Mliokuwa mnafikiri miradi ya Hayati Magufuli ni halalisho la kuua demokrasia, hili la Bandari litawasaidia kujua gharama ya demokrasia

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,034
144,387
Watu wenye akili, werevu na wazalendo walipokuwa wanalilia demokrasia wakati wa Mwendazake, walipingwa kwa hoja dhaifu kama vile demokrasi inachelewesha maendeleo na kwamba sasa tumepata kiongozi anaeweza kutuvusha na kuwa demokrasia ya kuchagua na kuchaguliwa haina maana na hata katiba bora nayo sio issue ya msingi tumuache Jembe apige kazi.

Leo hii tunashuhudia matunda ya kutokuwa na Bunge lilichaguliwa na wananchi wakipitisha na wakibarikia mkataba wa kuwakabidhi Waarabu waendeshe bandari yetu haya yakiwa na matunda ya Bunge la Chama kimoja linalofanya kazi yake chini ya hii katiba mbovu inayotoa madaraka makubwa kwa Raisi wa nchi hii.

Maswali:

1. Mliokuwa mnaona sahihi Mwendazake kuminya demokrasia, leo hii mna haki ya kulalamikia yaliyofanywa na hili Bunge?

2. Thamani ya kiuchumi ya miradi aliyoianzisha Mwendazake, inaweza kufidia hasara ya kiuchumi itayotokana na kuwapa wageni waendeshe Bandari yetu iwapo mkataba huo kweli utakuwa wa kimangungu?

3. Tungekuwa na uchaguzi huru, tungepata Bunge la kupitisha mikataba kama hii kirahisi kama ilivyotokea?

4. Je, bado mnaamini Mwendazake alikuwa sahihi katika misimamo yake?

5. Je, hamuoni kuwa Mwendazake alikuwa ni kiongozi asieona mbali?

6. Wafuasi wa Mwendazeke, bado hamuoni nchi hii inahitaji strong institutions na sio strong individuals?

7. Iwapo kweli Mkataba huu utakuwa mbovu kwa nchi yetu, baada ya Mama, mtu wa pili wa kulaumiwa katika hili la Bandari ni nani zaidi ya Mwendazake?

Endeleeni kupuuza madai ya katiba mpya mkifikiri mnawakomoa CHADEMA wakati huko majumbani mwenu mna watoto wadogo wataokuja kurithi hii nchi hapo baadae nyie mkiwa vikongwe au teyari marehemu.
 
Hata upinzani ungekuepo bungeni hakuna kitu kingebadilika, walikuepo wakati ATCL, TTCL, TRL, bomba la Gas na hakuna kitu walizuia.

Walikuepo wakati wa Meremeta, Richmond, Dowans, Symbions, IPTL...zaidi ya makelele hakuna kitu kilibadilika or sent iliyorudi.
 
Tufanye assumption ni kweli alikuwa mzalendo. Swali ni je, angeishi milele?
Jibu ni ndiyo.
We huoni saivi muamko wa watanzania kuwa na uchungu na nchi yao umekuwa mkubwa tofauti na pre magufuli.
Hii bandar ingeuzwa kpind cha kikwete watu wasingerise kama saivi.

So anaweza kuwa amekufa kimwili...ila spiritually ameacha spirit ya kuonesha watu TUNAWEZA bila kutegemea misaada na bakuli. Na mbegu aliyoacha ipo siku itatumika kuwaamsha waTz wengi kuupindua utawala wa mafisadi.
So in a sense,anaishi milele.
 
Hoja ni kama tungekuwa na uchaguzi huru na wa haki, Bunge linge-balance na mikataba ya aina hii isingeweza kupita kirahisi kama ilivyofanyika.
Kwaio uchaguzi huru na wa haki ni kwa JPM tu?sio kwa Mwinyi, Mkapa or JK, au hawa wengine hawakufanya uchaguzi?ht uchaguzi ungekua huru na wa haki upinzani wasingekua na wabunge zaidi ya Nusu bungeni kuweza kuzuia muswada, hizi ni hesabu za kawaida tu huitaji kua mtaalam wa statistics kulijua hili.
 
