Zaidi ya mwaka mmoja uliopita, hiyo ikiwa ni mara ya pili (first time ilikuwa 2009) nilitoa changamoto hapa JF kwamba ni kwanini basi CHADEMA wasiitekeleze sera yao ya majimbo kwa kuanzia na majimbo ya kiungozi kwa chama badala ya kusubiria kushika dola! Nilisema kwamba, inaonekana wazi sehemu ambako CHADEMA imetoa viongozi ngazi za juu basi nako huwa wanakuwa na nguvu kubwa sana. Nikatoa mifano ya Kigoma, Arusha, K'njaro! Aidha, nikashauri kwamba viongozi waliopo ambao ni influencial kv Mnyika, Zitto, Heche, and the like ndio wawe viongozi wa awali kwenye kanda hizo bila kuangalia origin! Kwamba, eti kv Zitto anatoka KGM basi akaongoze kanda ya huko!! Kwamba viongozi watoke pale Kinondoni makao makuu na waende kuongoza kanda hizo mpya! Hii maana yake ni kwamba, endapo Watanzania wanavutika sana na viongozi wenye majina makubwa, basi uwepo wa viongozi hao kwenye kanda hizo unge-stimulate shauku ya watu kutaka kujiunga nao.
Hili, limefanyika and the pleasure is mine hata kama si maoni yangu ndiyo yaliyowafanya wao walete mpango huo! Pamoja na yote hayo, lazima nitamke wazi kwamba CHADEMA wamekurupuka na hawakutumia busara hata kidogo! Hakuna upungufu wa busara uliotumika kama kuanza na Kanda ya Kaskazini! Yaani hili limefanyika katikati ya tuhuma mzito kwamba CHADEMA ni chama kinachoendekeza ukanda! Mtoa mada ameita "PROPAGANDA DHAIFU!" Msijidanganye, hii si propaganda ya kupuuzwa hata chembe na itakuwa ni kituko kujiaminisha kwamba ni propaganda dhaifu wakati kila siku inaendelea kumea kwenye mioyo ya Watanzania! Na hali inakuwa mbaya zaidi pale CHADEMA wanapozindua jambo linaloashiria hizo hizo mnazoita propaganda dhaifu! It's very unfortunately, utawala wa awamu ya kwanza ulituaminisha kwamba utawala wa majimbo ni hatari kwa mustakabali wa taifa hili....this means that suala zima la utawala wa majimbo halifahamiki vizuri na Watanzania. So unapoanza na uzinduzi wa Jimbo la Kaskazini, kwa chama kinachotuhumiwa Ukaskazini, hapo bila shaka ni kuwapa gazeti la Uhuru best Headline of the Week!! So what, hapo Nape akisimama jukwaani na kusema "si mmeona, tuliwaambia kwamba hawa wana ajenda ya Ukaskazini....!!" je, mtamkejeli kama ilivyo silika yenu?!
Binafsi nilitarajia CHADEMA wangeanza na jimbo la Kusini kwa maana ile ile! Kwamba, pamoja na kujidanganya mnakojidanganya hapa jamvini kwamba mna wanachama wa kutosha nchi zima lakini ukweli bado unabaki pale pale kwamba kuna maeneo, hususani kusini; CHADEMA hamna chenu kule!! So kwa kuanza na Kusini, tena unamweka mtu kama Zitto Kabwe kuwa Katibu Mkuu wa Southern Province, basi sina shaka kwamba angebadilisha status ya maeneo hayo kwa hali ya juu sana! By the way, kuanza na sehemu kama hiyo ingetoa positive justification...! Sizani kama kuna jibu la kuvutia as to why mmeanza na Kaskazini lakini the answer could be short and clear kwamba mmeamua kuanzisha uongozi wa Kikanda na kuanzia Kusini coz' you don't have enough supporters kule!!