Umeweka mifano ya wabunge wenye wasi wasi na majimbo yao kiasi wako radhi kutumia fedha zao mifukoni kuwahonga watu waliokata tamaa ili wawape kura kwa kuwa waliwakopesha.
Labda nikuulize swali: Unadhani ni nani mwenye jukumu la kukopesha wajasiriamali? Mbunge au Financial Institutions?
Wewe niambie kwa akili yako unaonaje: Wabunge watoe 'hongo' za mikopo kwa wananchi au tukazania kwenye uboreshaji wa sera ili kila mwananchi akopesheke kwenye taasisi za fedha?
Kama ulivyosema, unaishi Dar. Sasa acha nikukumbushe kuwa UNAISHI DAR na SIO UBUNGO. Ubungo inakaliwa na watu wasomi wasiodanganyika na senti na mikopo isiyo na tija. Tangu waanze kukopeshwa hao wanaokopeshwa ni miaka, lkn maisha yao yako vile vile sbb ya sera mbovu za CCM. Sasa Mnyika anapoongea bungeni vilaza kama wewe unamuita 'muongeaji'.
Naomba unikumbushe tathmini ya 'the so called mabilioni ya Kikwete'. Kichefuchefu kitupu, na bado mpo mnaoamini kuwa mbunge akija kukukopesha sh 200,000 basi maisha yako yataboreka. Mkopo ukiupata huku sera za biashara na uchumi ni mbovu hamna kitu mdogo wangu.
Kwa faida yako na wenzio, mbunge ni mwakilishi wetu na sio mhamasisha michango. Mbunge anatusaidie mikwamo inayohusisha propaganda za kisiasa na sio fedha za mfukoni mwake. Akili zako zimekaa ki -CUF CUF nikimaanisha za KIKABWELA