Hoja ni kama tungekuwa na uchaguzi huru na wa haki, Bunge linge-balance na mikataba ya aina hii isingeweza kupita kirahisi kama ilivyofanyika.
Na wapinzani wa hovyo tulio nao hiyo mikataba isingeweza kupita kirahisi ila ingepitishwa kwa kuwepo idadi kubwa ya wabunge wa CCM, si ingepigwa kura?

Ninyi mnojiita wapinzani sasa mna muda wa kijitafakari mwataka nini maana bado mmelewa asali mwaongea tu.

Ntaendelea kusisitiza kuwa Tanzania hakuna wapinzani wa kweli wote ni wababaishaji tu.
 
Mwendazake ali wambia mtanikumbuka walidhani wata mkumbuka kwa mazuri tu, sasa side effects za mwendazake ndo kama hizo za bandari kupewa dubai world na yale makumbaliano yanauwezo wakupewa bandari zote nchini incase akizitaka sasa tulieni dawa iwaingii vzri.
 
Nimeuliza sana kwenye hizi threads zinazohusu Hii issue ya Bandari lakini sijajibiwa mpaka sasa. !!

Labda niulize tena Je ni Suala gani lililopelekwa na Serikali bungeni ili likajadiliwe kisha bunge baada ya kulijadili wakalikataa lile suala lililopelekwa ???!! Naomba nijulishwe kuanzia bunge la kwanza la vyama vingi 1995 na kuendelea. !!
 
Nimeuliza sana kwenye hizi threads zinazohusu Hii issue ya Bandari lakini sijajibiwa mpaka sasa. !!

Labda niulize tena Je ni Suala gani lililopelekwa na Serikali bungeni ili likajadiliwe kisha bunge baada ya kulijadili wakalikataa lile suala lililopelekwa ???!! Naomba nijulishwe kuanzia bunge la kwanza la vyama vingi 1995 na kuendelea. !!
Katiba ya Warioba
 
Nimeuliza sana kwenye hizi threads zinazohusu Hii issue ya Bandari lakini sijajibiwa mpaka sasa. !!

Labda niulize tena Je ni Suala gani lililopelekwa na Serikali bungeni ili likajadiliwe kisha bunge baada ya kulijadili wakalikataa lile suala lililopelekwa ???!! Naomba nijulishwe kuanzia bunge la kwanza la vyama vingi 1995 na kuendelea. !!
Hawa ni wasindikizaji wa CCM na si wapinzani.

Muda wote huo (tokea 1992) wamekuwa wakila keki ya taifa na CCM na hamna kitu hapo.

Ni wachache sana walojaribu na twafahamu wameishia wapi.

Safari hii wamepewa asali, kimya.

Wapinzani makini walitakiwa waanzishe kampeni ya nchi nzima kupinga suala hilo (tangia Mbarawa apewe kazi 2022) hivyo hata kabla kulikuwa na haja ya kufanya mjadala na kuelimishana juu ya hii kitu DP World.

Lakini wapi matokeo yake ndo tumeona leo.
 
Tufanye assumption ni kweli alikuwa mzalendo. Swali ni je, angeishi milele?
Kwahiyo neno Mzalendo halipo kwa sababu watu hawaishi milele?

Jipambanie na tupambane sote. Acha kuhamishia magoli kwa mwendazake.

