Mo Hawezi patikana..

Mo Hawezi patikana..

Kiukweli bora kuyasikia kwa jirani. Lakini ukiwa mke, mme mtoto au mzazi wa mhanga, jamani....ni jehanamu kamili maumivu ya moyo unayoyapata.

Kweli.tumuombee Mo apatikane mapema akiwa hai na tuzidi kuwaombea familia yake kipindi hiki kigumu ambacho hata lepe la usingizi hawalipati kwa mawazo........
 
Ni siku ya 3 sasa tajiri na mmoja kati ya watu walioajiri vijana wengi zaidi TZ haonekani.

Baada ya wiki watakaobaki na maumivu ni familia pekee huku jeshi la polisi litazidi kujinasibu kushikilia watu ambao kiuhalisia hata hawaelewi chochote.

Mipango ya kumteka mtu kama Mo haiwezi fanywa na zaidi ya watu 5 tena wanaofahamiana vyema. Naona kabisa nafasi ya Mo kuonekana akiwa salama ni ndogo sana. Yote kwa yote Ulinzi wa Mungu umuangazie huko aliko Jeshi letu halitaweza kamwe kufanikisha kumpata
Organised crime
 
Kuna vitu wanaandikishana na makontena hivyo mtamuona soon.
Yule Mchungaji anajiita command mashimo kasema ataachiliwa leo amepiga maombi ya kufa mtu kasema. Ngoja tusubirie usiku upite kwanza hawaachiliwagi mchana ili wasipajue
 
Mkuu una uhakika gani kama Mo hajajiteka mwenyewe?? Mimi naona hii ni "movie" tu imechezwa kwa sababu fulani fulani ambazo hatuzijui. Kama kweli ametekwa Serious basi watekaji wangeshadai fidia muda mrefu sana. Ukiona mtu anatekwa pasipo watekaji kudai "fidia" basi fahamu huo utekaji unamashaka makubwa.

Kama lengo lao lilikuwa ni kumuua basi wangeweza kumchapa "risasi" pale pale nje ya Hoteli, na kama lengo lao ni kupata "information" basi mpaka sasa hivi wangekuwa wameshamwachilia, na pia kama lengo lao ni kupata pesa pia mpaka sasa wangekuwa wameshadai walipwe fidia (ransom).... Kwa kifupi mimi naamini Mo amejiteka mwenyewe.
 
Kinachoumiza wanaopotea kwa kutekwa wakirudi wanakaa kimya hawana maelezo yoyote. najua atapatikana japo hatakuwa na maelezo
Ni moja ya masharti ya kuachiwa Roma anauzoefu kwa hilo.
 
Akipatikana nitaamini kua ngamia anaweza kupenya kwenye tundu la la sindano!

WaTanganyika walivyo wanafiki sasa hivi wana kikampeni eti bring back our Mo...ngoja baada ya wiki uone kila mtu kashahau na maisha yanaendelea na wataendelea kumsifia Pombe ambaye kwa mtu mwenye akili timqmu anajua fika kabisa kuna mkono wa "system" ktk kutekwa kwa jamaa!


Oneni kwa yule tajiri mkurya wa Tarime Zakaria...zilivumaa weee lakini sasa hivi kimya.
Angekua boya si ungekuta na yeye kapotea kama huyu Muhindi?

Truth be told, Kichaa anahusika na huu uhuni unaoendelea hapa Tanganyika!


Ila ninawahakikishieni kua KAMA KWELI POMBE ndo MDHAMINI wetu sisi Raia wa Tanganyika....basi yule MUHINDI hataonekana tena na huu upepo utapita pia na tutausahau kama tulivousahau ule wa Tundu Lissu.

It's everyone for himself now.
 
Mkuu una uhakika gani kama Mo hajajiteka mwenyewe?? Mimi naona hii ni "movie" tu imechezwa kwa sababu fulani fulani ambazo hatuzijui. Kama kweli ametekwa Serious basi watekaji wangeshadai fidia muda mrefu sana. Ukiona mtu anatekwa pasipo watekaji kudai "fidia" basi fahamu huo utekaji unamashaka makubwa.

Kama lengo lao lilikuwa ni kumuua basi wangeweza kumchapa "risasi" pale pale nje ya Hoteli, na kama lengo lao ni kupata "information" basi mpaka sasa hivi wangekuwa wameshamwachilia, na pia kama lengo lao ni kupata pesa pia mpaka sasa wangekuwa wameshadai walipwe fidia (ransom).... Kwa kifupi mimi naamini Mo amejiteka mwenyewe.
Utekaji mwingine hauhitaji kuomba fidia, kumbuka waliyemteka ndio boss wa kampuni kama wangetaka kutumia hostages kupata pesa wangeteka ndugu yake wa karibu.
Hawa jamaa kama ni pesa basi wanatumia njia za kimtandao kumuibia na huwezi kujua inachukua muda gani kufuta "traces" zote za wao kukamatwa Japo upande wa pili inaweza ikawa ni njia ya kufanya "political spinning" hivo upepo ukikata watamrudisha bila hata jeraha.
 
Inshallah MO atapatikana.

Mungu ni muweza, Mungu ni mkubwa, Mungu ni mwema sana. Naamini kwa uwezo wake hakuna linaloshindikana.
 
MO kaleta shida kubwa kwetu madereva,tunapigwa faini za barabarani zisizo za haki na askari walitapakaa kila mahali.
 
Back
Top Bottom