Mo Dewji anzisha king'amuzi chako, Azam wanatawala sana

Na huko kwenye biashara nako ni kuiga tu products za watu, kwa kubadirisha majina tu!!kama kwenye vinywaji ndio balaa, anasubilia azamu aanzishe kinywaji kipya sokoni kikikubalika tu utasikia naye huyo!!anaongeza neno MO"....ila kinachomshinda ni radha kuipatia!!labda kitu ambacho hakuiga alitumia akili yake ni yale maguta yake ambayo yanalia kama genereta la meli, kelele tupu!!!
Ndugu yangu unajua Mo hela amepta wapi ?
Unajua biashara ya nafaka Mo ndio exporter mkubwa wa korosho, ufuta ,mbaazi nakadhalika unaijua hiyo biashara ilivyo kuwa na hela wacha kabisa nasema wacha kitu kama hujui huyo jamaa... He might be a true richest man in Tz.
 
Hawawezi kukutoa kwa sababu tu ya masharti yao. Timu za chini ya ligi kuu hazijapewa masharti ya kutoingia mikataba na wawekezaji, sasa huwezi kuzuia mtu kutekeleza mkataba wake sababu tu ya masharti yako ambayo yeye hakuwa sehemu ya makubaliano. labda kama utamlipia gharama za uvunjaji wa mkataba huo. Na hapo ndipo patakapolazimu majadiliano baina ya pande zote tatu, TFF, Azam na hao wengine
Baba unazunguk sana..ligi kuu ina mkataba na azam yyte anayeshiriki lazima aendne na mktaba
 
Kwanza mimi ninachojiuliza hivi hao kina Mo, na GSM, kuna faida gani hasa wanazopata kutoka kwenye timu hizi?
Ukichukua mapato na matumizi ni kama ardhi na mbingu!!halafu utasikia jitu linasema ohhh eti wanatuibia?!!simba, yanga charter kubwa!!!
Hao kina METL na GSM wanazitumia hizo clubs kama marketing strategy na inawalipa sana compared na hela ambayo wanatumia kurun hizo clubs.

Bidhaa za Mo zinaposafiria brand ya Simba zinafahamika kwa uharaka zaidi kwa consumers..same goes to GSM kwa case ya Yanga.

Yanga na Simba wana Mashabiki kila kona ya nchi hii. So ukitumia brand ya hizi clubs kujitangaza unafahamika haraka sana na ku attract wateja.

Hivyo kiujumla ni marketing tu ya hayo makampuni na kiuhalisia ingekuwa kama Europe huko Mo na GSM walitakiwa watoe mpunga mrefu zaidi kujitangaza kupitia clubs.
 
Usione vyalelea ujue vimeundwa!!! Mkuu investment aliyofanya Azam ktk kufanikisha kwake kuona hizo mechi sio ndogo, kuna ajira, watu wamepata, ushindani umeongezeka na muamko wa soka umekua mkubwa. Vile tulivyokua tunaviona DSTV sasa vinaonekana Bongo, tumpe sifa amefanya kazi kubwa sana. Kulikua na kipindi tunatamani DSTV waoneshe ligi yetu ila ilikua ngumu maana vifurushi vyao tu vilikua moto leo hii Azam amesababisha DSTV anzishe vifurushi nafuu.
 
Kumchukia mwamedi hakutapunguza ufukara ulio nao !!! Pambana fisi wewe mlaumu mamaako kuzaa na babako masikini
Kwa hiyo wewe ukimpenda ndiyo unakuwa tajiri? Basi mwambieni aanzishe ili ashindane na Azam kama ana hiyo jeuri.
 
Ngoj nikuach tyuuu! Sik hz watot hamn akil hat kidog. Mnatukan tyuuu bab zen mchan kweupe.
Uandishi wako huo wa hovyo kabisa! Mo Ni tajiri kubali tu usiweke hasira za unasikini wako kwa wenye bidii, asingekuwa na hela asingemudu kuihudumia Simba kwa miaka yote hii.
 
Nilichoshwa na ile kandarasi! Eti tenda anapewa mwenye dau kubwa

Ukiangalia EPL, La liga, Bundasliga n.k utaona zinaoneshwa na TVs kibao hadi za uarabuni huko

Sasa nikajiuliza, kwanin TFF wasingetoa % kwa kila media ili wapate ukwasi kutoka media nyingi na wawarahisishie watu kuangalia mpira bila kulazimika kuwa na Azam!!???

Lakini nikajua tu kuna mawili;
Umbumbumbu wa TFF na fursa kwa Azam
Upigaji wa TFF na fursa kwa Azam

Yote kwa yote wanatufanya tununue liazam wakati wengine hata hatulitaki
Tatizo mifano yenu tu ndo inanichosha...haiendani kabisa
 
Bilionea Mohamed Dewji, wewe ni mdau mkubwa wa soka na unaufahamu vizuri sana. Najaribu kukushawishi uanzishe king'amuzi au decorder itakayoitwa mo sattelite tv. Pamoja na vipindi vingine uanzishe channel za soka za kuonyesha live mechi za ligu kuu ya bara. Ukiritimba wa azam na TFF ni hatari kwa mustakbali wa soka nchini.

