Mnyika kaleta maendeleo Ubungo?

Mnyika kaleta maendeleo Ubungo?

tunapaswa kkmbuka kwamba hatra kipindi cha ukoloni watawala hawakuwa tayari kuwatengenezea waafrika mazingira mazuri ya kujitawala na kitu ambacho kinajitokeza kwa sasa hapa nchini ccm hawapo tayari kusaidia maendeleo katika majimbo yaliyoshikiliwa na upinzani kwahyo basi ni jukumu letu kuhakikisha tunaunga mkono wabunge wetu akiwemo Mnyika na sio kumvunja moyo ili kupambana na huu udhalimu wa chama kilichokosa mwelekeo ccm.
:der:!!!!!!!!!!!!!
 
kwa upeo wako hayo kayafanya mnyika au ni serikali? Mpango wa ujenzi ulianza lini ni swali unalopaswa kujiuliza
wewe ulitaka alete maendeleo yapi?atumie pesa yake ya mfukoni ndo uone kama kaleta maendeleo?acha kufikilia kitoto wewe.mbona hilo barabara haijajengwa ilala ai temeke,hayo majimbo hayana uhitaji au serikali haion?
 
Mtu katoa hoja ama swali la msingi, watu badala ya kujibu mkielezea mafanikio ya mbunge wenu mnarusha mawe, ndiyo yale ya CCM!!!! ukihoji jambo basi unatumiwa na wapinzani. Hivi nyie wanasiasa kulikoni? So Kikwete naye akiulizwa kuhusu mafanikio yake ajibu Mugabe kafanya nini.....Tunataka wanasiasa wawajibike regardless wanatoka chama gani, kwa sababu hawa wote wananalipwa toka kwenye kodi zetu.....we dont pay them kuigiza.
 
....ameleta maendeleo gan jimboni kwake zaid ya kelele anazopiga bungeni?
Pia ushauri mdogo tu kwa chadema muishio ubungo jimbo litabaki nyuma kama hamtombadilisha uchaguz ujao.kama hampend ccm mpeni chadema mwingine

Wewe huishi Ubungo, unauliza maswali kama unakimbizwa (kwakuwa hata nhukumalizia herufi zilizotakikana kwenye maneno), mwisho UNAMALIZIA kwa kujijibu mwenyewe ETI "JIMBO LITABAKI NYUMA".
Swali kwako; Hebu tuambie jimbo lako na mbunge wako pia maendeleo aliyoyaleta halafu sisi wa Ubungo tuendelee kukuwekea baadhi ya yale yaliyopo UBUNGO.
 
Mtemvu anataka awapeleke vijana wa Temeke wakawaburudishe waarabu huko Arabuni
bwahahahahahaha aiseee mtemvu anawaozesha vijaa na kwa waarabu umangani bwahahha
 
bwahahahahahaha aiseee mtemvu anawaozesha vijaa na kwa waarabu umangani bwahahha

:becky::becky::becky: mbunge huyo kawatafutia ajira vijana wa Temeke huko uarabuni kuwaburudisha waarabu sio wanakali uchumi tu wakati wakiwezeshwa wanaweza kuutumia
 
Hayo Maendeleo huyaoni? Morogoro Road inajengwa, Kimara kunajengwa daraja kubwa kuliko la Manzese huoni tu?

Mkuu najua vipo vyuo vya kufunza lugha ya kuwasiliana na mabubu na viziwi, lkn hii ya kwako ya kuwasiliana na wapumbavu umejifunza wapi?

Kuelewana na mtu mpumbavu kama huyu kwangu ingekuwa kazi sana, lkn kwa jibu lako naamini sasa na yeye ameyaona maendeleo ya Mnyika Ubungo. Tafadhali tu mbavu zangu
 
Mbunge kama mbunge hawezi kuleta maendeleao kwenye jimbo kwani hana chanzo cha mapato,bali serikali ndiyo yenye dhamana ya kuleta maendeleo na siyo ubungo tu bali Tanzania yote.Anachofanya mbunge kwa nafasi yake ni kuhakikisha maendeleo yanaletwa kwenye jimbo husika kwa kufuatilia watendaji ambao ni waajiriwa wa serikali na kuwasemea wanachi wajimbo lake bungeni.Anachfanya Myika John kingefanywa na wabunge wote yaani hata wa Chama Tawala leo Tanzania yetu ingekuwa Dubai ya pili.
Kama nimekosea naomba kurekebishwa.
 