Unachotakiwa kujua ni kwamba kwa Bunge hili hili la kijinga mwendazake bado asingepeleka muswaada huo wa kinyonyaji. Kwahiyo walaumu hao Wabunge kwa sababu pia siyo watoto wadogo
 
Mwendazake ali wambia mtanikumbuka walidhani wata mkumbuka kwa mazuri tu, sasa side effects za mwendazake ndo kama hizo za bandari kupewa dubai world ...............na yale makumbaliano yanauwezo wakupewa bandari zote nchini incase akizitaka sasa tulieni dawa iwaingii vzri.
Sikumbuki kama lipo bunge lolote hata kabla ya mwendazake lililowahi kukwamisha muswada wowote ule uliopelekwa na Serikali ili ukajadiliwe Bungeni. !!
 
Nimeuliza sana kwenye hizi threads zinazohusu Hii issue ya Bandari lakini sijajibiwa mpaka sasa. !!

Labda niulize tena Je ni Suala gani lililopelekwa na Serikali bungeni ili likajadiliwe kisha bunge baada ya kulijadili wakalikataa lile suala lililopelekwa ???!! Naomba nijulishwe kuanzia bunge la kwanza la vyama vingi 1995 na kuendelea. !!
Ndio maana wenye akili wanalilia katiba mpya inayoruhusu hata Raisi wa nchi kushitakiwa.
 
Watu wenye akili, werevu na wazalendo walipokuwa wanalilia demokrasia wakati wa Mwendazake, walipingwa kwa hoja dhaifu kama vile demokrasi inachelewesha maendeleo na kwa sasa tumepata kiongozi anaiweza kutuvusha na kwamba demokrasia ya kuchagua na kuchaguliwa haina maana na hata katiba bora nayo sio issue ya msingi tumuache Jembe apige kazi.

Leo hii tunashuhudia matunda ya kutokuwa na Bunge lilichaguliwa na wananchi wakipitisha na wakibarikia mkataba wa kuwakabidhi Waarabu waendeshe bandari yetu haya yakiwa na matunda ya Bunge la Chama kimoja linalofanya kazi yake chini ya hii katiba mbovu inayotoa madaraka makubwa kwa Raisi wa nchi hii.

Maswali:

1. Mliokuwa mnaona sahihi Mwendazake kuminya demokrasia, leo hii mna haki ya kulalamikia yaliyofanywa na hili Bunge?
2. Thamani ya kiuchumi ya miradi aliyoianzisha Mwendazake, inaweza kufidia hasara ya kiuchumi itayotokana na kuwapa wageni waendeshe Bandari yetu iwapo mkataba huo utakuwa wa kimangungu?
3. Tungekuwa na uchaguzi huru, tungepata Bunge la kupitisha mikataba kama hii kirahisi kama ilivyotokea?
4. Je, bado mnaamini Mwendazake alikuwa sahihi katika misimamo yake?
5. Je, hamuoni kuwa Mwendazake alikuwa ni kiongozi asieona mbali?
6. Wafuasi wa Mwendazeke, bado hamuoni nchi hii inahitaji strong institutions na sio strong individuals?
7. Iwapo kweli Mkataba huu utakuwa mbovu kwa nchi yetu, baada ya Mama, mtu wa pili wa kulaumiwa katika hili la Bandari ni nani zaidi ya Mwendazake?

Endeleeni kupuuza madai ya katiba mpya mkifikiri mnawakomoa CHADEMA wakati huko majumbani mwenu mna watoto wadogo wataokuja kurithi hii nchi hapo baadae nyie mkiwa vikongwe au teyari marehemu.
Hii vita itakushinda ukiendelea kumuona mwendazake mbaya! Kwenye hili taka usitake mwendazake anaendelea kuwa shujaa
 
Tufanye assumption ni kweli alikuwa mzalendo. Swali ni je, angeishi milele?

Hilo la kuishi milele ni kwa Mwenyezi MUNGU tu hata shetani anamuda wake wa kutawala, kikubwa asingefanya huu uhawayani wa kiwango hiki katika kuuza Mali za Tanganyika. Hawa ndo wamefanya yao Mwendazake kaenda zake bila kuaga ndo tatzo lilipo
 
Back
Top Bottom