Ukiangalia mambo 2 makubwa la kwanza hakuna tv inayoingia mkataba na chama cha soka cha nchi husika kwa miaka 10 eti kwa bilioni 250 yaani kila mwaka bilioni 25. Mechi 4 tu za yanga na simba zinawarudishia gharama zote. La pili TFF na Karia hawaangalii maslahi kwani hii tenda waliyoipata azam ilikuwa inatakiwa iwe ya miaka 3 mitatu tu.

Kuipa miaka10 bila tenda ni ukiukwaji mkubwa. Tuna dstv, star times na nyinginezo zingeshindanishwa na kupewa asilimia kila tv. TFF ingeingiza matrillioni. Kwa kuwa upo simba anzisha decorder yako na wafunze hawa TFF international broadcasting kama England.

Usikubali kuiingiza simba katika mtego huu. Simba ni timu kubwa wakitaka azam kuonyesha mechi zenu igeni real madrid au barcelona. Kila game wawalipe kiasi fulani kikubwa na kama derby isiwe chini ya 1 billion shs. Najua watakataa, lakini njia bora ni wewe kama bilionea kuziokoa timu kama coastal union, Namungo na nyinginezo. Karia kauza. Anzisha decorder yako. Watu ndio wataujua ukweli wa azam tv na TFF. Wewe ndio mwokozi wa timu ambazo hazina uwezo.
Hivi unadhani Mo anaweza ku challenge pilika za Azam kwenye uwekezaji ktk soka...FIKIRIA VIZURI Muddy hana ubavu wa kuweka hata b100 kwenye huu udhamini aliofanya Azam..kama unabisha tuombe uhai baada ya miaka 10 kama atatokea umbwa yeyote anayeweza kuja na dili nono,so that tutaachana na Azam.
 
Nilichoshwa na ile kandarasi! Eti tenda anapewa mwenye dau kubwa

Ukiangalia EPL, La liga, Bundasliga n.k utaona zinaoneshwa na TVs kibao hadi za uarabuni huko

Sasa nikajiuliza, kwanin TFF wasingetoa % kwa kila media ili wapate ukwasi kutoka media nyingi na wawarahisishie watu kuangalia mpira bila kulazimika kuwa na Azam!!???

Lakini nikajua tu kuna mawili;
Umbumbumbu wa TFF na fursa kwa Azam
Upigaji wa TFF na fursa kwa Azam

Yote kwa yote wanatufanya tununue liazam wakati wengine hata hatulitaki
Hivi hata ilitangazwa tenda?,walioomba ni kina nani?
 
Uandishi wako huo wa hovyo kabisa! Mo Ni tajiri kubali tu usiweke hasira za unasikini wako kwa wenye bidii, asingekuwa na hela asingemudu kuihudumia Simba kwa miaka yote hii.
Tumia akili wewe! Huyo niliyekuwa namuandikia hivyo ni bongotole mmoja aliye ni quote! Alianza yeye kuniandikia hivyo 'tyuu'!! Na mimi nilikuwa namsanifu tu! Sasa wewe unachukulia kama ndiyo mimi vile!
Unategemea mimi na akili zangu naweza nikatumia aina hiyo ya maandishi?

By the way, kama huyo Moo wenu ana hela kiasi hicho cha kuanzisha luninga ya michezo ili kushindana na Azam, si aanzishe sasa!
Ameshindwa kutoa bilioni 20 kwa Klabu, ndiyo awe na uwezo wa kushindana na Azam wanaodhamini Ligi kwa mabilioni ya shilingi!! Muwe mnajiongeza wakati fulani!
 
Hivi unadhani Mo anaweza ku challenge pilika za Azam kwenye uwekezaji ktk soka...FIKIRIA VIZURI Muddy hana ubavu wa kuweka hata b100 kwenye huu udhamini aliofanya Azam..kama unabisha tuombe uhai baada ya miaka 10 kama atatokea umbwa yeyote anayeweza kuja na dili nono,so that tutaachana na Azam.
Mashabiki wa Simba wana mihemko sana! Yaani Forbes inawalisha matango pori, na wenyewe wanaamini huyo Moo eti ndiye Tajiri namba moja nchini!!

Ukiwaambia ukweli wanatokwa na mapovu! Kisa eti anaidhamini Simba! Sasa mbona timu nyingi tu za Ligi kuu zina wadhamini na wamiliki kabisa!! Na wao ni Mabilionea bila shaka, tena wa kushindana na Mwekezaji Mkubwa kama Said Salim Bakhresa!!

Umbumbumbu mbaya sana.
 
Boss Mo pesa zake ziko kwenye vitabu vya Forbes, madeni ni mengi likiwemo 20 bil. ya timu yetu ya Simba tunamdai
Kuna wakati unakuwa na point mpaka basi!! Ila sasa kichwa chako kikitibuka, ni kuweka tu dislike 😡 mwanzo mpaka mwisho!!

Wewe ndiyo Kitimoto bhana!! 😁😁😁
 
Asante ndugu mleta mada,
Mimi hili wazo nalichukua kama lilivyo naenda kupest kwa MO.
Akikubali anipe kazi akikataa namusema kwa mama apandishiwe kodi kwenye biashara zake.
 
Back
Top Bottom