Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,180
- 7,355
Naomba nitofautiane moja kwa moja na mpango huu wa chama changu wa kuanza kuzindua kanda kwa kuanzia kaskazini. Kimsingi naunga mkono hoja ya kupeleka madaraka kikanda ya CHADEMA. Hata hivyo, kama nilivyosema siku CDM inatangaza mpango huu, implementation yake uwe kwa umakini mkubwa sana ili isiwe na reputational impact kwa chama. Na hapa naona kama chama kimeshaanza kuvurunda.
Hoja yangu ni kwamba
Napendekeza kuwa CDM kisithubutu kuruhusu kanda ya kaskazini iwe ya kwanza kuzinduliwa kwa mpango huu.
Mpango huu uliasisiwa na uongozi wa juu wa CDM, na kiukweli, huku chini wengi wanasubiri kuelimishwa utendaji wake. Kwa kanda ya kaskazini kuanza moja kwa moja kuzindua mpango huu, tena akiwepo mwenyekiti, ni wazi kwamba CDM, hasa kwa maeneo ambapo haijaimarika sana, wameachwa kwenye mataa. Kesho na kesho kutwa kanda nyingine zitakapoanza kufanya mpango huu, bila kuelimishwa, watachemsha, na endapo wakienda kuelimishwa itaonekana kuwa wanaelimishwa kitu ambacho wametoka nacho huko kanda ya kaskazini, maana wao bila hata kuelimishwa wameweza kufanya hivyo.
Narudia tena, chonde chonde, mheshimiwa Mbowe, mheshimiwa Slaa, sitisheni zoezi la uzinduzi wa kanda yeyote kwa sasa, undeni timu ya watu maalumu, watakaoandika terms and conditions za uanzishwaji na uendeshwaji wa kanda za CDM, timu hii izunguke nchi nzima ikiwasomesha wadau viongozi, na baada ya hapo utaratibu wa kuanzishwa kanda uanzishwe, na usimamiwe kwa karibu na viongozi wa juu, na usianzie kaskazini.
Lakini pia tukumbuke kuwa ni majuzi tu katibu katangaza mpango kabambe wa M4C. Sasa endapo haya mambo hayatatekelezwa bila interactions za hali ya juu, then yanaweza kuleta negative impacts kwa chama. Hii ina maana kwamba viongozi (wote) kuanzia hivi sasa watakuwa bize na kuanzisha kanda, at the same time kuendesha M4C. Probably performance ya moja au yote itaathirika kwa kiasi kikubwa. Kwa kuwa suala la zonalization ni muhimu sana, then liendeshwe kwa umakini, na kusiwepo na papara yeyote. Viongozi, wanachama, na umma waelimishwe kwanza kuanzia sasa, na kwa maoni yangu zonalization ianze pengine mwakani, tena baada ya uchaguzi wa ndani wa chama.
This is a technical advice, mkitaka uchukueni, la hamtaki uacheni, but impacts zake mtaziona...
Hoja yangu ni kwamba
- kwa kuwa zipo kanda ambazo CDM, haijaimarika kama kanda ya kaskazini
- kwa kuwa CDM imeimarika zaidi katika kanda ya kaskazini (idadi ya wabunge na madiwani wa kuchaguliwa ni ushahidi)
- kwa kuwa maadui zetu wanatumia propaganda(dhaifu), kuwa CDM ni chama cha kikanda (ya kaskazini)
- Kwa kuwa mwenyekiti na katibu wa CDM wanatokea katika kanda hii
- kwa kuwa mpango huu wa kuanzisha kanda ni mgeni kwa CDM
Napendekeza kuwa CDM kisithubutu kuruhusu kanda ya kaskazini iwe ya kwanza kuzinduliwa kwa mpango huu.
Mpango huu uliasisiwa na uongozi wa juu wa CDM, na kiukweli, huku chini wengi wanasubiri kuelimishwa utendaji wake. Kwa kanda ya kaskazini kuanza moja kwa moja kuzindua mpango huu, tena akiwepo mwenyekiti, ni wazi kwamba CDM, hasa kwa maeneo ambapo haijaimarika sana, wameachwa kwenye mataa. Kesho na kesho kutwa kanda nyingine zitakapoanza kufanya mpango huu, bila kuelimishwa, watachemsha, na endapo wakienda kuelimishwa itaonekana kuwa wanaelimishwa kitu ambacho wametoka nacho huko kanda ya kaskazini, maana wao bila hata kuelimishwa wameweza kufanya hivyo.
Narudia tena, chonde chonde, mheshimiwa Mbowe, mheshimiwa Slaa, sitisheni zoezi la uzinduzi wa kanda yeyote kwa sasa, undeni timu ya watu maalumu, watakaoandika terms and conditions za uanzishwaji na uendeshwaji wa kanda za CDM, timu hii izunguke nchi nzima ikiwasomesha wadau viongozi, na baada ya hapo utaratibu wa kuanzishwa kanda uanzishwe, na usimamiwe kwa karibu na viongozi wa juu, na usianzie kaskazini.
Lakini pia tukumbuke kuwa ni majuzi tu katibu katangaza mpango kabambe wa M4C. Sasa endapo haya mambo hayatatekelezwa bila interactions za hali ya juu, then yanaweza kuleta negative impacts kwa chama. Hii ina maana kwamba viongozi (wote) kuanzia hivi sasa watakuwa bize na kuanzisha kanda, at the same time kuendesha M4C. Probably performance ya moja au yote itaathirika kwa kiasi kikubwa. Kwa kuwa suala la zonalization ni muhimu sana, then liendeshwe kwa umakini, na kusiwepo na papara yeyote. Viongozi, wanachama, na umma waelimishwe kwanza kuanzia sasa, na kwa maoni yangu zonalization ianze pengine mwakani, tena baada ya uchaguzi wa ndani wa chama.
This is a technical advice, mkitaka uchukueni, la hamtaki uacheni, but impacts zake mtaziona...