Mungu uwape pumziko la milele marehemu na wale walioumia uwajalie kupona haraka....hizi ajali ni madereva, bara bara zetu ama magari mabovu, ama ni machanganyiko wa vyote? Kila kukicha ajali tu ajali....
Wanasema watu wamekufa lakini wanasema kati ya watau tisa na kumi
Ripoti za hivi punde zinasema waliopoteza maisha ni 16
Jamani poleni sana. Eneo hilo nalifahamu vizuri. Liko barabara kuu iendayo Moshi kutokea Arusha. Pana mteremko mkali sana pale. It is about 7 kilometers from AICC. Actually stretch hiyo kutokea Kwangulelo kupitia kwa mrefu hadi Tengeru ni black spot haswa. Wakati Magufuli akiwa waziri wa Ujenzi, sisi wakazi tuliwahi kumuomba iwekwe matuta TANROADS wakakataa kwa kutoa majibu ya kisheria. Lakini barabara hiyo hiyo uingiapo tu mkoa wa Kilimanjaro matuta hadi njia panda ya Himo. Yaani double standards at its best. Sielewi sielewi. It is very sad indeed.
Huu mto una mdudu gani jamani! Du Poleni sana watu wa arusha na mikoa jirani na watnzania wote kwa ujumla
Ajali za namna hii zimekuwa zikitokea mara kwa mara huku serikali na vyombo vya usalama vikitupa lawama nyingi kwa madereva na watumia barabara wengine kuwa waangalifu wakiwataka wafuate sheria za usalama barabarani.
Mimi nina mtazamo tofauti kwenye vyanzo vya ajali hizi. Sheria zipo sawa na ni lazima zifuatwe ila ajali kama hizi zinaweza epushwa kwa kuboresha barabara. Barabara zetu ni za karne ya 18 yaani "Two way one lane"(barabara moja inatumiwa na magari ya pande zote mbili. Hapa nina maana kama hakuna gari inayokuja mbele dereva anaweza kuendesha upande wa magari yanayokuja. Wao wana sema ni uchumi mbovu. Hivi kweli hatuwezi kujenga "Two way two lane"(Chukua mifano ya Nyerere, kawawa, Mandela na morgoro Road mpaka Mlandizi) Roads?. Jibu ni dogo tunaweza ila hatuna utashi kwa kutawaliwa na Tamaa za kifisadi.
Na kuna Taarifa za kuaminika kuwa hizi ajali zinatumiwa na watunga sera katika kuhalalishia kukinga bakuli la kuomba misaada ama wakisingizia kuzipunguza au la. Kuna wakati nilikuwa nafanya utafiti fulani ambao ulinilazimu kupata details za ajali nilihangaishwa pale traffic makao makuu na mmoja wa askari akaniambia hizi details hutoka kwa kibali maalum.
Sasa tumefika mahali tuangalie zaidi maisha na kutupiana lawama, kama ni uzembe wa barabarani kila sehemu duniani upo ila wenzetu wamechukua tahadhari sana kiasi kwamba uzembe wa dereva isiwe adhabu ya kifo kwa watu wasio na hatia.
Mimi nina mtazamo tofauti kwenye vyanzo vya ajali hizi. Sheria zipo sawa na ni lazima zifuatwe ila ajali kama hizi zinaweza epushwa kwa kuboresha barabara. Barabara zetu ni za karne ya 18 yaani "Two way one lane"(barabara moja inatumiwa na magari ya pande zote mbili. Hapa nina maana kama hakuna gari inayokuja mbele dereva anaweza kuendesha upande wa magari yanayokuja. Wao wana sema ni uchumi mbovu. Hivi kweli hatuwezi kujenga "Two way two lane"(Chukua mifano ya Nyerere, kawawa, Mandela na morgoro Road mpaka Mlandizi) Roads?. Jibu ni dogo tunaweza ila hatuna utashi kwa kutawaliwa na Tamaa za kifisadi.
Na kuna Taarifa za kuaminika kuwa hizi ajali zinatumiwa na watunga sera katika kuhalalishia kukinga bakuli la kuomba misaada ama wakisingizia kuzipunguza au la. Kuna wakati nilikuwa nafanya utafiti fulani ambao ulinilazimu kupata details za ajali nilihangaishwa pale traffic makao makuu na mmoja wa askari akaniambia hizi details hutoka kwa kibali maalum.
Sasa tumefika mahali tuangalie zaidi maisha na kutupiana lawama, kama ni uzembe wa barabarani kila sehemu duniani upo ila wenzetu wamechukua tahadhari sana kiasi kwamba uzembe wa dereva isiwe adhabu ya kifo kwa watu wasio na hatia.
Pale hapahitaji matuta, utawekaje matuta kwenye mlima/mteremko mkali, zaidi ya hayo kuna kona na daraja! Basi matuta yakawekwe pia Kitonga, Ngorongoro au hata Sekenke!
Kinachohitajika ni alama za barabarani na madereva waangalifu.
Marehemu wapumzike kwa amani. Poleni majeruhi na wafiwa.