Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

we unategemea nini mali hizo atachukua nani kama polisi wamaechelewa kufika eneo la tukio ? kufa kufaana ! binadamu wa sasa wengi hawana utu, mali mbele utu nyuma usitegemee kusaidiwa !
 
WanaJF ninajua hii topic ilishawahi kujadiliwa lakini sinabudi kuileta tena kama njia ya kuzidi kuliangalia kwa undani tatizo hili. Watu wanakufa kila siku kwa ajari za barabarani lakini sioni kama kuna mikakati ya maana inayowekwa kupunguza idadi ya vifo.
Nadhani baada ya malaria na ukimwi ni ajali za barabarani ambazo zinafuatia katika kuchukua maisha ya watanzania. Kwa nini hakuna mikakati ya kupambana na suala hili kama tunavyofanya kwa malaria na ukimwi.
Swala la kujiuliza ni kwa nini nchi kama TZ yenye idadi ya watu 40m inavifo vingi vya barabarani kuliko Marekani yenye watu zaidi ya 250m. Je madereva wanaoendesha magari wanazingatia sheria za barabarani au barabara zetu na alama zake hazifai?
Juzi nilipigiwa honi kwa nguvu sana na dereva wa gari la serikali nikiwa nimesimama kwenye Zebra Crossing mitaa ya Kunduchi mtongani nikiwapisha watoto wavuke barabara. Je kama dereva wa serikali hajui la kufanya kwenye Zebra crossing, tutapona?
Waungwana nipe mawazo yenu.
 
Sababu kubwa ni uzembe wa madereva: wengi wanajifanya wana haraka sana kwa hiyo hawajali sheria/alama za barabarani; wengine hawazijui (baadhi ya) sheria za barabarani - kumbe wanazivunja. Kwa kifupi madereva wengi hawana UTU wakiwa usukanini mwa magari yao. Pengine hii ni hulka ya watanzania wengi. Shida nyingine ya ajali ni magari mengi mabovu: hayana breki nzuri/imara. Haya pia yanakuwa chanzo kikubwa cha ajali.
 
Hii imerudi tena, haya. Kwa kiasi kikubwa ni barabara na si ubovu tu bali na jinsi zilivyo ni tatizo. Kinafuata madereva kutokuwa waangalifu, kwa sababu wangekuwa waangalifu japo kidogo tu ingepunguza hizi ajali. Walioko Ujerumani wataungana nami, ukiwa unataka kuvuka barabara na ukaigeukia iwe ni kwenye zebra cross au sio magari yote yatasimama. Binafsi nilipata taabu sana wakati fulani kwani sikuwa nimelijua hili, na kila nilipokuwa nikiangalia upande wa barabara nikashangaa magari yanasimama ndio nikajua nawapa watu taabu kwa kunisubiri nivuke kumbe mimi nina shida yangu nyingine. Kwa hiyo utaona ustaarabu na uangalifu unahitajika.
Kuhusu barabara, hapa ndio kwenye muskel mkubwa. Barabara zetu karibu zote zipo chini ya kiwango na ndio maana barabara inajengwa leo kesho watu wanafikria kuweka matuta. Wakati kabla ya kujengwa ilikuwa yote yawe yamekwisha onekana na ufumbuzi umeshapatikana, ikiwa ni pamoja na kuzuia ajali na jinsi gani waendao kwa miguu watavuka. Karne ya 21 tunajenga barabara tunayoita high way na matuta tangu mwanzo hadi mwisho?, na tusipofanya hivi watu wanagongwa kwa kwenda mbele.
 
Vyote vinachangi mfano:-
Dereva hana ujuzi wakujua nini kinasababisha ajali hivyo anawezakuendesha bila kujua wapi panaweza kusababisha ajali.
Pili uzembe upo kwa inspector's vehicles wote uwezikuwa unakagua gari kwa mwaka mara moja!!
Ubovu sa barabara wakandalasi wanachakachua rami naviwango vya kokoto resho siyo na mayokeo unakuta rami nyingi kuliko kokote hivuo jua,mvua vikipiga panateleza,
 
Kuna ajali mbaya ya basi la Harambee lililokuwa likitokea DSM kwenda Moshi usiku huu maeneo ya Mazinde huko Korogwe mkoani Tanga! Zipo taarifa za vifo na majeruhi kibao! Tunaendelea kufuatilia na taarifa zaidi tutawajulisheni!
 
Thanks for the info, I know the owners let me call them then will keep you posted.
 
harambee???? Thanx kwa taarifa ndg yangu...............
 
OMG nimeshtuka sana, kuna ndg wengi wanasafiri kuelekea hm kwa siku kuu za mwisho wa mwaka.
 
Jamani poleni wafiwa na majeruhi. Tafadhalini madereva mwisho wa mwaka huu jamani tulindieni uhai wetu. Mwendo kasi unaua. Abiria tujitahidi kukemea uendeshaji mbaya wa madereva............... roho ni moja tulizopewa na mwenyezi MUNGU and we only live Once.

N.b. Simaanishi kuwa dereva alikuwa mwendo kasi hapana kwa kuwa sijajua chanzo cha ajali. Ni caution tu.
 
May the soul of departed rest in peace. Let's be cautious wanajamii and pray to our Allah to keep us safe
 
Kuna habari kuwa basi la super feo likitoka songea kwenda dar limepata ajali.Ajali hiyo imetokea katikati ya songeea na njombe.
Kuna habari zimezagaa kuwa kuna watu wamefariki hapohapo idadi inayotajwa ni kati ya wawili mpaka sita .Majeruhi waliopo hospitali ya mkoa songea wanazidi kumi.
Mwenye habari zaidi atujuze .
 
Back
Top Bottom