatollah. Hana sifa za kidini. Hufanya kazi kwa siri, si hadharani. Uhusiano wake na IRGC? “Ukamili,” ikimaanisha yeye hawaamuru. Wao ni washirika. Wenza. Labda hata si wenza.

Kwa hiyo, nani anaendesha Iran sasa?IRGC. Wameweka mtu wao kwenye kiti cha Kiongozi Mkuu na kumuita mwana wa Khamenei ili ionekane halali. Hii ni utawala wa kijeshi wenye chapa ya kidini. Maulamaa wamepoteza. IRGC imeshinda. Ali Khamenei aliweza kuwaambia Walinzi wafanye nini kwa sababu alikuwa na mamlaka ya kidini waliyoheshimu. Mojtaba anawahitaji kwa uhalali. Huyo si kiongozi. Huyo ni kikaragosi.

Mfumo wa Iran ulikuwa daima “Jamhuri ya Kiislamu”: dini kwanza, kisha msaada wa kijeshi. Sasa imegeuzwa. Jeshi kwanza, dini kama mapambo. Trump alidhani kumuua Khamenei kungevunja utawala. Badala yake, kuliwapa IRGC kisingizio cha kuchukua udhibiti kamili huku wakihifadhi mwonekano wa mwendelezo. Urithi wa kifamilia kuficha mapinduzi ya kijeshi. Hicho ndicho kilichotokea sasa hivi.

Nafasi ya Kiongozi Mkuu ilipoteza nguvu mara tu walipoipa mtu asiye na sifa za kidini za kuithibitisha.
 
Back
Top Bottom