Mnyika kuzindua kanda ya Kusini rasmi

Mnyika kuzindua kanda ya Kusini rasmi

Ni kweli!, mimi na timu yangu tunalipwa na CCM kupambana na Chadema kwenye social media ... tunajua kuwa ACT ilianzishwa kwaajili ya kudhoofisha Chadema!. Hatujawahi hata siku moja kuandika taarifa za uchunguzi kuhusiana na uhusiano wa moja kwa moja wa CCM na ACT ... Kwetu sisi CHADEMA ni Tishio na kila siku huwa tunajaribu kuipakazia udini, Ukabila na Ukanda!. Mimi siku zote nimekuwa mtetezi wa ZZK hata kwenye Sakata la ESCROW sikuwahi kuhoji kwanini PAC ilijaribu kuwapotezea BoT na wahusika waliokwapua Stanbic Bank ..
Pasco
Hahahahahaaa... Mkuu Pasco, kama hukuwahi kuhoji kwanini PAC iliwapotezea BoT, mie Msaka tonge mwenzako uvumilivu ulinishinda na nilihoji ni kwanini Zitto katika ripoti yake alionekana ni kama anam-defend Gavana Ndulu hadi nikatoa mfano wa Bank Teller kwamba, pamoja na ukweli Bank Teller ndie mtu wa chini kabisa among Bank Staffs (Bankers) lakini yeye ndie mwenye sauti ya mwisho kuamua alipe au asilipe! Teller akishakuwa na mashaka, mathalani na cheque iliyopo mbele yake, hata Branch Manager hana ubavu wa kumlazimisha alipe! Nikahoji, sasa ikiwa Bank Teller ana maguvu yote hayo, inakuaje Gavana wa Benk Kuu aonekana hana hatia wakati yeye ndie Head Teller not mentioning kwamba taasisi yake inajitegemea!! Kwanini Zitto kila wakati alikuwa anaonekana kumtetea sana aGavana Ndulu!!!??
 
Last edited by a moderator:
Mmechelewa, Mtwara twasubiri kuipokea ACT Wazalendo, Chadema ni chama cha kaskazini

Hivi ni lini ulirudisha Kadi ya Act mkuu?ama ndio yale yale act ni nyumba ndogo Yenu kwa masisiem!!!
 
Mkuu nadhani naweza sema nimekuelewa vizuri tu na kama hiki ndicho kilichopelekea kupishana maneno na.wadau wawili watatu hapo mwanzo basi hawakutaka kukuelewa, Kimsingi kuna hoja yenye majibu mazuri tu na kila mmoja angetoka anatabasamu..

Ni kweli kama unavyosema wengi wamekuwa wakitaka Chadema hata kama inafanya mikutano basi isifanye kwa sana yale maeneo inayokubalika kwa sana IJIKITE VIJIJINI na hiiw hoja yako ni moja ya hoja ambazo zimekuwa na mchango mzuri tu na nadhani zinafanyiwa kazi na viongozi.wanaopita hapa.

Ila mkuu nadhani kwenye Mfumo wa Kikanda, ni kweli tunahitaji watu Origin kama unavyodai, isipokuwa pale penye upungufu wa Viongozi wanaomata kwamaana walio "Maarufu" na wazuri wa kujenga hoja Jukwaani basi Viongozi wa Makao makuu na wale ambao wananguvu kwenye chama wanatakiwa waongeze Nguvu kwa sehemu hizo zenye Viongozi Dhaifu wa Kikanda kwa kufanya mikutano mara kwa mara ikiwemo kuendesha operesheni za kila wakati ili kuu-Keep Busy Kanda hisika isilale. Nadhani kwa kufanya hivi tungeondokana na Propaganda ambazo zingejitokeza kwamba Chadema imeshindwa kuwaamini Viongozi Origin wa kanda husika badala yake imeleta viongozi waw Kanda nyingine ili kuongoza Kanda fulani.

Kama utakumbuka kwenye uchaguzi wa Karenga kama sikosei Chadema kwa kudhamiria kushinda uchaguzi ule iliamua kuita Mawakala toka Arusha ili kuongeza ufanisi ktk zoezi la kuhesabu kura. Matokeo yake ni jambo hilo kugeuka na kuwadhuru wao wenyewe pale Ccm walipodai kwamba Wanakarenga hawaaminiki ndani ya Chadema ndiomaana wameletwa mawakala toka Arusha na kwamba Chadema hawataki kutoa hela za uwakala kwa wanakarenga isipokuwa kwa Wanaarusha. Wakaenda mbali zaidi kwa kudai, kama wao wameahindwa kuwaamini kwanini wao waamini kwa kuwapa kura zao? Naam madhara ya propaganda hizo sote tunayafahamu.