Mkuu najua vipo vyuo vya kufunza lugha ya kuwasiliana na mabubu na viziwi, lkn hii ya kwako ya kuwasiliana na wapumbavu umejifunza wapi?

Kuelewana na mtu mpumbavu kama huyu kwangu ingekuwa kazi sana, lkn kwa jibu lako naamini sasa na yeye ameyaona maendeleo ya Mnyika Ubungo. Tafadhali tu mbavu zangu

:becky::becky::becky::becky: mkuu La Biblicana umenivunja mbavu, watu kama hawa wasio jua kazi ya mbunge ni nini katika eneo husika analo ishi inabidi umpe mifano ya wazi inayo onekana kabisa kwenye eneo analo ishi
 
Last edited by a moderator:
Naomba kuuliza kwa watu wenye mapenzi mema na CHADEMA hivi Mnyika toka kawa mbunge ameleta maendeleo gan jimboni kwake zaidi ya kelele anazopiga bungeni?

Pia ushauri mdogo tu kwa CHADEMA muishio Ubungo jimbo litabaki nyuma kama hamtombadilisha uchaguzi ujao,kama hampendi CCM mpeni CHADEMA mwingine.

wewe ni mjinga tena sana sababu watumiwa na huyo shonza.
 
:becky::becky::becky::becky: mkuu La Biblicana umenivunja mbavu, watu kama hawa wasio jua kazi ya mbunge ni nini katika eneo husika analo ishi inabidi umpe mifano ya wazi inayo onekana kabisa kwenye eneo analo ishi

Mungu aihurumie tu hii nchi, kama mtu mwenye uwezo wa ku - access web ndio ana mawazo haya, tumtarajie nini aliyoko Igunga huko vijijini kabisa? Ndio maana kuna wakati madikteta hutakiwa kunyoosha mambo. Mtu juha kama huyu unamweleweshaje mpaka akuelewe?
 
barabara ya external kupitia shungashunga, ujenzi kwa kiwango cha lami na kujengwa daraja jipya, ilikua haipo katika bajeti ya mwaka huu lakini kwa kelel za mnyika imetengwa na tanroad 1.2b ujenzi unaendelea, fidia kwa wakazi tisa wa barabara ya makoka ambayo ilishindwa kulipwa tangu mwaka 2004 lakini kwa kelele za mnyika wananchi wameshalipwa na barabara na nyumba zimeshabomolewa na ujenzi unaanza na imetengwa zaidi ya 180m, daraja la golani suka ambalo lilikua kero kubwa kwa watu wa kimara na saranga daraja limeshajengwa na lipo katika hatua ya umaliziaji, ujenzi unaendelea wa ujenzi wa tanki kubwa la maji na vioski vidogo kwa kata ya kwembe na kibamba mradi umefadhiliwa na BTC mkandarasi lucolo anaendelea na ujenzi huo, daraja la mpakani wa goba na makongo limekamilika. hii ni baadhi tu ya mafanikio kwa muda wa miaka miwili ukitaka zaidi ingia kwy blog ya mnyika.
 
Tehetehe hukimu inakaribia... 2015: Wabunge kupenda kujiingiza kwenye miradi ya kitaifa ati barabara ya mabasi yaendayo kasi, ati maji.... miradi hii haina uhusiano wowote na mbunge yeyote wa Dar...
 
Vivios kauliza kwania njema ila alivyojibiwa sasa...eeh! Hii ndio JF

Toka kwa MrArsenal

Jamani naomba kuuliza kwa watu wenye mapenz mema na chadema hivi mnyika toka kawa mbunge ameleta maendeleo gan jimboni kwake zaid ya kelele anazopiga bungeni? Pia ushauri mdogo tu kwa chadema muishio ubungo jimbo litabaki nyuma kama hamtombadilisha uchaguz ujao.kama hampend ccm mpeni chadema mwingine

ALIULIZA KWA NIA NJEMA EH? NIA NJEMA UNAMKANDIA MTU KUWA ANAPIGA KELELE BUNGENI? MAJIBU ULIYOPEWA NI DOZ INAYOKUFAA WALA USILALAMIKE
 
Tehetehe hukimu inakaribia... 2015: Wabunge kupenda kujiingiza kwenye miradi ya kitaifa ati barabara ya mabasi yaendayo kasi, ati maji.... miradi hii haina uhusiano wowote na mbunge yeyote wa Dar...
sasa kama haina mahusiano kwanini haikutengenezwa kabla ya mnyika kuwa mbunge ikiwa miradi mingine ilikwama tangu mwaka 2004, au serikali ilikua inasubili hadi mnyika awe mbunge ndio watekeleze?
 
