Mnaopanga kuandamana tena

Mnaopanga kuandamana tena

Mtufikirie na sisi tunaoishi Maisha magumu...tunaoshindia maandazi na maji na bado na bado tunategemea kudra wengine tunajitegemea huku tuna challenge za kiafya

Vikiumana huko mtatuua wenzenu🥲
Hii nchi siyo ya wananchi wake kushindia maandazi na maji. Maandamano ndiyo yatakayo sababisha wahuni kutoka madarakani, na hivyo maisha kurejea kwenye hali yake ya kawaida.
 
Toa location tuje tukusaidie kwenda kwa Mungu moja kwa moja maana huko Imeandikwa Hakuna Njaa ni mwendo wa kutafuna Bikra 72
Imeandikwa wapi?
Hakuna maandiko kama hayo kwenye bible.
Mpelekee sheikh wako huko
 
Mtufikirie na sisi tunaoishi Maisha magumu...tunaoshindia maandazi na maji na bado na bado tunategemea kudra wengine tunajitegemea huku tuna challenge za kiafya

Vikiumana huko mtatuua wenzenu🥲
Ulichokizungumza ni sahihi kabisa

Na watanzania wengi wako hivyo ndio maana wengine wanatumia fursa ya kuvunja maduka na ATM wapate chochote kitu badala ya kuandamana kufikisha ujumbe wao

Wengi wamekutukana na kukupa majibu ya hovyo hii inaonesha jinsi gani watu wa aina hii hata wakipata uongozi wanaoupigania watadharau piah sauti za wananchi wao wanyonge

Mmoja hapo amekutukana tusi kali sana halafu ni Diaspora huyo yeye hayupo hapa Tanzania hana experience ya ile lock down tuliokutana nayo hajui ile situation umelala ndani na risasi zinagonga kwenye ukuta wa nyumba tena usiku wa manane

Walio na vyoo vya nje walijisaidia kwenye ndoo hata ndani kutoka mtu unaogopa usije ukala chuma

Safari hii haitokuwa na shida sana kwa sababu cha kwanza watu watakuwa wachache sana hata naowafahamu ambao walitoka mwanzoni hakuna anayetamani kurudi tena

Wamama wanawasihi waume zao hiyo siku hamna kutoka kwenda popote na wengi washaanza mipango kwenda vijijini kusalimia

Hiki kipindi kifupi jichange change usogee mahali ambapo unahisi hapatokuwa na kashikashi au hata kukiwa na kashikashi basi kuwepo na mahitaji ya kujitosheleza either iwe kwa ndugu au hata marafiki
 
Dah!! Mama mkwe nakuelewa tena nakuelewa sana, lakini kinachoniuma zaidi ni hawa walio madarakani, je wanawakumbuka watu kama nyinyi, kodi zetu wanazochukua na mali zetu za asili zilizojaa nchini, zinakunufaisha mkwe wangu kipenzi..
Kila jambo lina athari zake..
Pole sana mkwe, sitamani uteseke hope unajua hilo.
 
Back
Top Bottom