Kwakusema hayo mkuu NasDaz ningeomba uangalie wazo hili na labda tujikite kutokana na hapa tulipo, Uboreshaji wa kanda hizi na nguvu yake kuelekea uchaguzi mkuu. Na Vilevile tukumbuke hapa ilipo leo Chadema kwenye kanda hizi za kusini sipo ilipokuwa hapo awali, kiuhakika imesonga mbele ingawaje si kwa kiwango kile kilichotegemewa ama kulinganisha na Kanda zingine.

BACK TANGANYIKA
 
Last edited by a moderator:
Mkuu,NasDaz nakushauri kuna watu humu usibishane nao sana, hawachelewi kukutia hasira ukajikuta unakula ban bila kutegemea, niulize mimi, bado naikumbuka my one and only ban, ilitokana na watu kama hawa!, yaani Chadema ina baadhi ya mijitu mijinga ajabu, hadi unajuiliza hivi chama kiliipatia wapi mijitu kama hii?!, halafu unaambiwa hio ndio line-up ya watendaji wa Chama kuuingiza Chadema Ikulu ya Magogoni!..God forbid!.

Niliwahi kusema humu, tukifanya hesabu ya total mileage nani haswa wanaoisaidia Chadema kiuhalisia kati sisi ma critiques na ma praise worshipers!, utakuta sisi tunaikosoa Chadema ndio tunaisaidia zaidi kuliko hao machiriku wake humu ambao kazi yao ni kuiimbia nyimbo za sifa tuu na mapambio!, na siku Chadema inakula kipigo, hao ndi wa kwanza kulia kwa makelele na kujigalagaza chini utadhani wamepata msiba!.

Kwa lengo la critique ni kukisaidia Chadema, then usiwajali kabisa hawa mashabiki maandazi, endelea kutembeza bakora tuu, don't spare the rod and spoil the child!.

Pasco


Hata wewe tunakupuuza kama tunavyoyapuuza magamba yote.Njaa yako imekimbilia ubongoni na sasa unaonekana kituko kwa kukosa msimamo.
 
NasDaz Nimepitia uzi wote huu na kweli nimeona mashambulizi ya kipumbavu kabisa ambayo hukutakiwa kuyapata. Ni kweli baadhi yetu (Wahumini wa CDM) tuna matatizo makubwa sana, nimekusoma vizuri sana na nimelielewa lengo lako, kuhusu Mnyika ni labda wengi wanadhani kwamba ulikuwa unamshambulia jambo ambalo si sahihi.. Lakini pia hata wewe uwe unaangalia watu wa kujibu hoja zao. Wengine unawaignore tu.. Sikuhizi kuna mijitu mingine ya CDM imepoteza weledi wa kujibu hoja kwa hoja badala yake wao ni ACT na Zitto. Hawa mi nawafananisha wa wale akina lasi si pesa ambao akili zao wameshikiwa, hii post haihusiani chochote na ACT wala Zitto lakini nimeshangazwa na watu kushambulia upande huo..

Lakini hata wewe kubali tu umekongoroka mahali, kama mlivyokubaliana na mkuu Pasco kwamba nyie ndio mnaoisaidia CDM kuliko hata wale washabiki wake, sasa kwanini ulalamike juu ya ushauri ambao unadai uliutoa?? Nadhani ungekuja na post ya kufurahishwa na jambo ambalo ulishauri chama na limetekelezwa.

Mwisho, tuko hapa kupambana na CCM and the only winning team is UKAWA hivyo hata kama utaendelea kutukosoa hapa hakikisha kura yako ya Udiwani, Ubunge na Urais unatudondoshea. Shukrani
 
Last edited by a moderator:
Mkuu JokaKuu,
Kama kumbukumbu zangu zipo sawa, Kanda ya Kusini inaongozwa na Matiko Matare! Je, unamfahamu Matiko Matare? Kama haumfahamu, je. hilo jina lina dalili ya kuwa ni mtu wa Kusini? Kwa ufupi tu Matiko Matare ni Mkurya wa Musoma... ikiwa unalikumbuka sakata la UDSM mwaka 1989, Matare alikuwa ndie Rais wa DARUSO... lakini pamoja na yote, amepewa Kanda ya Kusini na mimi katika hilo sina tatizo hata kidogo provided ana uwezo wa ku-deliver lakini I doubt ikiwa anao uwezo huo!!!

..Matiko Matare aliachia ngazi.

..siku hizi ni Mchungaji, kwa hiyo aliona majukumu ya chama yataathiri kazi yake ya uchungaji.

