Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mungu wangu

Mkuu nimepita hapo saa nane kasoro kutokea kwa mzee kiki nikiwa na mamsapu... bahati nzuri palikua bado shwa ila gari zilivyokaa ilikua ni hatari kwani both sides of the road palikua pamejaa

madhani kuna haja ya kuangalia usalama siku za weekend hapo, hii si mara ya kwanza
 
Daaah,mkuu yaani ilikuwa balaa sana..kuna mtu alikuwa na prado anatoka mwenge anaenda mjini,speed kubwa na kilaji juu..sasa hizi gari zilikuwa zimepaki pande zote.sasa kuna mtu alikuwa anarudi reverse na pajero..kwa hiyo hii ilikuwa inarudi reverse ilikuwa ya kwanza kugongwa ndipo prado ika loose control na kugonga magari mengine 4..kujeruhi na kuua walinzi waliokuwa wakilinda magari ya barabarani..
 
pole sana wafiwa.... wiendi na mwisho wa wmezi vinatoa sadaka roho za watu
 
Jamani ajali mbaya sana imetokea nje ya zhonghua garden mida hii.yaani gari 5 zimegongana kwa mpigo na karibu watu 3 wamepoteza maisha..ni habari ya kuhuzunisha sana..

Inasikitisha.

Grants 43% alc; Valeur 42% alc;
 
Mwenyezi Mungu Awaweke mahali pema waliopoteza maisha, awafariji wafiwa na awape nafuu ya haraka majeruhi. Naomba kuelimishwa hiyo Zhongua Garden ndiyo wapi? Kwangu jina Zhongua lasomeka kama la Kichina!!!
 
Inasikitisha.

Grants 43% alc; Valeur 42% alc;
pombe ni chanzo cha ajali nyingi sana na nadhani kuna haja ya law enforement officers kupewa nguvu ya kusimamisha gari randomly usiku na kupima alcohol levels

wakifanya hivi kwa miezi mitatu, ulevi utapungua
 
Kuna kila sababu ya kupitia upya sheria za barabarani, watu wanaosababisha ajali kwa uzembe wanyang'anywe driving licence na wasiruhusiwe kuendesha gari maisha yao yote, hiyo itawaogopesha kidogo madereva.
 
Ah masikini poleni sana wafiwa na wahanga.... kusema kweli pale upakiji wa magari si mzuri kabisa yaani barabara inazibwa kabisa jamani. Duh walinzi masikini!!
Mungu aziweke roho za marehemu husika mahali pema peponi. Amen
 
pombe ni chanzo cha ajali nyingi sana na nadhani kuna haja ya law enforement officers kupewa nguvu ya kusimamisha gari randomly usiku na kupima alcohol levels

wakifanya hivi kwa miezi mitatu, ulevi utapungua

Ushauri mzuri kutoka kwa mtumiaji wa Grants!

Dont Drink and Drive. Pole kwa wahanga wote. RIP marehemu wote! Amen
 
pombe ni chanzo cha ajali nyingi sana na nadhani kuna haja ya law enforement officers kupewa nguvu ya kusimamisha gari randomly usiku na kupima alcohol levels

wakifanya hivi kwa miezi mitatu, ulevi utapungua
kwa stail hiyo mbona watakamatwa wengi!
 
Mungu alaze roho za marehemu mahali pema peponi.

Jamani ulezi mbona unakwu chanzo cha mambo mengi? mtu yuko radhi aacha kunywa soda, ila siyo pombe. Mungu atutie nguvu jamani. tupunguze kunywa.
 
valuer hoyeeee, ila kunyweni kwa kiasi bila kuathiri bongo zenu, kumbukeni pia pombe sio maji
 
Ndugu zangu nimepata taarifa kwamba kuja ajali mbaya imetokea maeneo ya kinondoni na magomeni njia ya kawawa ambapo roli limegonga na kusababisha magari mengine 4 kugongana .

Sijapata taarifa zaidi ya majeruhi wala vifo au uharibifu wa mali

Ila kuna foleni kubwa maeneo hayo ndio maana magari yamesimama muda mrefu njiani
 
Ajali yaua watano, vibaka wapora maiti


na Francis Godwin, Iringa


amka2.gif

WATU watano wamekufa papo hapo na mmoja kujeruhiwa vibaya katika ajali mbili tofauti zilizotokea wilayani Mufindi na Wilaya ya Iringa Vijijini jana, ikiwemo lori lililokuwa limebeba Mbolea, huku vibaka wakipora maiti kila kitu walichokuwa nacho.
Katika ajali ya kwanza iliyotokea juzi majira ya saa 2 usiku katika Kijiji cha Kinegembasi Wilaya ya Mufindi, kwenye barabara ya Iringa –Mbeya, lori lenye namba za usajili T 144 BCU aina ya Scania lililokuwa limebebea mbolea tani 32, liliacha njia na kupinduka na kusababisha vifo vya watu watatu akiwamo mwanamke mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja.
Wakizungumzia ajali hiyo, ndugu wa jirani Ibrahim Hamis, alisema lori hilo, lilikuwa limebeba mbolea aina ya UREA kutoka jijini Dar es Salaam kwenda nchini Malawi.
Alisema katika lori hilo, kulikuwa na watu wanne akiwemo dereva msaidizi wake na utingo pamoja na mwanamke mmoja ambaye ni abiria aliyekuwa amepewa msaada wa usafiri kutoka Mafinga.
Aliwataja waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni Gulam Mahamudu shambe, Foward Shwambe na mwanamke mmoja ambaye jina lake halifahamiki, anayekadiriwa kuwa na miaka kati ya 20 na 22, huku utingo wa lori hilo akijeruhiwa vibaya.
Hata hivyo, alisema kuwa lori hilo lilikuwa limesheheni mbolea likitokea Dar es Salaam kwenda Malawi na kuwa mbolea yote iliyokuwemo katika gari hilo imeibwa na vibaka na kubaki mifuko isiyozidi kumi pekee. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Evarist Mangalla alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo pamoja na ajali nyingine iliyosababisha vifo vya watu wawili iliyotokea katika kijiji cha Kivalali, kwa kuihusisha daladala yenye namba IT 2345. Katika ajali hiyo, iliyotokea jana majira ya asubuhi na kusababisha vifo vya watu wawili, akiwemo Swedy Samwel (40) na mtu mmoja mwanamume ambaye jina lake halijafahamika
chanzo:Tanzania daima
 
Back
Top Bottom