Jamani naomba kuuliza kwa watu wenye mapenz mema na chadema hivi mnyika toka kawa mbunge ameleta maendeleo gan jimboni kwake zaid ya kelele anazopiga bungeni?
Pia ushauri mdogo tu kwa chadema muishio ubungo jimbo litabaki nyuma kama hamtombadilisha uchaguz ujao.kama hampend ccm mpeni chadema mwingine
[h=2]Saturday, December 22, 2012[/h] [h=3]‘SUMATRA idhibiti nauli Kibamba'[/h]
na Betty Kangonga
MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) imetakiwa kudhibiti nauli za daladala zinazofanya safari zake katika barabara ya Morogoro.
Inaelezwa kuwa daladala zinazokwenda Kata ya Kibamba zinatoza sh 650 na zile zinazokwenda Kiluvya zikitoza sh 900.
Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), alisema jana kuwa katika kikao kilichoketi Oktoba 4, mwaka huu alimkumbusha mwakilishi wa Sumatra kushughulikia tatizo hilo, lakini hadi sasa hakuna hatua zilizochukuliwa.
Alisema pamoja na Sumatra kutangaza nauli ya daladala Machi mwaka jana na kutaja eneo lenye nauli zaidi ya moja, lakini hakuna uwiano unaostahili baina ya njia za Kibamba na za maeneo mengine yenye umbali mrefu.
"Sumatra inapaswa kutoa maelezo kwa umma kuhusu hatua iliyofikiwa katika kudhibiti nauli za njia zinazokwenda Kata ya Kibamba ambazo zina wastani wa sh 650, huku njia nyingine zenye urefu zaidi au unaokaribiana na wa njia za Kibamba wastani wake wa nauli ukiwa sh 500," alisema Mnyika katika taarifa yake kwa vyombo vya habari.
Alisema kwa nauli zilizotangazwa na mamlaka hiyo njia ya Kibamba hadi Kariakoo inapaswa kuwa sh 650, Kibamba hadi Muhimbili sh 650, Kibamba mpaka Magomeni sh 650 na Kibamba hadi Kivukoni sh 650.
Mnyika alisema njia nyingine ndefu zaidi au zenye umbali unaokaribiana na ule wa Kibamba zinatozwa kiwango kidogo akitolea mfano Gongo la Mboto hadi Mwenge sh 500, Kitunda hadi Ubungo sh 500, Mbagala Rangitatu hadi Ubungo sh 500.