Hayo Maendeleo huyaoni? Morogoro Road inajengwa, Kimara kunajengwa daraja kubwa kuliko la Manzese huoni tu?


Mi Nadhani wewe rudi tena darasani, maana hujaelimika na hujui Dunia Kama ni ya duara. Kamuulize Mnyika mwenyewe akutajie maendeleo aliyotuletea Ubungo uone Kama hayo uliyoyataja yamo
 
Mungu aihurumie tu hii nchi, kama mtu mwenye uwezo wa ku - access web ndio ana mawazo haya, tumtarajie nini aliyoko Igunga huko vijijini kabisa? Ndio maana kuna wakati madikteta hutakiwa kunyoosha mambo. Mtu juha kama huyu unamweleweshaje mpaka akuelewe?

mtu wa Igunga anaelewa mbunge lazima ampe chakula, mke wake akitaka kuzaa nijukumu la mbunge kumhudumia wabunge wengi wanalalamika wapiga kura wao huwa wanawasumbua usiku eti mke wake amezidiwa anataka v8 ya mbunge ampeleke hospitali
 
Mkuu najua vipo vyuo vya kufunza lugha ya kuwasiliana na mabubu na viziwi, lkn hii ya kwako ya kuwasiliana na wapumbavu umejifunza wapi?

Kuelewana na mtu mpumbavu kama huyu kwangu ingekuwa kazi sana, lkn kwa jibu lako naamini sasa na yeye ameyaona maendeleo ya Mnyika Ubungo. Tafadhali tu mbavu zangu

Mi Nadhani wewe rudi tena darasani, maana hujaelimika na hujui Dunia Kama ni ya duara. Kamuulize Mnyika mwenyewe akutajie maendeleo aliyotuletea Ubungo uone Kama hayo uliyoyataja yamo

msome jamaa hapo juu utaelewa nimetumia njia gani kumwelewesha mleta mada
 
Maendeleo mengine jaman ajafanya kama ujenz wa barabara ni mipango endelevu ya serikari yetu bwana.
Ila nashukuru kwa maelezo yenu mana mi sijuagi analofanya ndo mana niliomba msaada wa kupata maendeleo alioyaleta ila still hakuna la maana

Watu kama wewe ukijulikana 2015 ni wakuwashughulikia maana ndo wapinga maendeleo ya nchi hii kwa kutaka kuendeleza usultani wa CCM. Huna hata aibu, unaweza kumkosoa mbunge kama mnyika kweli? Kweli kuna mbunge kama mnyika? Unaweza kumlinganisha na nani kwenye hili bunge la sasa! kazi ya mbunge siyo kutoa fedha zake mfukoni na kununua madawati sijui ambulance sijui mashuka hospitalini, kuleta magreda ya kupalua barabara. Kazi ya mbunge makini ni kuwakilisha hoja za jimbo lake mbungeni na kuzisimamia ili zitekelezwe na kama hazitekelezwi anarudi kwa wananchi kuwapa sababu na wananchi ndo wanaamua wachukue hatua gani kudai haki hiyo. Halafu usichangeanye kazi za mbunge na za diwani vitu vingi sana viko chini ya diwani kama barabara za mitaani hizi ni kazi za serikali za mitaa.

Kumbuka jimbo la ubungo lina madiwani na viongozi wa mitaa kutoka ccm hivyo unapoona mtaani kwako hakufanyiki kitu muulizae mjumbe wako wa mtaa ndiyo anawajibu wa kutoa majibu. Tatizo tulilonalo wa bongo tunamwangalia mbunge tu tuna viaacha hivi vijamaa vya serikali za mitaa vinatanua tu bila kazi huku tulivipatia kura.

Anza na mjumbe wako wa mtaa kwanza kabla hujafika hata kwa diwani au mbunge na huo ndiyo utawala bora,
 
Back
Top Bottom