..lakini ukumbuke kwamba Matiko Matare ana mizizi huko kanda ya kusini. Matiko amekuwa akiishi huku kwa muda mrefu kidogo.

..nadhani CDM wata-benefit zaidi kama watapanua uwigo wa nafasi za uongozi kwa ku-recruit makada wenye uwezo toka mikoani, ili wakisaidie chama hukohuko mikoani.

..kama kuna mkoa au kanda ambayo imekosa uongozi imara, basi makao makuu wanaweza kutuma watu kwenda kuwaongezea nguvu. lakini haja ya kuwa na viongozi wenyeji wa maeneo husika; wanaoelewa mila, miiko, taratibu, na tamaduni za maeneo hayo, nadhani ni suala la kuzingatiwa.
 
Sasa huku kusini na wachaga wapi wapi??

Hicho mnajua fika ni chama cha kikanda kidin na kikabila.

Huku mnafuata nin.

Mnapoteza muda wenu tuh
 
Chadema kusini mnjisumbua tuh.

Wamakonde sio wapuuz tuwape kura wachaga.

Kwan kilimanjaro pekee haiwatoshi??

Mmekiua chama wenyewe kwa kuendekeza udini ukanda na ukabila.
 
Chadema kusini mnjisumbua tuh.

Wamakonde sio wapuuz tuwape kura wachaga.

Kwan kilimanjaro pekee haiwatoshi??

Mmekiua chama wenyewe kwa kuendekeza udini ukanda na ukabila.
Chadema inaendelea kukua zaidi, tuhuma za udini siku hizi zimekufa, sasa hivi wimbo ni ukabila. Chadema jiimarisheni kupitia kanda
 
NasDaz,

..CDM wakitoa viongozi makao makuu na kwenda kuongoza mikoa na kanda watasingiziwa kuwa ni wabaguzi na wanaona wenyeji wa mikoa na kanda hizo hawafai kuongoza chama.

..kuna mikoa na kanda chache sana hapa Tanzania ambazo zinaweza kuongozwa na watu toka nchi ya maeneo hayo.

..Kwa mtizamo wangu hakuna njia ya mkato ktk suala hili. CDM wahakikishe kwamba kila mkoa na kanda zinapata viongozi ambao ni wenyeji wa eneo husika ambao wanauelewa wa tamaduni na changamoto za maeneo hayo.


cc Pasco, Crashwise, uaminifukazi, Molemo, Chademakwanza
Naomba niweke Mambo sawa viongozi wa kanda niwenyeji wa hizo kanda husika na ndio maana zinafanya vizuri sana
 
Last edited by a moderator:
ubungo maji hayatoki jamani da subiri nibebe ndoo niende kinondoni nikachote ya kunywa
 
Naomba niweke Mambo sawa viongozi wa kanda niwenyeji wa hizo kanda husika na ndio maana zinafanya vizuri sana
Zinafanya vizuri upande gani siuliza kwa mantiki ya kupinga bali kupewa maelezo zaidi ya kwanini hii sera ni muhimu kwa CDM ?

  • Kanda ni kwa sababu ya political value chain administration ama? na hao viongozi wa ukanda wanasaidia vipi juu kutunga let alone autonomy yao kwenye overall CDM objective?
  • Ukanda ni kwa sababu ya combination strategy za CDM? zipi na kuna inter-relation gani structure wise kuweza harmonize kutatua matatizo au kuweza kutunga national policies bora kwa yale yasiyo na ukanda?

Mtakuja kutuletea matatizo kudandia vitu msovyovielewa kwa kufanya vitu kichwa kichwa bila ya kujua taratibu gani za management zinahitajika let alone when you allow such thinking kwenye jamii ambazo perception za wengi bado ndogo.
 
Zinafanya vizuri upande gani siuliza kwa mantiki ya kupinga bali kupewa maelezo zaidi ya kwanini hii sera ni muhimu kwa CDM?

  • Kanda ni kwa sababu ya political value chain administration na hao viongozi wa ukanda wanasaidia vipi juu kutunga?
  • Ukanda ni kwa sababu ya combination strategy za CDM? zipi na kuna inter-relation gani structure wise kuweza harmonize kutatua matatizo au kuweza kutunga national policies bora kwa yale yasiyo na ukanda?

Tulivyosema sasa tunafanya kazi kitasisi ulielewa?
 
Tulivyosema sasa tunafanya kazi kitasisi ulielewa?
Naelewa nini taasisi ndio maana nimeuliza maswali yanayotaka kujua objective za taasisi kufikia malengo yake kupitia njia ya ukanda especially taasisi yenyewe ikiwa chama cha siasa..
 
Back
Top Bottom