Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Ajali nyingi zinasababishwa na madereva wasiostahili kuwa barabarani kwa kuwa hawana leseni, hawaoni vizuri n.k. Halafu Askari wa barabarani nao wameweka mbele rushwa badala ya kuhakikisha usalama wa Watanzania barabarani. Matokeo yake wakishapewa takrima yao basi wanamuachia dreva asiyestahili kuwa barabarani au gari lisilokuwa na hadhi ya kuwa barabarani.

Tumvaline njuga Waziri wa mambo ya Ndani L. Masha na wizara yake ili wapunguze ajali za barabarani ambazo zimeua na zinaendelea kuua WaTanzania wengi wasio na hatia.
 
Ajali nyingi zinakwepeka. Naambiwa ukitoka Dar au Morogoro kuelekea Mbeya, gari kugonga ng'ombe, mbuzi, n.k ni jambo la kawaida kutokea.




Hii inaleta matumaini kidogo. Ajali ilitokea Jumatatu wiki hii

Imetolewa mara ya mwisho: 04.12.2008 0002 EAT

Dereva wa Sumry apandishwa kizimbani

Na Francis Godwin, Iringa

JESHI la Polisi wilayani Mufindi limemkamata na kumfikisha mahakamani dereva wa basi la Sumry aina ya Nissan namba T 293 ASA, Bw. Ibrahim Ng'umbi (44), mkazi wa Soweto, Mbeya akikabiliwa na mashitaka 17 ya usalama barabarani.
Miongoni mwa mashitaka hayo ni la kusababisha kifo cha abiria wake mmoja Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP), Bw. Ramadhan Kalowa na kujeruhi abiria wengine 14.

Pamoja na kukamatwa kwa dereva huyo, Polisi pia inamsaka mmiliki wa kampuni ya mabasi ya Sumry na wa ng'ombe aliyegongwa na kusababisha ajali hiyo, ili nao wafikishwe mahakamani.
Dereva wa basi hilo ambalo lilitumbukia katika korongo juzi baada ya kugonga ng'ombe eneo la msitu wa Sao Hill Mafinga, ambaye alikuwa amekimbia baada ya kusababisha ajali hiyo, alijisalimisha kwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Mufindi (OCD) Bw. Peter Kakamba, jana saa tatu asuhuhi.
Mwandishi wa habari hizi alishuhudia jana saa 4 asubuhi askari wa kituo cha Mafinga, wakiongozwa na Mwendesha Mashitaka wa Polisi, Bw. Yohana Mjengi na kumfikisha mtuhumiwa huyo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Mufindi, Bibi Mary Moyo, kusomewa mashitaka 17.
Bw. Mjengi alidai kuwa mtuhumiwa anadaiwa kuendesha gari kwa uzembe na kusababisha kifo cha abiria mmoja na madai mengine 14 ya kuendesha gari na kusababisha majeruhi 14 waliokuwa kwenye basi hilo.
Anadaiwa pia kushindwa kuripoti Polisi kwa muda wa saa 24 tangu ilipotokea ajali hiyo na pia kuendesha gari kwa uzembe na kusababisha uharibifu wa gari hilo mali ya kampuni ya Sumry ya Sumbawanga.
Alidai kuwa mtuhumiwa alitenda makosa hayo Desemba mosi mwaka huu saa 4.15 jioni kwenye barabara kuu ya Iringa–Mbeya wakati basi hilo likitoka Dar es Salaam kwenda Tunduma, Mbeya.
Mtuhumiwa alikana mashitaka yote na upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na hakuna pingamizi la dhamana.​
 
Alidai kuwa mtuhumiwa alitenda makosa hayo Desemba mosi mwaka huu saa 4.15 jioni kwenye barabara kuu ya Iringa–Mbeya wakati basi hilo likitoka Dar es Salaam kwenda Tunduma, Mbeya.
Hivi jioni uanzia saa ngapi na kwisha saa ngapi?
 
Kuna ajali mbaya imetokea Arusha kama dakika kumi zilizopita ambapo gari ya Coca cola semi trela likitokea Moshi limetumbukia katika mto Nduruma baada ya kugongana na Costa na Hiece. Costa inaning'inia nusu mtoni nusu barabarani. Habari zaid baadaye
 
Wajameni kuna gari tano zimeanguka mto NDURUMA Arusha sasa hivi....
Ndio naelekea eneo hilo.
Nitawataarifu baadae
 
Mto Nduruma uko nje ya mji wa Arusha eneo karibu na kwa mrefu.
Niko eneo la ajali hali mbaya sana askari wa usalama barabarani wako hapa kudhibiti vurugu,ni vigumu kupata taarifa sahihi ila inakadiriwa watu 20 wamefari.
 
Wanasema watu wamekufa lakini wanasema kati ya watau tisa na kumi
 
Demo, asante kwa info. Tunaomba pia utupe angalau kwa juu juu tu hiyo ajali imehusiaha magari gani na gani.

Mungu awasaidie majeruhi woote wapate kurecover mapema.
 
Huu mto una mdudu gani jamani! Du Poleni sana watu wa arusha na mikoa jirani na watnzania wote kwa ujumla
 
Poleni wana Arusha na Watanzania kwa ujumla Mugu aziweke mahali pema peponi roho za marehemu na majeruhi wapone kwa haraka.
 
Ni ajali mbaya kati ya ajali zilizowahi kutokea hapa nchini, Watu wamepasuka hovyo hovyo kwa sababu ya kujirusha kutoka kwenye costa inayoning'inia darajani, taarifa zisizo rasmi ni watu sita tu wamenusurika kwenye basi la costa. barabara bado imefungwa kwa muda. tusubiri taarifa rasmi ya kamanda wa mkoa wa Arusha.
 
Mungu uwape pumziko la milele marehemu na wale walioumia uwajalie kupona haraka....hizi ajali ni madereva, bara bara zetu ama magari mabovu, ama ni mchanganyiko wa vyote? Kila kukicha ajali tu ajali....
 
Ajali imesababishwa na nini?

imetokea muda gani?

Askari wamefika hapo ndani ya Muda?

Vikosi vya kuokoa watu vipo hapo?

Je watu wa Zimamoto wapo?

Poleni sana ambao mtakuwa mmeguswa na ajali hii
 
Back
Top Bottom