Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mie nimewahi shuhudia jamaa akigida Safari huku akiwa anaendesha live morogoro road na huku ana mobile anaongea. Ilikuwa rahisi kumuona kwani tulikuwa katika foleni ta Ubungo. Na hiyo ni pombe. Je Unga ?
 
Huyu jamaa aliyefanya uharibifu atakuwa alikesha Casino hapo NA! Hainijii akili jinsi gani gari inaweza kusababisha ajali mbaya sehemu kama hiyo. Alihisi amefika nyumbani kwake!

Pole majeruhi
 
Heshima mbele wakuu wa jamvi.Nimeonelea niwajuze kwa uchache na kipicha zaidi juu ya ajali iliyotokea mida ya saa moja ikihusisha RAV4 kugonga kibanda cha walizni na kujeruhi walinzi pamoja na kufanya uhalibifu wa ATM room.

Samahani kwani mwanga wa picha ulikuwa mdogo na kwa hivyo zitaonekana kwa uhafifu ila nilifika kwa kuchelewa kidogo na kwa ufupi ndiyo hayo kama kutakuwa na mtu mwenye taarifa zaidi atujuze ila gari ilitokea mitaa ya baharini ikienda maktaba na ghafla ikaingia kwenye ATM ila nahisi dereva alikuwa amelewa.

Tafadhari Mode ikisha somwa waweza kuifuta

Walinzi wamepelekwa hospitali

Nawakiliwa
Bongo mdebwedo sana!
 
Ng'ombe aliyetumbukia bwawan.jpg
Ng'ombe aliyetumbukia bwawani akiokolewa huko Motcombe, Dorset
NG’OMBE mmoja aliyekuwa amepotea alijikuta akiogelea katika bwawa moja huko Dorset, Uingereza, baada ya kukimbia kutoka katika shamba moja.

Haikufahamika ni kwa nini ng’ombe huyo alikimbilia kwenye bwawa hilo, lakini watoa huduma wa sehemu hiyo walilazimika kufanya juhudi za kumwokoa ambazo zilichukua masaa kadhaa kumtoa majini.
Kioja hicho kilitokea asubuhi jana, wakati mnyama huyo aliyepewa jina la Daisy na waokoaji alipotoroka kutoka shambani huko Motcombe, na kuanza kuzurura katika eneo la nyumba ya jirani.
2.jpg
Daisy akiwa ameokolewa.
Kikosi cha zimamoto kutoka Shaftesbury, kundi la kuokoa wanyama kutoka Poole, daktari wa wanyama na gari maalum la kufanyia kazi hiyo, vilitumika katika operesheni hiyo.
Ofisa wa zimamoto Michael Stead, aliyefika kwenye eneo la tukio, alisema ng’ombe huyo aliyekuwa hajafikisha hata umri wa mwaka mmoja angeweza kukaa majini humo kwa masaa kadhaa bila kudhurika.

“Kitu cha ajabu, alionekana kuwa mtulivu,” alisema Stead, “lakini alifanya matata kidogo tulipotaka kumfunga kamba ili kumtoa.”
Hata hivyo, Daisy alibidi kudungwa madawa ya usingizi kabla ya kuondolewa majini na kurudishwa kwa tajiri wake.

“Alionekana mchovu kama vile amelewa, bila shaka kwa kushangaa na kile kilichokuwa kimemtokea,” alisema ofisa mmoja wa zimamoto na kuongeza: “Nimeshiriki katika matukio kadhaa yanayohusu ng’ombe lakini hili limenishangaza. Hata hivyo, tunafurahi hakupata madhara yoyote.”
 
Sijui hapa bongo ukidumbukia majini kama unaweza kupata msaada wa haraka na timu ya wataalamu kama aliyopata huyu ngo'mbe
Lazima nikiri kuwa ngo'mbe huyu ana bahati kuishi Uingereza simaanishi mimi sina bahati kuishi TZ
Mix with yours
 
kama ATM imeharibika wahi mchote fedha zenu hapo
 
Basi la Batco limepata ajali karibu na kijiji cha Nyanguge likielekea mjini Mwanza, watu kadhaa wamejeruhiwa.
 
ajali%20migo.jpg

Mmoja wa wananchi ambaye jina lake halikuweza kufahamika, akiteremka kwenye moja ya magari yaliyopata ajali eneo la Magomeni Mikumi, jijini Dar es Salaam jana.Magari hayo ni lori lenye namba za usajili T267 APE, Toyota Hiace lenye namba T189 AJG na Benz T587 AAC. Katika ajali hiyo iliyohusisha magari saba, dereva wa lori alipata majeraha na kukimbizwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu.
 
Kuna Lori limepinduka katikati ya Daraja la Tegeta: haionyesha kama kuna Majeruhi. Kuna jitihada za kuliondoa zinaendelea. Kwa wale wanaoishi maeneo ya Tegeta hadi Bagamoyo watahangaika sana kuja katikati ya Mji

Alternative route: Kuingilia Tegeta Nyuki na kutokea Maeneo ya Kunduchi au Barabara ya IPTL
 
Ndugu wana JF, Tumekuwa tukisikia na kushuhudia ajali mbaya sana zikitokea katika maeneo mbalimbali ya Tanzania kila kukicha. Ajali hizi zimekuwa zikikatisha maisha ya watanzania wengi ambao ni nguvu kazi muhimu kwa maendeleo ya taifa letu, na kuacha wengine wakiwa na ulemavu wakudumu wa viwango tofauti.
Tumeshuhudia Tume zikiundwa kuchunguza vyanzo vya ajali hizi, huku wanatume wakilipwa fedha lukuki za hawa wahanga!!!, Lakini bado tunaendelea kushuhudia hizi ajali zikitokea kila kukicha. Je!! Ni nini chanzo chake!!,Je uzembe ni hulka ya watanzania? Au kuna tatizo la kimfumo?. Na Nini kifanyike ili kupunguza tatizo hili, Kwa maana sisi sote ni wahanga,Waliokwishapata ajali wao wametangulia tu, we are all potential victims!!. Au tunaamini kuwa ni mipango ya Mungu????
 
Siyo mzizi mmoja. Ni mizizi: magari mabovu, udreva usio na viwango, corruption kwa wadhibiti wa usalama barabarani, uzembe wa madreva, barabara mbovu au nzuri sana, etc, etc. Ni mizizi mingi!
 
nguvu za giza (kafara) +backwardness (leseni bandia, magari mabovu n.k)+ulevi = ajali nyingi
mix with yours
 
Kuna habari kuwa barabara ya Bahari Beach umefungwa na wananchi kutokana na hasira za kuuwawa kwa watoto wawili wa shule ya msingi iliyopo karibu na hapo.
Ajali nimetokea pale Kunduchi.
Wenye shughuli sehemu hizo chukua tahadhari!!!
 
Mimi naishi maeneo ya kule....ajali za waenda kwa miguu kugongwa zinatokea mara nyingi sana
 
Back
Top Bottom